Uchaguzi 2020 Hongereni timu za kampeni Uchaguzi wa mwaka 2020 kwa kutupilia mbali siasa za majitaka

masare

JF-Expert Member
Joined
Oct 12, 2010
Posts
1,791
Reaction score
1,830
Mpaka sasa sijasikia siasa za majitaka wala kuongelea maisha binafsi ya wagombea.

Nakumbuka uchaguzi wa mwaka 2010 mgombea mmoja aliambiwa eti kaiba mke wa mtu.

Uchaguzi wa 2015 mwingine aliambiwa eti ni mgonjwa.

Hongereni vyama vyote kwa kufanya kampeni za kisayansi.

Tunatumaini hii hali itaendelea kuwa shwari Hadi mwisho wa Kampeni.
 
Hujasikia tu....

Kuna baadhi ya "inzi wa kijani", wanamwita mgombea wa upande ule kuwa ni "mlemavu".....

It's too sad kusikia binadamu wa kawaida kuwa na akili za namna hii...!
 
Hujasikia kuwa eti mgombea anae ongoza kwenye mbio anajifanya alipigwa risasi
 
Hujasikia tu....

Kuna baadhi ya "inzi wa kijani", wanamwita mgombea wa upande ule kuwa ni "mlemavu".....

It's too sad kusikia binadamu wa kawaida kuwa na akili za namna hii...!
Hiyo hawaioni kama ni udhalilishaji watasema wamemsifia na tume na mamikwara yake yooote itakaa kimya kama ilivyokaa kimya kwenye "mashavu!!"
 
 
Tarime mjini mwenyekiti wa ccm wilaya alizindua kampeni kwa kumtukana mgombea ubunge Tarime mjini kwa tiketi ya Chadema, matusi ya nguoni na wala tume hawakusema chochote...!!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…