Hongera Raisi Samia anatumia akili kukuza uchumi na sio hisia binafsi

Hongera Raisi Samia anatumia akili kukuza uchumi na sio hisia binafsi

Kamundu

Platinum Member
Joined
Nov 22, 2006
Posts
7,823
Reaction score
10,857
Namshukuru Raisi Samia kwa kutumia akili na maarifa kukuza uchumi wetu bila kuweka mbele hisia binafsi. Hisia binafsi ni pamoja na kuweka ukanda, ukabila na uchama mbele ya Tanzania kwa ujumla wake.

1. Kitendo cha kuelewa katiba ni muhimu kwa uchumi wetu. Hasa kwenye sheria za kibiashara na uchumi
2. Kuweka uhusiano mzuri na watu wote mfano serikali haiwezi kuwa na uhusiano mbaya na wahudumu wa watalii wetu zanzibar, Arusha , Kilimanjaro na maeneo mengine halafu tukasubiri 25% yamapato kutoka utali!.
3. Uhususiano na wafanyabiashara
4. Uhusiano wa nchi na nchi kama tumeona biashara za mazao Kenya zimeongezeka
5. Kutoa uhasama na watu wote nakumbuka ilifika wakati wafanyabiashara, watu wa media na mpaka wasanii kutekwa
 
Anastahili pongezi Tausi wetu mpendwa.
 
Uchumi gani huo wakati gharama za maisha zinapanda kila siku??
 
Uchumi gani huo wakati gharama za maisha zinapanda kila siku??
Afrika nzima inashuhudia mfumuko wa bei kwa hapa Afrika ya mashariki sisi ndo tuna ahueni kidogo

So kudos Tausi.
 
Afrika nzima inashuhudia mfumuko wa bei kwa hapa Afrika ya mashariki sisi ndo tuna ahueni kidogo

So kudos Tausi.
Ondoa hilo neno sisi.

Labda wewe na familia yako.
 
Back
Top Bottom