Hismastersvoice
JF-Expert Member
- Jan 26, 2013
- 21,741
- 26,735
Wanabodi,
Kama kawaida yangu, kila nikipata fursa, huja na makala zangu za "Kwa Maslahi ya Taifa"
Hili ni maslahi ya taifa ya pongezi kwa TRL, nimeona mzigo wa mabehewa mapya ya kisasa ya reli ya kisasa ya SGR ukipokelewa bandarini, DSM, hivyo hatua ya kwanza ni kutoa pongezi kwa TRL
Tulichoelezwa ni hiki
Kwa sisi baadhi yenu, tulioishi nchi za wenzetu, tumepanda treni hizi za kisasa za kasi zinazoendeshwa kwa umeme, bulet trains, ambazo zinakwenda hadi kasi ya speed 160kmh kwa saa!, ila mabehewa ya abiria ya wenzetu tuliyo yapanda, sio kama haya tunayo letewa sisi!, hivyo kwanza natoa hongera sana TRL kwa mabehewa haya.
Kwavile SGR ni reli mpya ya kisasa, je vichwa, mabehewa haya tulioletewa ni mabehewa mapya ya kisasa? Kwa jicho tuu la kawaida, behewa hilo ni lile la kwenda mwendo kasi wa 160kmh?. Naona kama sio! Kama tumenunua mabehewa mitumba, tuelezwe tuu, Watanzania ni watumiaji wazuri wa vifaa used, na hakuna ubaya wowote kutumia vitu vilivyotumika yaani used au mitumba, Ila kitu muhimu ni kwa Watanzania tuelezwe tu ukweli kuwa mabehewa haya ni used, na sio viongozi wetu watueleze tumenunua mabehewa mapya ya kisasa, kumbe ni mabehewa mitumba yaliyo karabatiwa, kupakwa rangi na kufanyiwa nakshi nakshi tu?
Hapa ninachokisoma na kinachokanushwa ni vitu viwili tofauti, kwanza Watanzania tunapaswa kuambiwa ukweli
1. Taarifa ya TRC inasema vichwa vipya na mabehewa mapya, lakini ukweli ni kuwa ni vichwa mitumba na mabehewa mitumba ya mwaka '1947'!.
2. Mkataba ni wa ukarabati na kutiwa nakshi nakshi kwa vichwa na mabehewa mitumba!, na sio kuundwa kwa vichwa na mabehewa mapya!.
3. Hakuna ubaya nchi kununua vichwa mitumba na mabehewa mitumba, kitu muhimu ni Watanzania tuelezwe ukweli!.
4. Je, hivyo vichwa viliundwa lini, wapi na vimetumika muda gani kabla sisi hatujauziwa?
5. Mitumba hiyo imenunuliwa kwa bei gani na inakarabatiwa kwa bei gharama gani?
5. Tufanyiwe comparative analysis, kama tungenunua vichwa vipya na mabehewa mapya, tungetumia gharama kiasi gani, compared na kununua vichwa mitumba na mabehewa mitumba, ili tujue tumeokoa fedha kiasi gani kwa kununua mitumba hiyo?
6. Japo gharama za kununua vitu vipya ni juu ila maintance cost ni ndogo, unaweza kununua mitumba kwa bei poa kumbe ni mitumba choka mbaya, hivyo maintenance cost ikawa juu.
7. Sii wengi wanajua kazi ya CAG sio kutoa tuu zile ripoti za hesabu za serikali, CAG ni Mdhibiti na Mkaguzi, ufhibiti unafanywa kabla ya manunuzi, je, kulifanyika tathmini yoyote rail worthness report ya vichwa mabehewa hayo mitumba kabla hayajanunuliwa?. Then CAG atufanyie value for money audit, msikute mitumba hiyo tumepewa bure, huku watu wakipiga kubwa tunauziwa kwa bei ya mapya!.
8. Ukiingia mkataba wa manunuzi, mzigo ukanunuliwa, delivery ndio ikachelewa, huwezi kuvunja mkataba huo ukabaki salama, hivyo kesi ikifunguliwa, Tanzania tunashindwa hata kabla kesi haijaanza!.
9. Tulivinja mkataba wa Dowans, watu wakajiapisha "over my dead body", tulishitakiwa, tukashindwa, tukadaiwa tukasema hatulipi!, ukweli ni kuwa tumelipa kwa siri, Watanzania hatukuambiwa!.
10. Tulipo vunja mkataba wa Dowans, Zitto akashauri tuitaifishe mitambo ile, Wabunge wetu wakagoma kuwa Tanzania hatununui mitambo mitumba!
11. Mitambo ile ikanunuliwa na Simbion, tukaingia nao mkataba ule ule wa Dowans tuliovunja, kwa gharama zile zile na tukawalipa!
12. JPM alipoingia tukavunja mkataba wa Simbion, tukashitakiwa, tukashindwa, JPM akagoma kulipa!, ila baada tuu ya JPM kuitwa kule, huku nyuma, sio tuu tumelipa, bali pia tumeinunua ile mitambo kwa bei ya ajabu, sasa mitambo ile tuliosema ni mtumba hatununui, sasa ni mali yetu na malipo yote yaliisha fanyika chap chap, ila Watanzania hatuambiwi!
Tuambiwe tu ukweli!
Paskali.
Chombo chochote kinachokwenda mwendo kasi ninakushauri usinunue mitumba, tatizo la mabehewa yakitumika zaidi ya muda wake mabehewa huanza kutoka na kurudi kwenye reli hii ni hatari kwa abiria, wanapokarabati wanajaribu kuaraini ili yasitoke na kurudi kwenye reli na hilo ndilo muhimu kuliko viti, vyoo na madirisha, lakini kuna lamuhimu zaidi ni viungio kati ya behewa na behewa yaani zile seheme zenye maturubai kama ya akodiani ya muziki au kwenye mabasi ya mwendokasi.
Serikali inayonunua mitumba ni serikali ya wajanja kwani bei ni ya maelewano kati ya watu wawili vivyo hivyo na muda wa matumizi haumo kwenye mkataba yaani "you buy as it is".