DOKEZO Hospitali ya Mloganzila inatumia wanafunzi (interns) kuhudumia wagonjwa mahututi, na manesi wana huduma mbaya, mnatumaliza

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
Pole sana, lakini kumbuka kifo kipo tu. Hospitali gani wagonjwa hawafi?

Kuna vitu tunalaumiana lakini nasi tunachangia, unakuta mtu anaumwa hatua za awali haendi hospitali, akiishafikia hatua mbaya ndio sasa utaona dugu wanajichangisha kumtafutia mpendwa wao huduma, halafu wanataka apone haraka.

Kuna wagonjwa wanaletwa hospitali, unamuangalia halafu unawaangalia waliomleta unashindwa hata kuongea.

Wakati mwingine unakuta mlichelewa sana, au hali ya mgonjwa imesha pitiliza hatua ya kutibika.

Tunapotupiana lawama tujiangalie nasi pia.

Sitaki kukuongezea machungu ila nimechangia kama wengine, samahani ikiwa nitakuwa nimekosea pia.
 
Mloganzila mbona Mimi nilihudumiwa kama mfalme mkuu??
Hosptal yangu pendwa Ile na.mwanafunzi akikuhudumia lazima awe na daktari bingwa hapo pembeni .sijawai kuona mwanafunzi akiwa mwenyewe pale.pole kwa yaliyokukuta.
Kuna watu wapuuzi tu nchi hii! Nina classmate wangu pale ni daktari. Atakuwa sasa na miaka 20 kazini kama daktari. Huyu mwamba anahitimisha eti hakuna madaktari pale ni interns tu! Uongo huo!
 
Hakuna taasisi ya serikali yenye huduma nzuri,tena mahospitari ndio kabisa, upuuzi mtupu,
 
Ile ni hospitali ya kufundishia! Pale wagonjwa wanapelekwa kwa ajili ya Wanafunzi madaktari,manesi,nk
 
Siku zote wanasema ukipelekwa Mlogazila aga kabisa majirani zako.
 
Hili tatizo ni kubwa na lipo KCMC,BUGANDO NA MUHIMBILI
 
Pole mkuu. saivi hata muhimbili mwendo ni uouo full interns. usipokaa sawa umeleta shida ya mguu wenzio wanang'ang'ana kukagua kichwa. ukitaka madaktari nguli hadi uwafate kwenye vilinge vyao.
Udakitari sasa umerahisishwa, kila dakitari ana kompyuta mpakato kwa ajili ya kugugoo na kutoa tiba.
 
Mloganzila ni Deathrow😁 kule unapelekwa ukaishilie tu.

Wale wagongjwa ambao wana critical cases huwa wanasukumiwa kule wakafarijiwe na interns kwa siku mbili tatu kabla hawajakata moto.
 
Huduma za Mloganzila zipo vizuri sana kwa sasa. Labda unaongelea miaka mitano iliyopita
 
Mloganzila is good ukilinganisha na hosp nyingine za Dar. Nililazwa pale x 2.
Asubuhi natembelewa na jopo la madaktari wasio pungua watano. wakiongozwa na mbobezi, mabingwa kadhaa na intern.
Mloganzila wako vizuri.
Janabi anafanya kazi nzuri.
 
Kwa mloga kwa kuwa ni teaching hospital siwezi kushangaa sasa muhimbili usiku asilimia kubwa unakuta wanabaki intern nimewahi kushuhudia dogo anapiga sim kwa chief anamwambia hii issue ni ngumu anataka ushauri.
 
Mbona hyo muda sana tangu ianze. Mgonjwa wetu alihudumiwa na wanafunzi Hadi tunatoka hospitali. Magnesium nao wana roho mbaya kama wanahudumia Simba na nyoka na sio binaadam
 
Kuna mdogo wangu alilazwa pale aliandikiwa kwenda kufanyiwa kipimo cha MRI mpaka anafariki hakufanyiwa hicho kipimo kisa hakuna wa kumpeleka kwenye hiyo machine,labda useme wewe una mtu wa kukushika mkono
Alilipia hicho kipimo?na mbona wale manurse huwa wako vizuri Sana kushusha wagonjwa kwenye vipimo jamani??
 
Mleta mada anadepression kwa hiyo sioni kama kuna ukweli au uwongo ya hayo madai.
 
Kuna ndugu yangu mmoja anafanya kazi Mloganzila aliniambia nikajifungue kule nilikataa nikamuambia kuna huduma mbaya watu wanakufa akaniambia shida moja wagonjwa wengi ni wa rufaa unakuta mpaka analetwa Mloganzila kashakuwa hali mbaya hawaletwi hali nzuri wnaapoteza maisha lawama kwetu sababu wanaletww critical condition.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…