Hongera Wizara ya Ujenzi! Sasa twende na reli za mijini kwa kutumia sekta binafsi

Hongera Wizara ya Ujenzi! Sasa twende na reli za mijini kwa kutumia sekta binafsi

Lord denning

JF-Expert Member
Joined
Jun 3, 2015
Posts
15,819
Reaction score
33,255
Moja ya sababu zilizofanya Tanzania kuwa nyuma kimaendeleo ni suala la sera zetu kuegemea ujamaa yaani kila kitu kufanywa na serikali jambo ambalo limekuwa likifanya tuchelewe sana kupata maendeleo.

Jitihada kadhaa zimekuwa zikifanywa kuondokana na haya ila bahati mbaya zimekuwa zikikosa consistency.

Nimefurahishwa sana na mpango huu wa Wizara ya ujenzi wa kujenga barabara ya highway kutoka Kibaha hadi Morogoro kwa kutumia sekta binafsi ambapo watu watakuwa wanalipia kuitumia. Haya ndo maendelo sasa tiliyokuwa tunayataka maana yatachochea ujenzi wa miundombinu bora na kuongeza mapato ya serikali kupitia kodi na ajira kwa wananchi.

Sasa msiishie hapo kuanzia sasa muende na kwenye reli za mijini kwenye majiji makubwa kama Dar, Dodoma, Mwanza, Arusha na Mbeya.

Tunaweza anzia Dar kwenye mzunguko mkubwa wa hela, karibisheni wawekezaji wa sekta binafsi wajenge miundombinu ya reli kwenye mifumo yetu ya barabara na kuweka treni za haraka za kufanya safari za mijini kama ilivyo kwenye majiji makubwa duniani huko.
 
Back
Top Bottom