Houth ilivyobadili mbinu kupambana na US,UK na France na huku Hamas wakiua komando mkubwa wa Israel

Houth ilivyobadili mbinu kupambana na US,UK na France na huku Hamas wakiua komando mkubwa wa Israel

Webabu

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2010
Posts
8,870
Reaction score
14,258
Kuanzia majuzi wanamgambo wa Houth wameanza kuzipa onyo meli zinazokatiza maeneo yao kabla ya kuzirushia makomboa.

Wakitumia meli yao ya wanamaji wiki iliyopita walimuonya kapteni wa meli ya True Confidence kwamba alikuwa akikatisha njia ambayo si salama kwake.

Kwa mara nyengine akaelekezwa apindishe meli yake kutoka uwelekea aliofuata.Na ilipokuwa dhahiri kapteni huyo wa meli kubwa sana ya mizigo akikaidi onyo la Houth ndipo iliporushiwa kombora na kusababisha vifo vya mabaharia 3 ikiicha meli hiyo kwenye hali mbaya.

Mbinu nyengine za Houth zinazotumika na kuanza kuleta mashaka iwapo wako peke yao au wameanza kupata ushiriikiano kutoka mataifa hasimu na Marekani mbali na Iran, ni kushambulia kwa kutumia kiwingu cha droni kama vile inavyofanyika kule Ukraine.

Hapo jana Houth walirusha droni 37 kwa mpigo kulenga meli za kivita za Marekani na washirika wake pamoja na meli moja ya kibiashara iliyokuwa ikipita eneo hilo.

Kati ya droni hizo 28 zilifanikiwa kudondoshwa kutoka mifumo ya ulinzi ya meli za washirika. Zilizobaki haikutajwa kuwa zilifanikiwa kufikia shabaha zao au zilidondoka zenyewe baharini.

Mambo yakiwa kama hivyo katika bahari nyekundu, kule Gaza jeshi la Israel limekiri kumpoteza komandoo wake wa cheo cha juu kwenye mapiganona Hamas kusini mwa jimbo hilo.

Israel confirms killing of high-ranking commando in Gaza

1710051367870.png
 
Houthis Wana copy mbinu za Ukraine ambazo alifungishwa na marekani. Ukrainians walifanya hivo kushambulia meli za kivita za Urusi, wakaharibu underwater pipes za North Stream 2. So Houthi nao wakakataa mikonga ya mawasiliano (underwater sea optic cables) kutoka ulaya kwenda Asia ,now mawasiliano between western countries na Asia hayako sawa on internet na simu. Na hizi cable ndio zilikua zinawapa kiburi kujiunga na màtumizi ya 5G now 6G ambayo ni technology ya Mchina. So Kuna China and Russia wako pia nyuma ya wa Houthis . Huku Russia ikilipiza kisasi na China ikielekea Kupata new western clients wanaojiunga na technology ya 5&6G
 
Nilisoma article Moja ya a western analysts alisema in the history ili uweze kuzuwia watu kupitisha meli eneo fulani ya bahati lazima uwe na fedha nyingi ,jeshi kubwa na meli za kivita kuliko wote. But Houthi with simple means and less cost wameweza kuweka naval blockade to western nations at a cheap cost . But cheap cost doesn't mean simple technology. It is costing the supremacists so dearly
 
Kuanzia majuzi wanamgambo wa Houth wameanza kuzipa onyo meli zinazokatiza maeneo yao kabla ya kuzirushia makomboa.
Wakitumia meli yao ya wanamaji wiki iliyopita walimuonya kapteni wa meli ya True Confidence kwamba alikuwa akikatisha njia ambayo si salama kwake.Kwa mara nyengine akaelekezwa apindishe meli yake kutoka uwelekea aliofuata.Na ilipokuwa dhahiri kapteni huyo wa meli kubwa sana ya mizigo akikaidi onyo la Houth ndipo iliporushiwa kombora na kusababisha vifo vya mabaharia 3 ikiicha meli hiyo kwenye hali mbaya.
Mbinu nyengine za Houth zinazotumika na kuanza kuleta mashaka iwapo wako peke yao au wameanza kupata ushiriikiano kutoka mataifa hasimu na Marekani mbali na Iran, ni kushambulia kwa kutumia kiwingu cha droni kama vile inavyofanyika kule Ukraine.
Hapo jana Houth walirusha droni 37 kwa mpigo kulenga meli za kivita za Marekani na washirika wake pamoja na meli moja ya kibiashara iliyokuwa ikipita eneo hilo.Kati ya droni hizo 28 zilifanikiwa kudondoshwa kutoka mifumo ya ulinzi ya meli za washirika.Zilizobaki haikutajwa kuwa zilifanikiwa kufikia shabaha zao au zilidondoka zenyewe baharini.
Mambo yakiwa kama hivyo katika bahari nyekundu,kule Gaza jeshi la Israel limekiri kumpoteza komandoo wake wa cheo cha juu kwenye mapiganona Hamas kusini mwa jimbo hilo.

Israel confirms killing of high-ranking commando in Gaza

Una Tabia za kike sana wewe. Jana ulikuja unalia kwamba watu gaza wanakufa kwa njaa
 
Una Tabia za kike sana wewe. Jana ulikuja unalia kwamba watu gaza wanakufa kwa njaa
Hueleweki kinachokuuma ni kipi
Jana stori za vifa vya Gaza kwani uongo na kuhusu Houth kwani ni uongo na kwanini unavihusisha na mimi.
 
Back
Top Bottom