Houichi: Bondia Hassan Mwakinyo kagoma kupigana na Bondia Brandon Tysse kutoka Afrika Kusini

Houichi: Bondia Hassan Mwakinyo kagoma kupigana na Bondia Brandon Tysse kutoka Afrika Kusini

Linguistic

JF-Expert Member
Joined
Mar 16, 2021
Posts
3,669
Reaction score
8,268
RAIS wa Africa Boxing Union (ABU), Houcine Houichi amesema moja katika sababu iliyofanya wamvue mkanda Bondia Hassan Mwakinyo ni kugoma kupigana na Bondia Brandon Tysse kutoka Afrika Kusini.
.
Houichi anadai Mwakinyo alipewa ofa ya Dola za Kimarekani 20,000 [Tsh Mil 46] Lakini alikataa ofa hyo na kusema hapigani chini ya Dola 40,000 [Tsh Mil 92.8].

Rais huyo anasema ofa hiyo aliyoitaka Mwakinyo ilikuwa haina uhalisia kutoka na thamani yake ya sasa

Neno moja kwake Hassan Mwakinyo
 
Tjamani ya bondia ni nani anaipanga?labda tuanzie hapo
Inapangwa kuringana na mapambano unayocheza. Ukubwa wa mtu unaepambana nae ni wangapi duniani. Unacheza mapambano mangapi yenye ukubwa gani? Tatizo kwa Mwakinyo thamani yake haipandishi mapambano mengi amechezea Tz na aliopambana nao sio wa rank ya juu kiihivyo kwa uzito wake.

Hilo pambano, japo lilikuwa la hela ndogo,angecheza lingemsogeza mbele kwenye thamani.

Lakini kwangu naona bado yuko sahihi kuona kiwango kinachofaa.

Nimesikia yuko marekani, naona yuko kuchukua uzoefu zaidi na mazoezi yenye tija. Nina uhakika ana malengo ya mbali tutegemee makubwa kutoka kwake.
 
Inapangwa kuringana na mapambano unayocheza. Ukubwa wa mtu unaepambana nae ni wangapi duniani. Unacheza mapambano mangapi yenye ukubwa gani?...
Halafu ndo aje kucheza na yule wa Moro alipwe mil 10 sijui 5 kumbe chalii anapiga pesa ndefu ndo maana jeuri sana nilidhani kapata Dana mil 15 kumbe anavuta parefu
 
Inapangwa kuringana na mapambano unayocheza. Ukubwa wa mtu unaepambana nae ni wangapi duniani. Unacheza mapambano mangapi yenye ukubwa gani?...
Mpaka atake fedha yote hyo Pambano lake la mwisho alicheza lini na Bondia Gani?
 
Halafu ndo aje kucheza na yule wa Moro alipwe mil 10 sijui 5 kumbe chalii anapiga pesa ndefu ndo maana jeuri sana nilidhani kapata Dana mil 15 kumbe anavuta parefu
Mwakinyo alijikuta sana, ndo imemcost
 
Inapangwa kuringana na mapambano unayocheza. Ukubwa wa mtu unaepambana nae ni wangapi duniani. Unacheza mapambano mangapi yenye ukubwa gani?. Tatizo kwa Mwakinyo thamani yake haipandishi mapambano mengi amechezea Tz na aliopambana nao sio wa rank ya juu kiihivyo kwa uzito wake.

Hilo pambano,japo lilikuwa la hela ndogo,angecheza lingemsogeza mbele kwenye thamani.

Lakini kwangu naona bado yuko sahihi kuona kiwango kinachofaa.

Nimesikia yuko marekani, naona yuko kuchukua uzoefu zaidi na mazoezi yenye tija. Nina uhakika ana malengo ya mbali tutegemee makubwa kutoka kwake.
Mkuu umeeleza vizuri lakini bado hujasema ni 'Nani' hasa ndio anapanga hio thamani? Je kuna mamlaka husika au ni yeye bondia au ni mapatano tu.

Yaani kwa mfano Mwakinyo aliposema hio hela ni ndogo alitumia vigezo gani kujua ukubwa wake,na hao waliotoa hio offer walijuaje ana thamani hio kiasi kwamba lazima akubali, Hapa bondi anawezaje kukwepa uonevu?

Je hakuna mamlaka inayosema kwamba kwa mapambano uliyopogana na upingwa uliochukua mpaka sasa dau lako linaanzia $ kadhaa hadi kadhaa,kwamba anaweza kupatana ndani ya kiwango tajwa?
 
Hakuna cha neno moja kwa Mwakinyo..

Jamaa ngumi ni kazi yake yanayotokea ulingoni ye ndio anajua, akisema hailipi hailipi, mnaweza mumpe hamuwezi muacheni.

Kwangu naona yuko sahihi mtoto wa kitanga.

Sasa ameshavuliwa Mikanda yote karibuni ataanza kupigana Mbagala underground si anataka alipwe kama Mayweather.
 
Sasa ameshavuliwa Mikanda yote karibuni ataanza kupigana Mbagala underground si anataka alipwe kama Mayweather.
Aliyekwambia kuvuliwa mkanda utarudi kupigana manzese bani kaka, unajua lakin anabaki kwenye nafasi ile ile katika viwango vya ubora?
 
Mkuu umeeleza vizuri lakini bado hujasema ni 'Nani' hasa ndio anapanga hio thamani? Je kuna mamlaka husika au ni yeye bondia au ni mapatano tu.

Yaani kwa mfano Mwakinyo aliposema hio hela ni ndogo alitumia vigezo gani kujua ukubwa wake,na hao waliotoa hio offer walijuaje ana thamani hio kiasi kwamba lazima akubali, Hapa bondi anawezaje kukwepa uonevu?

Je hakuna mamlaka inayosema kwamba kwa mapambano uliyopogana na upingwa uliochukua mpaka sasa dau lako linaanzia $ kadhaa hadi kadhaa,kwamba anaweza kupatana ndani ya kiwango tajwa?
Mkuu jiulize hawa wasanii malipo ya shows zao kuna mtu huwa anapanga thamani yao?

Ada za uhamisho/usajili wa wachezaji wa mpira wa miguu je?

Nadhani ni suala la demand ya mwanamichezo husika kwa wakati huo na jinsi mapromota watakavyoona itawalipa kumpa kiasi anachotaka.
 
RAIS wa Africa Boxing Union (ABU), Houcine Houichi amesema moja katika sababu iliyofanya wamvue mkanda Bondia Hassan Mwakinyo ni kugoma kupigana na Bondia Brandon Tysse kutoka Afrika Kusini.
.
Houichi anadai Mwakinyo alipewa ofa ya Dola za Kimarekani 20,000 [Tsh Mil 46] Lakini alikataa ofa hyo na kusema hapigani chini ya Dola 40,000 [Tsh Mil 92.8].

Rais huyo anasema ofa hiyo aliyoitaka Mwakinyo ilikuwa haina uhalisia kutoka na thamani yake ya sasa

Neno moja kwake Hassan Mwakinyo
Tumuache afanye atakalo, kwanza kwenye status alionayo alijipandisha mwenyewe, wengi walimjua baada ya kushinda huko nje ambako alienda bila promo au offer zao.
 
Back
Top Bottom