Hili ndo tatizo la watanzania,Kuna MTU mmoja nae alipataga kituko kama chako,sema yeye ni kutoka kwa boss wake,ilikuwa hivi ,huyu jamaa alikuwa anafanya kazi sehemu kama janitor ,sasa kwenye ile nyumba akapatikana mpangaji Wa kizungu ni mdada,yule mzungu akatokea kuiva sana na yule janitor (kijana Wa Usafi) sasa yule kijana maskini akahisi yule mzungu amekolea kwake,akaja akaniomba ushauri kuwa boss wake inavyoonyesha amempenda ila anashindwa tu kumwambia, nikamwambia asubiri kwani wazungu kumpenda MTU kwao si ajabu na kama itakuwa kimapenzi atamwambia tu,jamaa akaniambia Mimi sielewi ndo maana namwambia hivyo akasema hadi soda wanapokezana then Mimi nasema asubiri!akaachana na Mimi akaenda kuomba ushauri kwa fundi mmoja hivi na yule Fundi nae sijui vipi lakini,akamwambia Huyo kakupenda wala haina shaka na wala haiitaji kuuliza,jamaa kutoka pale akaenda dukani akanunua jinzi la kike na card ya mapenzi akampelekea mzungu,mzungu akaipokea huku akishangaa sana , alipomaliza kuisoma akaanza kulia na kukimbia ndani,akampigia mwenye nyumba simu ili aje amuondoe yule kijana pale,alihofia anaweza bakwa,maana jamaa hana akili,utamtongaje anayekulipa mshahara huo ni uchizi
Sent using
Jamii Forums mobile app