Elius W Ndabila
JF-Expert Member
- Jul 17, 2019
- 324
- 649
TUMEMSKIA MH RAIS MAGUFULI LEO?
Na Elius Ndabila
0768239284
Leo Mh Rais akimuapisha Mkuu wa Mkoa na Wakuu wa Wilaya za Morogoro, Monduli na Arusha mjini ametoa hotuba ambayo inaweza kuwa msumali wa moto kwa baadhi ya viongozi. Hotuba ya Mh Rais ilikuwa na dhima nyingi, lakini ninataka nizungumze neno alilochomekea la *MRIDHIKE* na nafasi zenu.
Mh Rais amewataka wstumishi wa umma wote, hasa viongozi wake wateule kuridhika na nafasi wanazopewa. Amesema hakuna sababu ya kiongozi kutoridhika na nafasi yake aliyonayo wakati anafanya vizuri na ana miaka mingi. Amesema atawashangaa sana. Ametumia mfano IGP, CDF na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro kama wanatamani kugombea ili akawateue Uwaziri. Mh Rais amesema ni haki yao kidemokrasia, lakini wanapoenda wawe na uhakika wa kushinda. Amesisitiza kuwa hata ukiwa wa kwanza si lazima iteuliwe kugombea kwani ninaweza kumteua hata mtu wa nne, anazungumza huku akitolea mfano Naibu waziri wa Mambo ya nje aliyeshika nafasi ya nne lakini akateuliwa kugombea.
Kwa tafsiri rahisi hotuba ya Mh Rais ilijikita kufikisha ujumbe kwa watumishi wengi ambao sasa ofisi zao hazifanyi vizuri na wako busy kusaka ubunge. Mh Rais inaonyesha wazi anajua kuwa wateule wake wengi wanaona sasa majukumu waliyopewa ni nonsense na kuona Ubunge ni bora. Kitendo cha Mh Rais kuzungumza hadharani inaonyesha wazi amekasirishwa na hatua hizo za wateule wake kuacha kazi na kumkimbiza na harakati za majimboni. Mh Rais amesisitiza kuwateua kugombea kwenye uchaguzi kunatokana na alivyoamka siku hiyo kwani anaweza kuwakata hata kama wanaongoza kura.
Dhana ya kutoridhika inaonyesha ndiyo iliyowaondoa aliyekuwa mkuu wa mkoa Wa Arusha na DC wake kwa kuwa wamekuwa wakigombana kwa miaka miwili mfululizo bila kufanya kazi zao vizuri. Ukimsikiliza kwa umakini Mh Rais akitoa wosia kwa wateule wapya amesema hakuridhika na migogoro kwa viongozi hao. Hata hivyo wadadisi wa mambo ya kisiasa wanasema Mh Rais kumtumia IGP, CDF na RC Iringa ilikuwa ni kufikisha ujumbe kwa Mh Gambo ambaye amekuwa akitajwa kugombea ubunge Ilala au Arusha kitu kilichopelekea kutotimiza vizuri majukumu yake na kutumia mda mwingi kugombana na wasaidizi wake na kuchochea migogoro ya kujipatia umaarufu.
Rai kwa watumishi wote wenye nia ya kwenda majimboni, jitafakarini kwanza, ongeeni na Mungu wenu kwanza kama mko tayari kurudi Misiri kama safari ya Kanani itashindikana. Mh Rais amekuwa mwema mno kusema hadharani hasa kutahadharisha. Wewe kama unaona bado Mungu hajasema nawe endelea kutimiza majukumu ambayo Mungu amemtumia mteule wake Mh Rais kukuamini, lakini kama wakati wa Bwana unasema sasa hapo ulipo umeshatumika vya kutosha na sasa ni wakati wa kwenda kuwawakilisha wananchi kwenye chombo cha kutunga sheria na kuishauri serikali nenda jimboni.
Na Elius Ndabila
0768239284
Leo Mh Rais akimuapisha Mkuu wa Mkoa na Wakuu wa Wilaya za Morogoro, Monduli na Arusha mjini ametoa hotuba ambayo inaweza kuwa msumali wa moto kwa baadhi ya viongozi. Hotuba ya Mh Rais ilikuwa na dhima nyingi, lakini ninataka nizungumze neno alilochomekea la *MRIDHIKE* na nafasi zenu.
Mh Rais amewataka wstumishi wa umma wote, hasa viongozi wake wateule kuridhika na nafasi wanazopewa. Amesema hakuna sababu ya kiongozi kutoridhika na nafasi yake aliyonayo wakati anafanya vizuri na ana miaka mingi. Amesema atawashangaa sana. Ametumia mfano IGP, CDF na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro kama wanatamani kugombea ili akawateue Uwaziri. Mh Rais amesema ni haki yao kidemokrasia, lakini wanapoenda wawe na uhakika wa kushinda. Amesisitiza kuwa hata ukiwa wa kwanza si lazima iteuliwe kugombea kwani ninaweza kumteua hata mtu wa nne, anazungumza huku akitolea mfano Naibu waziri wa Mambo ya nje aliyeshika nafasi ya nne lakini akateuliwa kugombea.
Kwa tafsiri rahisi hotuba ya Mh Rais ilijikita kufikisha ujumbe kwa watumishi wengi ambao sasa ofisi zao hazifanyi vizuri na wako busy kusaka ubunge. Mh Rais inaonyesha wazi anajua kuwa wateule wake wengi wanaona sasa majukumu waliyopewa ni nonsense na kuona Ubunge ni bora. Kitendo cha Mh Rais kuzungumza hadharani inaonyesha wazi amekasirishwa na hatua hizo za wateule wake kuacha kazi na kumkimbiza na harakati za majimboni. Mh Rais amesisitiza kuwateua kugombea kwenye uchaguzi kunatokana na alivyoamka siku hiyo kwani anaweza kuwakata hata kama wanaongoza kura.
Dhana ya kutoridhika inaonyesha ndiyo iliyowaondoa aliyekuwa mkuu wa mkoa Wa Arusha na DC wake kwa kuwa wamekuwa wakigombana kwa miaka miwili mfululizo bila kufanya kazi zao vizuri. Ukimsikiliza kwa umakini Mh Rais akitoa wosia kwa wateule wapya amesema hakuridhika na migogoro kwa viongozi hao. Hata hivyo wadadisi wa mambo ya kisiasa wanasema Mh Rais kumtumia IGP, CDF na RC Iringa ilikuwa ni kufikisha ujumbe kwa Mh Gambo ambaye amekuwa akitajwa kugombea ubunge Ilala au Arusha kitu kilichopelekea kutotimiza vizuri majukumu yake na kutumia mda mwingi kugombana na wasaidizi wake na kuchochea migogoro ya kujipatia umaarufu.
Rai kwa watumishi wote wenye nia ya kwenda majimboni, jitafakarini kwanza, ongeeni na Mungu wenu kwanza kama mko tayari kurudi Misiri kama safari ya Kanani itashindikana. Mh Rais amekuwa mwema mno kusema hadharani hasa kutahadharisha. Wewe kama unaona bado Mungu hajasema nawe endelea kutimiza majukumu ambayo Mungu amemtumia mteule wake Mh Rais kukuamini, lakini kama wakati wa Bwana unasema sasa hapo ulipo umeshatumika vya kutosha na sasa ni wakati wa kwenda kuwawakilisha wananchi kwenye chombo cha kutunga sheria na kuishauri serikali nenda jimboni.