Hongera serikali kusikia kilio cha tozo

Hongera serikali kusikia kilio cha tozo

Pongezi kwa waanzilishi wa tozo? Hamna tatizo walilotatua hapo.
 
Haka ni kachawa kadogo kanawinda uteuzi Kwa nguvu zote. Ona kalivyo kajinga na ka hovyo kabisa.

Kachawa tena ka damu ya mzee kama wale chawa wa zile za VIP wanafuata rangi ya pindo lake na rangi yake inakua ivo ivo. Bora chawa mweusi wa kwenye nywele nyeusi kichwani hana kigeugeu
 
Serikali kupitia Wizara ya Fedha na Mipango imetangaza kufuta tozo tatu za miamala ya kieletroniki kuanzia Oktoba Mosi mwaka huu.

Naipongeza serikali kwa kuwa sikivu na kuja na marekebisho yaliyowezesha kufutwa baadhi ya tozo. Aidha, naungana na wasomi na wabunge walioshauri kuangalia namna ya kuongeza wigo wa walipa kodi nchini, kwani ukweli ni wkamba wanaolipa kodi ni wachache kuliko wanaostahili.

Pia kama Watanzania tunapaswa kutambua kwamba hakuna nchi inayoendelea bila kutoza kodi watu wake hivyo tujitahidi kulipa kodi na tozo ili tupate maendeleo tunayoyahitaji.

Hata misaada inayotolewa na nchi washirikia wa maendeleo inatokana na kodi za wananchi wake, hivyo Watanzania wote wanapaswa kujenga utamaduni wa kulipa kodi ili fedha zake zitumike kuwaletea maendeleo.

Tanzania itajengwa na Watanzania wenyewe. Kazi Iendelee kwa sababu Mama Yuko Kazini.

Hiyo danganya toto ndio unasema sikivu? Eti tozo imetolewa kwenye muamala wa kibenki usiozidi 30,000! Katika marekebisho ya hivyo unadhani kuna wajinga wa mtawapata?

Watu wanalipa kodi, na kama ni kidogo basi ujue huo ndio uhalisia. Hizo tozo hatutaki. Kauzeni zile raslimali mnazosema tunazo mpaka wazungu wanatuonea wivu. Hayo mambo ya kulipa tizi ili mkazunguke na maVX/R hatuko tayari.

Kuanzia sasa viongozi wote waondolewe matumizi ya VX, watumie magari ya chini ya 50m, misururu ya viongozi kwenda kufanya show off ifikie mwisho. Wafanyakazi kwenye miji yenye kundi kubwa la watumishi wa serikali, waende kazini kwa mabus. Vikao visivyo na tija iwe mwisho.
 
Tozo sio mzigo, bila tozo baadhi ya miradi ya kimaendeleo haiwezi kutekelezeka, keep that in mind.

Uzeni zile raslimali, ile list ya vituo vya afya mmetoa kuhalalisha makusanyo ya tozo, ni uongo wa mchana kweupe. Tunataka jedwali la kweli likionyesha vituo vya afya vilivyojengwa wakati tozo imeanza, ikionyesha thamani ya mradi, muda wa mradi kuanza, mkoa, wilaya na tarafa mradi ulipo.

Hatuoni sababu ya sisi kukamuliwa tozo wakati tunalipa kodi kibao. Tunataka mkauze hizo raslimali mnazosema tunazo, ili kutuondolea hizi tozo zisizo na kichwa wala miguu.
 
Tozo sio mzigo, bila tozo baadhi ya miradi ya kimaendeleo haiwezi kutekelezeka, keep that in mind.

Miradi ipi nyau we[emoji23][emoji23][emoji23] madarasa? Hayo mwanzo tuliambiwa pesavza uviko au unajisahaulisha sasa hivi!!!
 
Back
Top Bottom