Kwanza nyie wote mlioko Dar na mnajua hamkuzaliwa Dar nawakumbusha kurudi vijijini kwenu mkasaidie wazee wenu wanateseka, vyakula ni ghali sana, pesa hakuna mtaani.
Zile show off zenu za Samaki samaki acheni mara moja, rudini huko kwenu mkaishi maisha halisi acheni kuigiza.
Wengine kwenu Kilosa rudini mkasaidie kulima mpunga, wa Kyela rudini mkazalishe mpunga huko, wasukuma rudini mkachunge ng'ombe nyama imekua ghali sana.
Niweke bayana jiji la Dar ni kwa ajili ya wazaramo, nyie mnang'ang'ania nini lakini?
Tena nyie wasukuma nyie hakikisheni mnaondoka na Bashite wenu akachunge ndama kwao.
Mwisho nawatakia maisha magumu wote mnaong'ang'ania kuishi Dar ilihali maisha yenu ni duni kuliko anayeishi Matombo vijijini.
Natania tu [emoji23] [emoji23]