Hongera Simba kwa kumpa Mgunda timu kama Kocha Mkuu, apewe mshahara mnono na siyo kutumiwa kama njia ya kubana matumizi

Hongera Simba kwa kumpa Mgunda timu kama Kocha Mkuu, apewe mshahara mnono na siyo kutumiwa kama njia ya kubana matumizi

mbingunikwetu

JF-Expert Member
Joined
Feb 17, 2015
Posts
13,897
Reaction score
18,477
Tutumie uzi huu kuipongeza Simba kwa kumpatia Mgunda nafasi ya kuwa kocha mkuu wa Simba. Naamini kabisa kuwa Mgunda almaarufu kama Gurdiola Mnene ataifanyia Simba maajabu ambayo hatujawahi kuyapata kwa makocha Wazungu.

Angalizo langu ni kuwa isitokee hata kidogo kuwa simba wamempa nafasi hiyo kama namna ya kubana matumizi kwa kumpa mshahara mdogo!

Hiyo itakuwa ni laana. Kama ambavyo mishahara ya makocha wa kigeni huwa inawekwa wazi (na huu ndiyo utamaduni wa kwenye soka), tunaitaka Simba iweke hadharani mshahara wa mgunda kama Kocha Mkuu wa Simba! Tusisikie eti mnampa vi milioni 10 - 20 huo utakuwa ni uchawi na kutaka kunyanyasa makocha wazawa! Napendekeza kuwa Mgunda apewe mshahara si chini ya kocha yeyote wa kigeni aliyeifundisha Simba hivi karibuni!

Nawasilisha!
 
Wakati mwingine Watanzania huwa tunatia aibu sana! Kumpa mshahara mkubwa mtanzania mwenzako kwa kazi na ubora ule ule (wakati mwingine bora zaidi) ambao unafanywa na wazungu tunaona haiwezekani.

Huu ni utumwa!! Simba tuanze na mabadiliko haya ya fikra na kiutu! Gurdiola mnene atatufikisha mbali zaidi mashindano ya CAF kuliko walivyofanya wazungu.

Naiona nusu fainali kama siyo fainali na huenda tukabeba ndoo! Mpeni mkwanja wa kueleweka ili kumhamasisha zaidi! Tusisikie mnampa m10!! hayo yatakuwa ni matusi!
 
Shida yako nn?UTOPOLO bana Simba walipopanda Pipa kwenda Angola siku Moja kabla ya mechi mlisema wamefilisika Leo hii UTOPOLO mmeiga hakuna anayesema mmeishiwa Kwa akili hizi Yanga Kuingia Makundi mwaka ni ndoto labda mwakani
 
Kuweka hadharani mshahara sio sawa. Ila apewe mshahara mzuri iliwezekana iwe zaidi ya makocha wazawa EA
Kwa nini usiwekwe hadharani? Mbona mishahara ya makocha wazungu huwekwa hadharani? Ikiwa ni siri lazima atapunjwa!! Mbaya zaidi anaweza kupewa mshahara mdogo kuliko baadhi ya wachezaji wa kigeni na hawatamheshimu!!
 
Viongozi wa Simba wasimwonee wivu wala wasimbanie!! Mgunda atafanya maajabu!! Ni mbunifu sana!! Ameihamasisha timu na amewapa wachezaji kujiamini sana na kila mmoja anaona ana nafasi!! Tutunze hazina hii!
 
Mnene kanifurahisha juzi anadai aliwahamasisha wachezaji kuhusu game na utopolo wachezaji wakamgomea wakamwambia wanataka nusu fainali CAF game ya utopolo ni ndogo kulinganisha na malengo yao.

Sent from my Lenovo TB-7305X using JamiiForums mobile app
Tuwaachie yanga wanaokomaa na mechi za bongo hadi kutembeza bahasha! Sisi tuangalie kubeba ndoo ya CAF, ile ya ligi kuu itakuja yenyewe! Ni kama mtu aliyepanda ndege kwenda London, lakini inapitia Adis Ababa Ethiopia!! Lengo lake ni kwenda London, hapo Adis Ababa japo siyo lengo lake atafika tu maana ndege inapitia hapo!! Sasa wenzetu wana lengo la kwenda Adis Ababa halafu wanadhani watafika London kwa miujiza bila malengo hayo!!
 
Mwenye ukaribu na viongozi wa Simba wawatonye kufuatilia uzi huu!!
 
Mm nashauri apewe binti bikra kama mshahara wake atasaidia kumpunguza mwili kwa ujumla.
 
Kwa nini usiwekwe hadharani? Mbona mishahara ya makocha wazungu huwekwa hadharani? Ikiwa ni siri lazima atapunjwa!! Mbaya zaidi anaweza kupewa mshahara mdogo kuliko baadhi ya wachezaji wa kigeni na hawatamheshimu!!
Ulishawahi kusikia mshahara wa kocha mzungu unawekwa hadharani na uongozi wa timu?
 
Viongozi wa Simba wasimwonee wivu wala wasimbanie!! Mgunda atafanya maajabu!! Ni mbunifu sana!! Ameihamasisha timu na amewapa wachezaji kujiamini sana na kila mmoja anaona ana nafasi!! Tutunze hazina hii!
Nimesikia interview zake na Maestro, jamaa kichwa sana
 
Kwa nini usiwekwe hadharani? Mbona mishahara ya makocha wazungu huwekwa hadharani? Ikiwa ni siri lazima atapunjwa!! Mbaya zaidi anaweza kupewa mshahara mdogo kuliko baadhi ya wachezaji wa kigeni na hawatamheshimu!!
Mshahara wa kocha gani mzungu uliwekwa hadharani?
 
Mshahara wa kocha gani mzungu uliwekwa hadharani?
Acha ushamba!! Kwenye ulimwengu wa soka mishahara siyo siri hata kidogo, na Tanzania siyo kisiwa! Usiri hulenga uonevu!! Anayeruhusiwa kuamua mshahara wake uwe siri ni kocha mwenyewe na anafanya hivyo kwa maandishi!! Ona hapa:

Highest Paid Premier League Manager Said To Earn More Than Arsenal & Chelsea Bosses Combined​

A report by a British newspaper has published salary figures for all 20 current managers in England's Premier League.
According to the information, no Premier League manager earns as much as Manchester City's Pep Guardiola, who is said to be on £19m per year.
Liverpool boss Jurgen Klopp is apparently second in the pay table on £16m per year - just over £300,000 per week.
Tottenham's Antonio Conte (£15m per year) and Leicester's Brendan Rodgers (£10m) are the only other Premier League managers credited with eight-figure salaries.
These numbers were published by The Sun this week alongside the news that Arsenal manager Mikel Arteta is set to increase his pay to £8.3m per year, putting him fifth on the list.
Arteta will soon be earning more than Chelsea manager Thomas Tuchel (£7m), despite the German leading his side to Champions League and FIFA Club World Cup glory.
Dean Smith and Thomas Frank are reportedly the joint-lowest earners (£1.5m each) among the Premier League managers.
But they could be among the highest-earning bosses in the Championship next season as Norwich and Brentford are both prime candidates for relegation.
Antonio Conte and Pep Guardiola shake hands after Tottenham's 3-2 win at Man City in February 2022
 
Back
Top Bottom