Hotuba ya Warioba Bungeni Dodoma: Jumanne, Tarehe 18 Machi 2014 na Hoja ya Muungano wa Serikali Tatu

Hotuba ya Warioba Bungeni Dodoma: Jumanne, Tarehe 18 Machi 2014 na Hoja ya Muungano wa Serikali Tatu

Mzee huyu alisifiwa sana na ccm kabla hajaweka wazi msimamo wa wadau wengi kuwa wanataka serikali 3,leo kawa adui mpk katengwa na jamii yanaccm ila watanzania bado tunamthamini na kumpa heshima za kipekee.

Mda mwingine unatamani rais wa nchi hii awe kama warioba,mtu anaethamini mawazo ta watanzani zaidi kuliko mawazo ya chama,watu wazima wenzangu tuigeni hekima hizi

Naunga mkono hoja mkuu
 
Mh warioba amesema wamepokea mapendekezo ya muundo wa serikali 3 yametolewa hata na taasisi na idara za serikali ambazo katika maoni yao waliyo wasilisha kwa tume kimaandishi yamependekeza 3gvnt,miongoni mwa taasisi na idara hizo ni ofice ya waziri mkuu,ofice ya makamu wa rais,baraza la wawakilishi znz na bunge la jamhuri ya muungano wote wametaka uwepo wa serikali ya tanganyika,zanzibar na ya muungano,hivyo wale ccm wanaopinga mfumo wa serikali 3 wanapata wapi kiburi hicho?
 
haya ni matokeo ya makosa yaliyofanywa (kwa makusudi) na 'aliyeanzisha' mchakato huu wa katiba mpya. Suala la uwepo wa muungano na aina ya muungano yalipaswa kufanyiwa referendum kwanza kabla ya kuandika katiba.

Kwa namna mchakato huu ulivyokwenda, kuna uwezekano mkubwa tukawa tumepoteza mabilioni yaliyotumika pasipo kupata katiba mpya. Rasimu imetengenezwa on the basis of a three tier government, endapo wajumbe wa bmlk wakiamua tu kuwa wanataka serikali mbili na si tatu, kimsingi watakuwa wamevuruga mchakato mzima na kwa uhalisia kazi nzima ingepaswa irudi ifanywe tena na tume ya katiba. Si rahisi kwa bmlk kuja na rasimu yenye msingi wa serikali mbili katika muda mfupi uliopo (labda kama watachukua katiba iliyopo (ya 1977) na kuibadilisha).

Ndio sababu jaji warioba alitahadharisha kazi ya bmlk iwe ni kuboresha rasimu na sio kubadilisha hoja ya (za) msingi.

i believe umeongea point ya maana hapa hili bunge bado sijaliamini iy is another rubber stamp ya ccm kupitisha kitu wqnachotaka
 
Revocatus Kashaga, naona unaongelea issue ambayo iko nje ya uwezo wako wa kufikiri. Opinion polls ni Sayansi na huendeshwa kitaalam kwa kufuata misingi ambayo kama utapenda kuielewa, labda thread ifunguliwe. Shida yako kubwa nadhani ni kutoelewa principle inayoongoza utafiti wa maoni ya walio wengi katika jamii. Hakuna namna unaweza kuwauliza Watanzania milioni 45 mawazo yao kama unavyotamani ingefanyika, badala yake unatumia kitu kinaitwa sampling. Ndio maana kwa nchi kama Marekani yenye watu zaidi ya milioni 350, maoni ya watu 35,000 (0.1%)kwa mfano, inatosha kabisa kuonesha wazi muelekeo wa wengi. Bahati mbaya sina muda, labda siku nyingine nitakuelewesha zaidi...naomba nikuache na hili hapa;
Labda nisaidie kidogo kuhusu utafiti wa maoni na takwimu zake. Ni hivi. Ni kweli kujua maoni ya Watanzania huhitaji kuwauliza wote M 45. Najua kwa uhakika kuwa sampuli ya kisayansi kwa Tanzania haijavuka watu 3000 wa kuhojiwa. Lakini msisitizo hapa uko ktk sayansi. Kanuni mojawapo ya utafiti wa maoni kisayansi ni kuwa wanaohojiwa hawafuatwi kwa kuwapenda, au kudhani wanajua. Na hawatakiwi kujileta kwa wakusanya maoni. Anayehojiwa ni ambaye tarakimu ya random numbers imemwangukia ili kila mtu awe na uwezekano sawa wa kuhojiwa. Wakijileta watakuwa wamejihamasisha kwa msimamo mmoja unaofanana, kwa hiyo mawazo hayatakuwa wakilishi tena. Kosa hili limefanywa na Tume zote za maoni ya Katiba. Ile Kamati ya Kisanga ndiyo ilitia fora kwenye kosa hili, ila waliojihamasisha nakujileta walikuwa wapenda serikali mbili, ambao asilimia yao ilivuka 90 , hadi ikawa kichekesho kwa Kamati hiyo kupendekeza serlkali tatu dhidi ya aslimia hiyo. Tume ya Warioba imefanya kosa hilo hilo kisayansi, ila waliohamasika ni wa serikali tatu. Tume hii iliambiwa hili, ikapuuza. Ndiyo sababu takwimu zake hazina uhalali mkubwa. Ukosoaji wa asilimia hizo kwa kutumia takwimu za Tume yenyewe, kama walivyofanya wasomi fulani, ni sahihi, lakini kosa kubwa ni msingi wa ukusanyaji maoni. Hii haina maana kuwa takwimu za Tume hazifai kabisa, maana hata wanaotaka yeyote anayejisikia atoe maoni kwa jambo fulani kwa simu au barua pepe hupata matumizi fulani ya takwimu zake. Lakini uzito wa ushahidi wa takwimu hizo hupungua sana. Ndiyo sababu Tume ya Warioba haiwezi kuhalalisha serikali 3 kwa takwimu zake za maoni tu, au kuzuia mabadiliko ya rasimu yake kwa ku invoke ukuu wa maoni ya wananchi
 
Hotuba ya Warioba itaishi Milele,haina unafiki hata Kidogo,imeeleza ukweli usiopendwa
 
Zikishatengenezwa hizo DVD zisambazwe kwa wananchi. Pia isambazwe kwa njia nyingine yoyote iwe ni kutengeneza mp3 n.k! Hususani ufafanuzi juu ya Muundo wa Muungano! Hii itawezesha kupata ukweli usioegemea upande wowote.

Kazi hii ifanywe na WanaHarakati au wengineo wenye mapenzi mema na nchi yetu! Ripoti yake inaelezwa reality na haiko biased


tena hizo dvd zitufikie na ss huku kalenga
 
Wasiwasi wangu zaidi,ukapatikana hapa,ktk hotuba hiyohiyo,ukurasa wa 12,,,"Zanzibar,wananchi karibu wote waliotoa maoni walijikita kwny suala la Muungano",,"Kati ya wananchi karibu 38,000 waliotoa maoni,Wananchi 19,000 walitoa maoni kuhusu muundo wa Muungano"



SASA ZANZIBAR,KWA MUJIBU WA SENSA YA 2012 INA WATU WAPATAO 1,303,569..WATU 38000 WALIOTOA MAONI,NI SAWA NA ASILIMIA 2.9 YA WAZANZIBARI WOTE,NA HAO 19000 WALIOZINGUMZIA MUUNDO,NI ASILIMIA 1.45 YA WAZANZIBARI WOTE....Je,HIYO INAYOSEMWA KWAMBA PALIKUWA NA MJADALA MKALI,,ULIKUWA UKALI WA ASILIMIA 2.9 YA WAZANZIBARI WOTE AU HII 1.45 YA WAZANZIBARI WOTE???. . .KWANGU MIMI,HAPA NDIPO NINAPOTILIA SHAKA UPACHIKWAJI WA NAMBA HIZI,KWA MALENGO YA KUIPATA SERIKALI YA TATU..NA NDIPO HAPAHAPA,NAJIKUTA,NAUNGANA NA CCM,JAPO WENYEWE WANAWEZA WASIWE WAMESIMAMIA KTK HOJA SANJARI NA HIZI ZAKWANGU,,,NA NI KATIKA HILI,NDIPO BINAFSI,NINAAMINI KUNA JAMBO NYUMA YA SHILINGI,AMBALO EITHER TUME,AMA WARIOBA PERSONALLY,ANALO,DHIDI YA MUUNGANO HUU

Mkuu unaweza ukawa sahihi, ila mimi nipo hapo kwenye numbers....Unafikiri ni nini kingefanywa ili kupata uwakilishi sawia/sahihi wa wananchi? Je kila mmoja wetu alitakiwa atoe maoni yake? If yes, katika muundo gani/upi rahisi? Manake hata ukirudi kwenye uchaguzi mkuu, tunakuta kuwa ni watu milioni 5 tu ndio waliopiga kura kumchagua rais! Sasa kwenye population ya watu 40m+, kweli raisi achaguliwaye ndiye kipenzi chetu wote?

Siko katika kupingana na hoja yako, ila najaribu kuangalia uwakilishi wetu wote kwenye mchakato tu. Je, tumeikimbiza sana ili hali tulihitaji muda zaidi ili angalau asilimia 90% ya wananchi itoe maoni yake?
 
..Kanuni mojawapo ya utafiti wa maoni kisayansi ni kuwa wanaohojiwa hawafuatwi kwa kuwapenda, au kudhani wanajua. Na hawatakiwi kujileta kwa wakusanya maoni. Anayehojiwa ni ambaye tarakimu ya random numbers imemwangukia ili kila mtu awe na uwezekano sawa wa kuhojiwa...
Unazijua njia zote ambazo tume ilitumia kukusanya maoni?

Hata wale waliopo nje ya nchi walikuwa na nafasi ya kufanya hivyo:

Kwa mujibu wa Ratiba iliyotolewa na Tume, Wajumbe wa Tume wamegawanywa katika makundi saba na kila kundi litakusanya maoni ya wananchi katika mkoa mmoja kwa siku ishirini na nane. Kwa mujibu wa Ratiba hiyo, kila kundi litatembelea kila wilaya iliyopo katika mkoa husika ambapo kitafanya mikutano miwili kila siku.

Kwa kuzingatia utaratibu ambao Tume imeuweka, Wajumbe wa Tume wakifika katika vituo vya mikutano hutoa maelezo ya utangulizi kuhusu madhumuni na kazi za Tume. Baada ya maelezo hayo, kila mwananchi hupewa fursa ya kutoa maoni yake kwa mdomo kwa muda usiopungua dakika tano. Wale wanaotoa maoni kwa njia ya maandishi, hupewa muda wa kutosha kufanya hivyo. Kwa mujibu wa Ratiba hiyo, kila kundi linapaswa kufanya mikutano miwili kwa siku ambayo hudumu kwa saa tatu kila mmoja.

Tume inatambua kuwa wananchi wana shauku kubwa ya kutoa maoni yao kuhusu Katiba Mpya na ingependa kumfikia kila mmoja mahali alipo. Hata hivyo, kwa kuzingatia jiografia ya nchi na muda ambao Tume imepewa, Tume imepanga ratiba ambayo itawezesha wananchi kutoa maoni kwa kuzingatia jiografia ya eneo husika. Hivyo basi, Tume inatoa wito kwa wananchi kujitokeza kwa wingi katika maeneo ambayo itafanya mikutano na kutoa maoni yao.

Tume inachukua fursa hii kuwafahamisha wananchi kuwa Ratiba ya mikutano ya kukusanya maoni haikupangwa kwa kuzingatia Kata bali imepangwa kwa kuzingatia eneo ambalo linaweza kujumuisha wananchi kutoka zaidi ya Kata moja.

Tume pia inapenda kuwafahamisha wananchi kuwa wanaweza kuwasilisha maoni kupitia tovuti ya Tume (www.katiba.go.tz); barua pepe ( maoni@katiba.go.tz) au kwa njia ya posta kupitia anuani zifuatazo:
a) Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Makao Makuu, Mtaa wa Ohio, S.L.P 1681, DAR ES SALAAM Au
b) Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jengo la Ofisi ya Mfuko wa Barabara, Mtaa wa Kikwajuni/Gofu, S.L.P. 2775, ZANZIBAR

Utaona kuwa kila mwananchi alikuwa huru kupeleka maoni kwenye tume kwa kutumia njia mojawapo kati ya zilizokuwepo. Nakumbuka hili lilipigiwa kelele sana, watu tu wazito sana kushiriki mambo ya msingi ya taifa letu lakini sisi ndio wa mwanzo kulalalama. Sitashangaa kama wewe ni mmoja kati ya wananchi wengi ambao waliona sio wajibu wao kupeleka maoni yao kwa tume na hukupeleka maoni yako! Tume ilikuwa haina mamalaka ya kuwalazimisha watu kutoa maoni.
 
Mkuu unaweza ukawa sahihi, ila mimi nipo hapo kwenye numbers....Unafikiri ni nini kingefanywa ili kupata uwakilishi sawia/sahihi wa wananchi? Je kila mmoja wetu alitakiwa atoe maoni yake? If yes, katika muundo gani/upi rahisi? Manake hata ukirudi kwenye uchaguzi mkuu, tunakuta kuwa ni watu milioni 5 tu ndio waliopiga kura kumchagua rais! Sasa kwenye population ya watu 40m+, kweli raisi achaguliwaye ndiye kipenzi chetu wote?

Siko katika kupingana na hoja yako, ila najaribu kuangalia uwakilishi wetu wote kwenye mchakato tu. Je, tumeikimbiza sana ili hali tulihitaji muda zaidi ili angalau asilimia 90% ya wananchi itoe maoni yake?


Labda nisaidie kidogo kuhusu utafiti wa maoni na takwimu zake. Ni hivi. Ni kweli kujua maoni ya Watanzania huhitaji kuwauliza wote M 45. Najua kwa uhakika kuwa sampuli ya kisayansi kwa Tanzania haijavuka watu 3000 wa kuhojiwa. Lakini msisitizo hapa uko ktk sayansi. Kanuni mojawapo ya utafiti wa maoni kisayansi ni kuwa wanaohojiwa hawafuatwi kwa kuwapenda, au kudhani wanajua. Na hawatakiwi kujileta kwa wakusanya maoni. Anayehojiwa ni ambaye tarakimu ya random numbers imemwangukia ili kila mtu awe na uwezekano sawa wa kuhojiwa. Wakijileta watakuwa wamejihamasisha kwa msimamo mmoja unaofanana, kwa hiyo mawazo hayatakuwa wakilishi tena. Kosa hili limefanywa na Tume zote za maoni ya Katiba. Ile Kamati ya Kisanga ndiyo ilitia fora kwenye kosa hili, ila waliojihamasisha nakujileta walikuwa wapenda serikali mbili, ambao asilimia yao ilivuka 90 , hadi ikawa kichekesho kwa Kamati hiyo kupendekeza serlkali tatu dhidi ya aslimia hiyo. Tume ya Warioba imefanya kosa hilo hilo kisayansi, ila waliohamasika ni wa serikali tatu. Tume hii iliambiwa hili, ikapuuza. Ndiyo sababu takwimu zake hazina uhalali mkubwa. Ukosoaji wa asilimia hizo kwa kutumia takwimu za Tume yenyewe, kama walivyofanya wasomi fulani, ni sahihi, lakini kosa kubwa ni msingi wa ukusanyaji maoni. Hii haina maana kuwa takwimu za Tume hazifai kabisa, maana hata wanaotaka yeyote anayejisikia atoe maoni kwa jambo fulani kwa simu au barua pepe hupata matumizi fulani ya takwimu zake. Lakini uzito wa ushahidi wa takwimu hizo hupungua sana. Ndiyo sababu Tume ya Warioba haiwezi kuhalalisha serikali 3 kwa takwimu zake za maoni tu, au kuzuia mabadiliko ya rasimu yake kwa ku invoke ukuu wa maoni ya wananchi
 
Hotuba ya Warioba imegusa nyoyo za watanzania na kuumiza nyoyo za watu wenye fikra mgando.
 
Kama kuna mtu mwenye softcopy au audio atuwekee tudownload maana wengine hatukuifaidi.
 
Mkuu unaweza ukawa sahihi, ila mimi nipo hapo kwenye numbers....Unafikiri ni nini kingefanywa ili kupata uwakilishi sawia/sahihi wa wananchi? Je kila mmoja wetu alitakiwa atoe maoni yake? If yes, katika muundo gani/upi rahisi? Manake hata ukirudi kwenye uchaguzi mkuu, tunakuta kuwa ni watu milioni 5 tu ndio waliopiga kura kumchagua rais! Sasa kwenye population ya watu 40m+, kweli raisi achaguliwaye ndiye kipenzi chetu wote?

Siko katika kupingana na hoja yako, ila najaribu kuangalia uwakilishi wetu wote kwenye mchakato tu. Je, tumeikimbiza sana ili hali tulihitaji muda zaidi ili angalau asilimia 90% ya wananchi itoe maoni yake?

Dina, nimelipenda jibu lako, pokea like yangu.
 
Nadhani kuwa jeshi letu la Navy litapanuliwa zaidi kwa sababu ya jukumu la ziada la kulinda mpaka baina ya Zanzibar na Tanganyika! Idara ya Uhamiaji itatakiwa kufanya kazi zake kwa makini sana kuhakikisha kuwa wapemba wote wanaondoka kwenye ardhi ya Tanganyika mara moja kwa vile terms zilizopwapa haki ya kuishia na kumiliki mali Tanganyika zitakuwa zimekwisha.
 
Back
Top Bottom