Hospitali ya Taifa Muhimbili yajibu hoja za Wana JamiiForums kuhusu vifo Hospitali ya Muhimbili-Mloganzila

Jamani, msinyooshee kidole Mloganzila tu,
Mahospitalini Hali si shwari.
Changamoto ni nyingi.

Haya utayakuta TMK, MNYMLA,AMANA na kwingineko.
Sema tu ni vile jicho la waandishi habari hua halifiki huko, na hata wakifika huko waandishi wenyewe hawawezi kuhoji maswali ya msingi Kwa kua waandishi walio wengi ni mbumbumbu wa health proffession .

Changamoto ni
Rasilimali watu,
Vifaa tiba.
Madawa ya kisiasa
Uongozi
Mishahara isio kidhi mahitaji
Siasa kwenye ngazi za maamuzi za ki proffessional
Umbumbumbu WA viongozi wa kisiasa kwenye health proffession
Ukiritimba wa madaktari bingwa dhidi ya madaktari wa chini Yao
Ubaguzi among health professionals

1. Tumpate kiongozi wa ngazi za juu wa kisiasa Daktari mwenye ushawishi na mwadirifu anaeweza mshari Raisi na serikali Kwa ujumla wake.

2..Bajeti iongezeke na sehem kubwa ielekezwe kwenye tiba. Na sio vikao na mikakati na kulipana allowances

3. Waandishi habari watiwe motisha kuandika habari za mahospitalini
4. Maslahi ya watumishi wa afya yaboreshwe, mathalani Dr. Wa chini kabisa awe na take home ya 3m.

5. Vifaa tiba na dawa za kisiasa zinunuliwe Kwa level ya Aghakhani na Hindumandal katika hospitali za mikoa

6. Tuongeze vibali vya ajira Kwa watumishi wa afya.

7. Tuweke mifumo ya kuondoa siasa kwenye uongozi wa hospitalini.

8.Tu buni mfumo wa ki taasisi utakao ziunganisha hospitali za mikoa na wilaya.

Nimatumaini yangu kua yakitendeka hayo, basi huduma ya afya nchini inaweza boresheka. Ni maoni binafsi
 
Kuna mtu kafa baada yakuvunjika mguu kutokana na ajali sasa huyu atapimaje mara kwa mara
Sent using Jamii Forums mobile app
 
On other side:

Mlongazila ilijengwa ili kuwa training hospital(yaani ingekuwa campus ya Muhas) na baada ya kukamilika mùhas walianza kuajiri taratibu taratibu staffs,Lengo likiwa ni kwenda hatua kwa hatua mpaka hospitali itakapokuwa na full man power.

Lakin ghafla no 1 akapindua meza kwanza kwa kusitisha kibali cha ajira,pili siku ametembelea pale ghafla akaamuru wagonjwa toka muhimbili wahamishiwe mlongazila na hii ilikuwa very shocking news kwa chuo cha Muhas kwa kuwa lengo ilikuwa ni chuo kijitegemee hadi kuwa na hospitali yake ya kufundishia.

Swala likaja man power inatoka wapi? nadhan ndio msala uko hapa. Na hao ma specialist anaosema prof sidhan kàma idadi hyo wanafika unless wanahudumu muhimbili na mlongazila kwa wakati tofauti. Sote twajua mpaka kupata daktari bingwa inachukua mda kidogo.

Yote kwa yote ilikuwa ni kosa kukurupuka kuhamishia wagonjwa mlongazila bila kuwa na nguvu kazi ya kutosha.Madharà yake ndio haya.

Mungu awahurumie wagonjwa wapone. Inauma kupoteza ndugu kwa uzembe. Lakini mambo ya siasa kwenye taaluma madhara yake ndio kama haya.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwanza siyo sahihi mgonjwa aliyekuwa refferred kwenda hospitali ya Taifa, anafika huko, anaenda kutibiwa na interns. Wakati wote interns wanatakiwa kuambatana na madaktari bingwa. Na lolote wanalolifanya wanatakiwa kufanya kwa maelekezo ya daktari bingwa, siyo kwa maamuzi yao.

Hawa ni wagonjwa wenye matatizo yaliyoshindikana kwenye hospitali za chini. Inakuwaje tena, wanafika hospitali ya Taifa wanahudumiwa na madaktari wanafunzi? Si aheri wangebakia hospitali za chini walikokuwa?
 
Acheni kutetea upumbavu au wee ndio unaongoza kuchezea smart phone badala yakufanyakazi hapo Mloganzila
umejigundua kama umeandika upuuzi kama vitu huvijui sio kuandika andika tu
mloganzila hakuna mwanafunzi anae enda na usi mdharau anae soma udaktari Tanzania tena muhimbili maana amekuzid vingi ukitoa kutopoka kwako

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Duh. Tatizo hapa linaonekana ni kubwa. Yaani wagonjwa 26 000 kwa robo mwaka, tena kwa ongezeko la karibu 50 % wanatibiwa na madaktari 102 tu.....!? Hapo kumuona Daktari lazima itakuwa ni shughuli.

Halafu Hii ratio ya 1 to 1 ya madaktari bingwa kwa madaktari wa kawaida na watarajiwa iko Sawa au ni standard ya Tanzania tu. Nilitegemea at least madaktari wa kawaida wawe zaidi ya mara mbili ya madaktari bingwa au inakuwaje...!?
 
siata,
Huyu anayejiita profesa naye sijui ana nini kwenye mishipa ya fahamu. Ukiitwa profesa onesha ufahamu wako! Nani asiyefahamu uzembe wa Muhimbili na Mloganzila? Wanafunzi wanafanyishwa mitihani mbele ya mgonjwa na ndugu mukiwepo munaona. Badala ya tiba, wewe unaletewa wanafunzi kujifunza bila hata kuomba samahani na kumuomba mgonjwa au ndugu.

Mbali na madakatari hovyo, madawa feki kibao hata Muhimbili ni hivyo hivyo! Nafanya compilation ya madawa niliyopewa Muhimbili yakashindwa na nilipokwenda mitaani, yakawaleta matokeo chanya.
 
Rebeca 83,
Nchi gani unayofahamu watu kwenda kupima bila ugonjwa? Yaani unakwenda hawa wanafunzi tunaowasema watafute ugonjwa mwilini? Are you serious?
 
Prof, Malalamiko yaliyotolewa dhidi ya hospitali hiyo ya Mloganzila.
Fanyieni Kazi kwa haraka Changamoto zote zinazojitokeza ili kurudisha Imani kwa Wananchi.
 
Neno kama desmosomes utaliitaje kwa kiswahii

Au phosphoribosyl pyro phosphate

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hii inaitwa failed Management.

Kama mdaktari wanapiga soga na wapo whatsapp.
Tatizo lipo kwenye Management.

Basi.
 
Profesa atenge muda wa kupitia malalamiko ya wananchi kupitia mitandao ya kijamii kisha aangalie uhalisia na kuyafanyia kazi Watanzania wa leo si wajinga na huwezi kuwadanganya kirahisi.
 
Najaribu kupima hy idadi ya vifo 1000+ kwa mwaka, ina maana kwa siku ni lazima wagonjwa wasio pungua wawili lazima wafariki. Ni changamoto kwa sekta ya afya kwa hospitali kubwa kama hii kuboresha uwezo wa kunusuru vifo vinavyotokana na maradhi mbalimbali.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ukiwa wafikiria kama great thinker watakiwa uanze kwa kufikiria aina ya wagonjwa wanaoenda Mloganzila. Watanzania wengi wakienda hospitali ujue wako terminally ill, na hospitali huwa kama sehemu ya wao kufia.
Jombaa kuna ishu ya dawa, fanya hivi ukiumwa kichwa kunywa paracetal ya hapa tanzania kisha lete mrejesho hapa jf
 
Sio kwa mwaka, ni kwa robo mwaka. Kwa ujumla hali sio nzuri
 
ki local local nataka nimuulize ze le Profeseri Museru..

pale mara ya mwisho mkewe kipenzi alipoumwa alimpeleka hapo!?

au yule bintiye

mmmhhh

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Julai-September wagonjwa 12,375 vifo 1000. Tafsiri rahisi zaidi kwa kila wagonjwa 120 kuna vifo 10

Tuombe afya njema

Sent using Jamii Forums mobile app
lkn ni moja ya hospitali inayopokea referral nyingin yani mgonjwa akishashindikana kwenye hospi tali ndogo anapelekwa pale, kwa maana hiyo lazima anakuwa kwenye hali mbaya.

tuliwawi kwenda na mgonjwa mmoja toka hospitali binafsi kwenda muhimbili wakasema kama hiyo hospitali wamemshindwa basi hali yake ni mbaya maana hiyo hospitali ni wabishi sana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…