Hongera sana Pascal Mayalla, Ndio Mwandishi Pekee Uliyemuuliza Swali Rais Magufuli

Hongera sana Pascal Mayalla, Ndio Mwandishi Pekee Uliyemuuliza Swali Rais Magufuli

Mayala alianza na mbwembwe za enzi ya "kiti-moto-akiwa na masai studio" kipindi kilikuwa kizuri DTV sijui ikawaje akakipeleka ITV na kukiulia pale, cha ajabu akauliza vitu km mwanahabari aliyebobea kwamba hajui Rais anachofanya.

Rais kamjibu vizuri tu hasa alipomrekebisha kuwa alitegemea angemuuliza kwa nini hotuba ya ubanaji matumizi aliitoa humo ndiyo Rais akatambaa hivi "katika eneo pia llinalopoteza pesa za masikini ni Bunge na kuwaomba wajipange maana yake ni nini, huko nyuma Ofisi ya Bunge ilishakuwa na desturi kuandaa hata safari za nje ambazo hazikuwa na maslahi ili mradi tu kuna watu watafaidika kwa bajeti hiyo.. ufafanuzi Mayala akaambiwa kwa kufanya hivyo hakuliingilia Bunge ni kweli Mihimili ni mi-3 ila Mihimili mmoja ndiyo unaotafuta hizo pesa alizoomba Bunge wajipange hapa ali-deal na Ofisi siyo Mamlaka ya Bunge kwa maana ya Maamuzi ya Bunge WABUNGE AT ALL nini hoja hapo wanaopokea pesa kutoka "Mhimili Serikali" ni "Ofisi ya Bunge" ambao hasa ni waajiriwa wa "Mhimili Serikali" ndiyo maana Bunge walijiongeza karudisha chenji ya Bunge la 10 na ile pesa ya "kujichana" amabayo Ofisi iliomba "Mhimili Serikali" yy akaikata bajeti ya ile sherehe kwa maana ya kuwa ni mtafutaji wa pesa hizo.

Na kikubwa alipomjibu juu ya "Mhimili Mahakama" kuwa wao walikuwa na shida kuwa kesi haziishi hawana pesa na kumweka sawa Mayala kuwa kwa "Mhimili Serikali" kuupa pesa fasta "Mhimili Mahakama" haikuonekana kuwa anaingilia huo Mhimili? Jibu liko clear yeye ha-deal na maamuzi ya "Mhimili Mahakama" kwa maana ya Maamuzi.ya kesi.

Rais hakuishia hapo bali alijitahidi kuufafanua kifalsafa kuwa "Mhimili mmoja umejichimbia chini sana"

Juu ya mikutano ya Vyama aliweka wazi kuwa Katiba isisomwe kwa kuchagua kifungu bali isomwe yote kwa tuliokuwa timamu tuliona ni jinsi gani Mawala alivyokuwa anaingizwa darasani licha ya kujifafanua kuwa ni MWANASHERIA pia,na kuongeza yeye asipokuwa na pesa kuwapa '' Wabunge - bila kubagua "ndiyo maneno yatakuwa mengi mno" but wao (Bunge na Mahakama) mishahara wanalipwa pesa yatoka wapi?" "MHIMILI SERIKALI"

Kiukweli Rais kaonyesha UMAHIRI MKUBWA kuulizwa maswali na Wahariri japo Mayala siyo mhariri.

Ila humu naona anasifiwa MAYALA vipi wale wa kutoka gazeti lile ambalo lilitolewa vyombo nje kwa KUKWEPA KULIPIA PANGO?

Wahariri wakweli leo hawakutaka kuumbuka kwa kuuliza uliza vitu ambavyo RAIS anavitolea ufafanuzi wa kina kila linapotokea jambo tata.
Shida ilikuwa mtandaoni ambako watu WAMELISHWA upupu wa kuaminishwa kuwa kila jambo la MTANDAONI NI SAHIHI.

MAYALA PASCHAL, Mzee wa Shariff Shamba kitambo a.k a. Mzee wa Kiti-Moto LEO KAJIUMBUA..eti "freelance broadcaster(mtangazaji wa kujitegemea).

SIKU NYINGINE MKISIKIA wanatakiwa WAHARIRI(EDITORS),muwe mnaelewa.

VIVA MAGUFULI, LONG LIVE MAGUFULI, ADUMU MAGUFULI.

This for Adults(bakulutu) kids(bamoke) don't touch this. [emoji106] [emoji106] [emoji106]
Alialikwa na Msigwa
 
M
Naona umemsifia sana Pascal Mayalla kuliko uhalisia wenyewe.
Kuweka kumbukumbu sawa hapa JF kuhusu Pascal Mayalla.

1/Alikuwa Mtangaziji wa DTV kipindi hicho Kipindi cha Kitimoto kikiwepo.
Kipindi hicho TVT ilikuwa haijaanzishwa. TVT ilianza kwa majaribio kuwa hewani 1999 wakati wa kifo cha Nyerere.

2/Ni kweli Pascal Mayalla ni mwandishi mzoefu sana lakini pia ni mwandishi mwenye njaa pia. Njaa huwa haiangalii uzoefu. Ukimpa chochote kizuri, Pascal anaweza kukupamba mpaka basi.

3/Mbali na taaluma ya mambo ya habari, Pascal Mayalla ni msomi wa sheria. Ni mjuvi sana wa mambo ya katoliki(Huenda alikuwa na mipango ya Upadri) na pia inazaniwa ni mtu wa usalama kwa siri.

Mkuu, with due respect, sisi wengine tunaomfahamu Paschal hatukubaliani kabisa na unayoyasema hapo juu. Give due where it belongs. Paschal ni mmoja kati ya waandishi wazuri sana hapa Tanzania. Lakini hapa wengi tunamsifu kwa sababu ameuliza maswali ya msingi kabisa. Nafiriki kama mwanasheria, ameuliza maswali yanayolenga pia kuondoa dukuduku la yeye kutoelewa (Kama Mwanasheria) mamlaka anayotumia Rais yanatoka wapi katika Katika ya nchi. Ni maswali yake ni ya msingi (Objective) kwa sababu majibu yake ni lazima yawe na references (toa quote kwenye katiba ambayo umeapa kuilinda). Lakini kwa sababu ya ubabaishaji wetu, tunataka kila kitu kuingiza siasa za maji taka.
 
Acha upuuzi huo mbumbu wa sheria ya katiba. 1.There is no absolute separation of power. 2. Rais wa TZ ana powers tatu: i.Head of state, ii.Head of the Government, iii. Head of th Armed forces. Huwezi ukamlinganisha Rais na spika au jaji mkuu. Raisi kikatiba ana mamlaka makubwa zaidi. Ktk mfumo wa Tz kikatiba mhimili wa serikali una mamlaka makubwa zaidi kuliko mihimili mingine. Kikatiba,Raisi ni sehemu ya Bunge. Kkatiba raisi huteua majaji wote. Unapoongelea separation of powers, you must also consider limitations of th same, depending on what is in our constitution which os binding.
Kwa hiyo tunaweza kusikia kuwa katika kesi zinazopelekwa mahakama ya mafisadi inaweza kutokea kesi yenye maslahi makubwa kwa nchi akaamua kuwa yeye atakuwa Jaji kwa vile yeye ni kila kitu?
 
Hongera sana kiongozi. Wewe ndo nimekuelewa sana... tofauti na wale wengine
 
IQ za watu zipimwe jaman ha ha ha ha ha ha kiklichoulizwa hakujibiwa mayalla oyeee Pascal Mayalla umekandamiza mwanawane kwa tulioenda shule tumepata feedback nyingi sana katika irrelevant answers !!hana mshauri na akiambiwa hawasikilizi watu mbaya zaidi nchi inataka iongozwe kwa utashi wake na sio katiba
 
Safiiii jamaa kauliza bila uwoga kuhoji anatumia mamlaka yapi cha ajabu anajibu kwa vijembe
kwa tulioenda shule ukifungua tu mdomo kujibu tunapata feedback nyingi sana ,kwanza jamaa anadhani nchi inaenda kwa utashi wake na sio katiba ,pili inaonyesha anashauriwa ila hawasikilizi watu ndo maana ali panic sana aliposikia swali in short ni irrelevant answers
 
Umesema ukweli!!

Hivi kweli kwa majibu hayo anaweza kumudu vyombo vya habari vya kimataifa? Naimagine Magufuli against Christine Amanpour ... hata kama atajibu kwa Kiswahili bado kijasho chembamba kitamtoka!!

Kwa ukweli maswali hayajajibiwa sawsawa zaidi ya mipasho, kejeri na vichekesho!!

Anyway, anatamba uwanja wa nyumbani ..... ajaribu ugenini tuone!! Hivi Kenya, waandishi walipewa muda kumuuliza maswali!!?
Christine Amanpour na wa aina hiyo, hao ni wa kimataifa sana. leo walikuwa wa kitaifa,,
 
Hizi ni akili uchwara kamwambie basi huyo kwanza aanze kuwanyoosha wachochezi Wastaafu akina Warioba, Mwinyi na Butiku.
Hivi mkuu BAK, kama DU kashindwa kujibu maswali ya mtu kama Paskal anayeuliza kwa nidhamu na ka woga kidogo ataweza kweli kukabiliana na waandishi makini kama wa CNN au BBC ambao huwa hawana woga wala unafiki kama alivyokuwa anajibishana nao Ben? Naanza kujisikia aibu kabla hajaenda
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Nimemsikia Pasco Mayalla akiuliza swali kwamba Rais amepata wapi mamlaka ya kuwaambia Wabunge (legislature) na Mahakama (Judiciary) waombe ruhusa kwake watakapo kusafiri?

Hoja ya Pasco ni kwamba kuna separation of powers yaani Executive, Judiciary na Legislature ambazo zinatakiwa zifanye kazi bila kuingiliana. Hilo ni sawa ila Pasco kweli hafahamu kwamba Rais wa Jamhuri ni mkuu wa dola na chini ya dola ndio unapata executive arm, judiciary arm na legisleture?

Hajui kwamba Rais wa Jamhuri ni Head of Government na wakati huohuo ni Head of the State?
KUMBE RAISI ANALIDHIBITI HATA BUNGE, SASA LINAISIMAMIAJE SERIKALI WAKATI LIKO CHINI YA RAISI.
 
Nahisi Paskall Mayalla atakuwa amejihisi vibaya sana
 
Ningelkuwa mshauri wa Rais, ningemshauri mambo mengine apige kazi kimya kimya. Nchi hii iko nyuma sana. Hapaswi kutoa uhakikisho kwa jambo lolote kwani ana miaka 10 tu. Ajenge misingi mizuri ya uchumi endelevu, lakini si kutoa uhakikisho kwamba ataacha nchi ya viwanda. Pili, ningemshauri pia awe Rais wa wote. Kwa sasa anaonekana ni Rais wa wana CCM zaidi. Hata anapoongea anaonekana wazi bado na ile "Sisi" na "Wale" huku wakati huo huo akisisitiza uchaguzi umekwisha na yeye ni Rais wa wote. Pengine anafanya hivyo kwa kuwalenga akina Mbowe, Lissu n.k, lakini kwa maoni yangu, kama Rais wa nchi, hapaswi kuonyesha kitu hicho kabisa. Hiyo awaachie akina Kinana na Sendeka.
 
mayala oyeeeeeeee zizonje ali sema baada ya kujibu swali kisanii
 
kwa jinsi alivyo jibu ni dhahiri kwamba Mh. rais anatumia madhaifu ya katiba yetu inayompa mamlaka makubwa kufanya chochote wakati wowote so kwa nn hataki katiba mpya tena ya warioba!?
 
Though alijibiwa kisiasa sana ila aliuliza swali la msingi sana
 
Umesema ukweli!!

Hivi kweli kwa majibu hayo anaweza kumudu vyombo vya habari vya kimataifa? Naimagine Magufuli against Christine Amanpour ... hata kama atajibu kwa Kiswahili bado kijasho chembamba kitamtoka!!

Kwa ukweli maswali hayajajibiwa sawsawa zaidi ya mipasho, kejeri na vichekesho!!

Anyway, anatamba uwanja wa nyumbani ..... ajaribu ugenini tuone!! Hivi Kenya, waandishi walipewa muda kumuuliza maswali!!?

..inaelekea jpm haelewi dhana ya separation of powers ya hii mihimili mitatu.

..yes, serikali ndiyo yenye vyanzo vya fedha. Lakini serikali haiwezi kutumia fedha hizo bila bajeti kupitishwa na BUNGE.

..Vilevile bunge linatunga sheria. Lakini mhimili wa MAHAKAMA ndiyo unaotafsiri sheria hizo na kutoa haki kwa wananchi.

..matatizo mengine yanatokea kwa kutokuelewa taratibu za kikatiba na kisheria. Kwa hili tunapaswa kumuombea.

Cc Pasco, Nguruvi3
 
Back
Top Bottom