Hotuba ya Warioba: Wabunge 9 wa Zanzibar watishia kujitoa CCM baada ya kikao cha usiku

Hotuba ya Warioba: Wabunge 9 wa Zanzibar watishia kujitoa CCM baada ya kikao cha usiku

Chadema Diaspora

JF-Expert Member
Joined
Oct 25, 2010
Posts
480
Reaction score
644

Hotuba ya Warioba: Wabunge 9 wa Zanzibar watishia kujitoa CCM baada ya kikao cha usiku


Habari kutoka chanzo chetu cha kuaminika ni kuwa kulikuwa na kikao cha CCM siku ya Jumanne usiku baada ya hotuba ya jaji Warioba Bungeni. Kikao hiKi kiliisha saa nane za usiku bila kuwa na muafaka.

Agenda kubwa ya kikao ilikuwa kujaribu kuwalazimisha wabunge wa Zanzibar wakapitishe mswaada kwenye Bunge la Zanzibar kutengua kipengele ambacho kilipitishwa 2010 kuwa Zanzibar ni nchi. Agenda hii ilizua mabishano makali kati ya wabunge wa Zanzibar na viongozi wa Tanzania Bara. Viongozi wa Bara (CCM) walionekana kulaamu maamuzi yaliyo fanyika 2010 ya kuitambua Zanzibar kama nchi kikatiba na walikuwa wanalazimisha wabunge wa Zanzibar wakatoe kipengele hicho.

Ajenda hii ilipata pingamizi kali kutoka kwa wabunge wa Zanzibar ambapo wabunge tisa (9) wa Zanzibar waliahidi na wametishia kujitoa CCM endapo hili swala litaendelea kulazimishwa na kupitishwa.

Tutaendelea kuwahabarisha kuhusu hili kila tunapo pata updates kutoka kwenye intelegencia yetu ambayo tumefanikiwa kuipandikiza ndani ya kamati kuu ya CCM.

WE REPORT, YOU DECIDE
 
Mimi bado najiuliza, WHO THE HELL ARE THEY kung'ang'ana kubadili maoni ya asilimia kubwa ya wananchi? WENYE NCHI wamesema serikali 3, WAO NI NANI HATA WAPITISHE VINGINEVYO? KWA MASLAHI YA NANI?!!!....Aibu iwe kwao. Nampongeza sana Mzee Warioba, ameonesha ukomavu wa hali ya juu na ujasiri kuzidi wote wanaopelekwa kama wanasesere!
 
Zanziba wameshauvunja muungano. Pinda amebaki na karatasi tu zilizoandikwa JMT. Hakuna atakaye ibadili katiba ya Zanziba ila viongozi wa hiyo wanayoiita Tanzania bara wabuni mbinu nyingine ya kuitambua hiyo nchi iitwayo Tanzania bara ili iwe ndo ilmeungana na Zanziba.
Huu ni muungano mpya ulio buniwa na ccm wala sio ule wa waanzilishi wa JMT. Ndo maana wakawaita Wazanzibari, nchi kamili ije kuandika katiba na nchi wanayotaka kuungana nayo sasa hivi. Bila katiba ya Tanganyika kwanza, hii ynayojadiliwa hapo ni feki kabisa.
 
ccm wote ni mazombi,hawajielewi wameshindwa kabisa kusoma alama za nyakati!
 
Watanzania wana miliki viwanda vya kutengeneza uongo-Jk.

Story from Ufipa Uongo Industry.
 

Hotuba ya Warioba: Wabunge 9 wa Zanzibar watishia kujitoa CCM baada ya kikao cha usiku


Habari kutoka chanzo chetu cha kuaminika ni kuwa kulikuwa na kikao cha CCM siku ya Jumanne usiku baada ya hotuba ya jaji Warioba Bungeni. Kikao hiKi kiliisha saa nane za usiku bila kuwa na muafaka.

Agenda kubwa ya kikao ilikuwa kujaribu kuwalazimisha wabunge wa Zanzibar wakapitishe mswaada kwenye Bunge la Zanzibar kutengua kipengele ambacho kilipitishwa 2010 kuwa Zanzibar ni nchi. Agenda hii ilizua mabishano makali kati ya wabunge wa Zanzibar na viongozi wa Tanzania Bara. Viongozi wa Bara (CCM) walionekana kulaamu maamuzi yaliyo fanyika 2010 ya kuitambua Zanzibar kama nchi kikatiba na walikuwa wanalazimisha wabunge wa Zanzibar wakatoe kipengele hicho.

Ajenda hii ilipata pingamizi kali kutoka kwa wabunge wa Zanzibar ambapo wabunge tisa (9) wa Zanzibar waliahidi na wametishia kujitoa CCM endapo hili swala litaendelea kulazimishwa na kupitishwa.

Tutaendelea kuwahabarisha kuhusu hili kila tunapo pata updates kutoka kwenye intelegencia yetu ambayo tumefanikiwa kuipandikiza ndani ya kamati kuu ya CCM.

WE REPORT, YOU DECIDE

Haya sasa wale walio kuwa wanamwandama Warioba wako wapi? Wajitokeze tuwaone .Ukweli mchungu huo Zanzibar wanatuchekezea sana .
 
Hongereni sana wawakilishi wetu mulio majemedari ktkt kuipigania Jamhuri ya Watu wa Zanzibar ile alotuachia Sheikh Karume, tunaelewa vizuri udhaifu wa viongozi na wawakilishi wa CCM Zanzibar ndio maana masindikizo kama hayo huelekezwa kwao bila kujali kwamba Zanzibar sio yao bali ni ya Wazanzibar wote hassa katika suala nyeti kama hilo linahitaji maamuzi ya Wazanzibar wote, lakini pia katika jambo la utambulisho wa nchi ya Zanzibar hapo hapana mjadala hadi Mzee Warioba ameliona kwamba Wazanzibar ktk suala kama hilo daima huwa pamoja bila kujali itikadi za vyama vyao, ila hebu tujiulize ikiwa CCM hushindikiza wawakilishi wafanye maamuzi ya kubadili katiba na kuondosha kipengele kilicho itambulisha hadhi ya Zanzibar kama ni nchi ndani ya Jamhuri ya Muungano, Jee wajumbe wa CCM wataweza....?
tukiangalia kwa kura za wajumbe kwa mujibu wa idadi ya wajumbe wa BLW, wajumbe wa CCM bado hawana 2/3 majority kwa kufanya maamuzi hayo, hivyo matakwa hayo daima hayatapitushwa ndani ya BLW kwa vile tutategemea upinzani mkali kutoka kwa wajumbe wa CUF ambao hao daima hawana kificho wala hawatafuni maneno katika kupigania Jamhuri ya Watu wa Zanzibar....!!
mwisho tukumbukeni pia katiba ya Zanzibar ya 2010 inatamka wazi kwamba lazima wananchi washirikishwe kupitia kura ya maoni katik kuamua hatima ya Zanzibar yao ikiwemo hilo la kuifanya Zanzibar kuwa ni mkoa kama wanavyofikiria viongozi wa Tanganyika,na hiyo ndio nguvu pekee Wazanzibar walionayo ndio maana tunasema azimio hilo buttu, lazima lije kwetu wananchi sio wawakilishi...!!
Zanzibar kwanza!!
Aluta Continua!!
 
Ebu yupige kura sisi members wa jf, niwangapi wanaunga mkono muungano waserikali tatu nawangapi serikali mbili
 
hii mibunge ya ccm kutoka tanganyika inatia aibu sana ! Badala ya kupigania nchi yao inahangaika na visiwa vidogooo!
 
hapa ni hesabu ndogo tuu .Zanzibar inatambulika kama nchi na wanakila kitu chao katiba yao bunge lao raisi wao bendera yao n.k
sasa huku upande wa pili nikinyume tena kizungumkuti kweli kweli na hata hatueleweki Tanganyika no katiba no bendera no raisi no bunge Bali kuna kudandia tu vitu vya muungano jamhuri ya muungano.
Tanganyika imefia wapi jamani??? hapa wakulaumiwa ni aliye lianzisha kama ni kuuvunja muungano basi Zanzibar ndio kinala tena wakiungwa mkono na viongozi waliopitisha sheria ya kuitambua Zanzibar kikatiba kua ni nchi why Leo hiii wanashikana mashati na kulalama ya kuwa msimamo wao ni serikali 2 na sio 3?
soon na watanganyika nasi tutadai haki yakutambulika kisheria na kikatiba ya kuwa ni nchi na inabidi hapo twende sawa kama Zanzibar .

hapo sasa ndio muundo wa serikali 3 utakapo pita bila kubwabwaja na kupingwa na mtu yeyote.

nakama watakomaa nakutoitambua Tanganyika basi kusiwepo na takataka yoyote inayoitwa jamhuri ya muungano?? na wao ndio watakuwa wameua muungano rasmi. kama no Tanganyika why ?? muungano ? utatoka wapi Zanzibar itakuwa imeungana na nani?? mpaka jamhuri ya muungano itambulike??

au ni hili jina la Tanganyika ndio linawachefua?? basi tutumie Tanzania bara kama nyie mnavyopenda ??

kwahili ccm hata mcheze vipi hamuwezi kukwepa aidha muungano ufe rasmi au mkubali kufufuka kwa Tanganyika na uwepo WA 3 serikali.
 
Hivi walikuwa wapi hadi madudu haya yakatokea?

Uvunjaji wa muungano wanauona Leo?

Leo Warioba wanamhukumu na kumlaumu kwa lipi?

SIMPLY, FOOLISHNESS
Tundu Lisu aliwahi kuonya kuwa kuna hatari kubwa kwa mustakbari wa muungano baada ya mabadiliko ya katiba ya Zanzibar. Alichoambulia ni kejeli, dharau na kupuuzwa. Hakuchoka, aliendelea kutoa dukuduku lake hata nje ya bunge, wachache sana wenye akili tulimuelewa. Leo macho yamewatoka walewale.......... mithiri ya mtu aliye fumwa anajisaidia haja kubwa njiani.
 
Back
Top Bottom