Hotuba ya Lukuvi bungeni kuthibitisha kauli yake kanisani, UKAWA kumchukulia hatua za kisheria

Hotuba ya Lukuvi bungeni kuthibitisha kauli yake kanisani, UKAWA kumchukulia hatua za kisheria

Lukuvi na mrema wote wako sahihi.Watanzania tunaoshindwa kuwachulia hatua ndo tuko wrong. Mrema anapigania maisha yake lukuvi kadhalika. Kama wako wrong tuwachulieni hatua
 
Jana nilipokua nafuatilia bunge mwenyekiti wa bunge alimpa nafasi waziri wa nchi sera uratibu na bunge ndg Lukuvi nafasi ya alichokiita kujibu alichosema prof Limbumpa baada ya hicho alichokiita majibu kwa Lipumba, mh Lukuvi alimsifia sana Mrema kwa mchango wake uliomfurahisha bila shaka na kuwafurahisha wakubwa wa ccm mpaka akafikia kumuahidi kwamba atahakikisha Mrema anapata mafao yake ,maswali ya kujiuliza
1. je ni haki ya Mrema kupata hicho Lukuvi anachookiita mafao au ni rushwa baada ya kuwafurahisha kwa mchango wake bungeni
2.kama ni haki yake inahitaji kujipendekeza kwao ndio upate haki yako?
3. hii inatufundisha nini kwamba mpaka tujipendekeze kwa ccm ndio tunaweza kupata haki yetu?
4. kwanini Watanzania tunaruhusu mambo ya kijinga haya yatokee katika nchi yetu kwanini tunaruhusu waziri atumie ofisi ya umma na rasilimali za umma kwa manufaa ya chama chao na serikali iliyoko madarakani
5.ni wangapi wataanza kujipendekeza kwa ccm na serikali yake ili wapate wanachokitaka je tutajenga demokrasia kwa njia hizi?
inakera sana

Kwani UBUNGE aliupataje?Si kwa njia hiyohiyo?Aliyekwambia Mrema ni mpinzani nani?Unajua wanasema hakuna lenye mwanzo lisilo na mwisho!Wenzetu hawa wanajisahahu mno.
 
Nami natamani kupata CD 1 tafadhali durufuni nyingi muwape 'machinga' watuuziye huko mitaani kwetu.
Hivi hekima ndani ya chama chetu hiki kikukuuu imekwisha kabisa, hamna aliyesalia anayeweza kuwakemea waste a hovyo hovyo! Yale mashindano ya hoja siku hizo yamegeuzwa ni mashindano ya vioja, kazi tunayo.
Eti wengine wananufaika na muungano wa serikali mbili kwa sababu ya vitunguu; na wengine wanaambiwa Mapinduzi hayakuja kirahisi, hivyo kama Pemba inahitaji kuongoza sharti wajiandaye kupindua la hasha; hawataongoza visiwa kamwe!
Wananchi ndo mnajukumu la kuweka mambo sawa; kazi kwenu
 
Ndio wawakilishi wa JK,its true. birds of the same wings fly together.
Mie nilitegemea mheshimiwa Rais angemkemea Lukuvi na si Lissu. Nakumbuka waziri mmoja katika awamu ya mzee Mkapa aliishatoa kauli mbaya sana kwa waliokuwa wanamlilia Nyerere wamfuate huko aliko?
 
lukuvi ana akili za kuvukia barabara tu
Na za kumwamisha afisa wa Takukuru aliyemkamata na Rushwa wakati wa kura ya maoni hizo ndo akili zake.Nyingine alizo nazo kwenda kutishia watu kanisani huku yeye akiabudu vinyago na mizimu!!Lukuvi ni hasara ya taifa.
 
Kwani UBUNGE aliupataje?Si kwa njia hiyohiyo?Aliyekwambia Mrema ni mpinzani nani?Unajua wanasema hakuna lenye mwanzo lisilo na mwisho!Wenzetu hawa wanajisahahu mno.

Mnakumbuka Mremba alijikomba kwa CCM kabla ya uchaguzi mkuu uliopita, kisha wakamchangia pesa za kwenda kuchukulia form za ubunge.
 
Hivyo Lukuvi anavyosema wananchi wanavitaka na hawataki Serikali 3 je hizo serikali 2 wanazozipigia Upatu si ndio zilizopo je zimeleta hayo wananchi wanayoyataka? kweli kwa sasa kuna baadhi ya viongozi hawana tofauti na maiti hawajitambui na kujielewa kabisa.

''Lukuvi alisema wakati wote wananchi hawataki serikali tatu, bali wanataka maendeleo ikiwamo maji, barabara na vitu vingine lakini vyote viwe kwa kupitishwa kwa serikali mbili''.
 
Mie nilitegemea mheshimiwa Rais angemkemea Lukuvi na si Lissu. Nakumbuka waziri mmoja katika awamu ya mzee Mkapa aliishatoa kauli mbaya sana kwa waliokuwa wanamlilia Nyerere wamfuate huko aliko?

Kama baba kavua NGUO kasimama mbele ya wanawe alafu akajiziba uso kwa viganja vyake, je watoto wake watafanya nini?

Kauli ya Lukuvi kanukuu kwa JK wakati anahutubia bunge. Kauli hiyohiyo kairudia Amani Karume pale Mwembeyanga temeke siku chache baada ya JK kuihalalisha bungeni. Kinana ananukuu kauli hiyohiyo nchi mzima. Swali la kujiuliza, je UKAWA watamchukulia hatua mtoto aliekaa uchi na kumwacha babake ambae ndo kaanza kusaula?
 
Kama baba kavua NGUO kasimama mbele ya wanawe alafu akajiziba uso kwa viganja vyake, je watoto wake watafanya nini?

Kauli ya Lukuvi kanukuu kwa JK wakati anahutubia bunge. Kauli hiyohiyo kairudia Amani Karume pale Mwembeyanga temeke siku chache baada ya JK kuihalalisha bungeni. Kinana ananukuu kauli hiyohiyo nchi mzima. Swali la kujiuliza, je UKAWA watamchukulia hatua mtoto aliekaa uchi na kumwacha babake ambae ndo kaanza kusaula?
Mkuu, ni Ali Karume na si Amani Karume.
 
ccm wachochezi na wameshavuruga Amani ya nchi.
Kweli mkuu, kama rasimu hii bora ingeheshimiwa nchi nzima ingetulia na kupata katiba mpya ila kwa kuwa Rais hayupo radhi kuipata ndio maana tunaona juhudi nyingin mno zinafanywa kuikwamisha kwa kuingiza mambo ambayo hayamo kwenye rasimu kama matusi, kuvunja muungano, jeshi kupindua nchi na kadhalika.
 
Nami natamani kupata CD 1 tafadhali durufuni nyingi muwape 'machinga' watuuziye huko mitaani kwetu.
Hivi hekima ndani ya chama chetu hiki kikukuuu imekwisha kabisa, hamna aliyesalia anayeweza kuwakemea waste a hovyo hovyo! Yale mashindano ya hoja siku hizo yamegeuzwa ni mashindano ya vioja, kazi tunayo.
Eti wengine wananufaika na muungano wa serikali mbili kwa sababu ya vitunguu; na wengine wanaambiwa Mapinduzi hayakuja kirahisi, hivyo kama Pemba inahitaji kuongoza sharti wajiandaye kupindua la hasha; hawataongoza visiwa kamwe!
Wananchi ndo mnajukumu la kuweka mambo sawa; kazi kwenu
Mkuu, pana mmoja alisema Mapinduzi walifanyika Unguja na Pemba palipandishwa bendera tu. Hii Rais haioni ila kaona ukosoaji wa Lissu tu ndio mshiko.
 
Mwenye link ya Youtube ya hiyo hotuba ya Lukuvi Kanisani aitupie hapa.

Twataka tujuwe mbichi na mbivu.

Tumemsikia Lipumba alivyoeleza na tumesikia Lukuvi akijiuma uma bila kutaja aliyoyaongea. Tunataka hiyo video tujisikilizie wenyewe na tuamue nani mkweli, Lipumba au Lukuvi.
 
peleka mahakamani huyo mburula,unajuahawa ccm walishajihakikishia kuwa watatawala nchi hii milele,The hegue inawasubiri kwa hamu sana
 
Kama baba kavua NGUO kasimama mbele ya wanawe alafu akajiziba uso kwa viganja vyake, je watoto wake watafanya nini?

Kauli ya Lukuvi kanukuu kwa JK wakati anahutubia bunge. Kauli hiyohiyo kairudia Amani Karume pale Mwembeyanga temeke siku chache baada ya JK kuihalalisha bungeni. Kinana ananukuu kauli hiyohiyo nchi mzima. Swali la kujiuliza, je UKAWA watamchukulia hatua mtoto aliekaa uchi na kumwacha babake ambae ndo kaanza kusaula?

Kadiri ya sheria na katiba ya sasa Rais ana kinga kutofikishwa vyombo vya sheria, isipokuwa Lukuvi hawezi kukwepa kitanzi hicho kama wakiamua kumchukulia hatua.
 
Hivi kweli hili linawezekana yaani tz ambayo ni t/nyika na znz iwe na account moja na znz?

Hivi kufungua account ni ishu sana ?

Vigezo vya kufungua account sio kujua benki ilipo bali ni pesa ulizonazo.

Hivi znz wakiulizwa leo mnalofungu limebaki la kuja kuweka kwenye account wataleta?
 
Mwenye link ya Youtube ya hiyo hotuba ya Lukuvi Kanisani aitupie hapa.

Twataka tujuwe mbichi na mbivu.

Tumemsikia Lipumba alivyoeleza na tumesikia Lukuvi akijiuma uma bila kutaja aliyoyaongea. Tunataka hiyo video tujisikilizie wenyewe na tuamue nani mkweli, Lipumba au Lukuvi.

Naona ukweli kuhusu madudu ya CCM ambayo tunalalamikia kila siku umeanza kuyaona, kwamba dhami ya ubaguzi ndiyo inayokuja kuiua CCM, leo wanapotamka wazi kuwabagua waislamu na Mkuu wa nchi ametia lijamu kinywani ni ishara wazi za itikazi walizo nazo.
 
Muda mwingine si elimu peke yake inayosaidia,bali hata umri na busara pia uwa ni msaada tosha!tunapoelekea siko kwenyewe kabisa

ningependa kwenye cd hiO wamuonyeshe yule binti amefanana na kawawa hawa ndo wamelewa madaraka kwelikweli
 
Wa dau Naomba ieleweke kuwa mgonjwa anayepelekwa nje ya.Nchi Kwa matibabu huwa wamwahindwa Kupona hapa ndani na Yupo hoi akihitaji kwenda kutibiwa nje ya Nchi . Iweje Kwa Lukuvi tuliueaminishwa kuwa kakatizwa safari ya kwenda matibabu India ili Aje atoe Ufafanuzi Kwa aliyotamka Kanisani....cha ajabu mgonjwa Huyo mbali na kuvunja kanuni katika Kuzingatia muda huku mwenyekiti akinyamaza kimya ameonekana akina na Afya njema sana
Nisaideni kujua Wana siasa wetu huenda nje kutibiwa nini?..,,
 
Back
Top Bottom