Hoyce Temu kaanza mwaka vibaya

Hoyce Temu kaanza mwaka vibaya

Kuna mambo yanafukuta huko katika wizara ya mambo ya nje. Mambo mengi yamefuatana miezi ya hivi karibuni.

Kibaya zaidi inawezekana rasilimali za nchi zimetumia kumtetea na kumlinda kwa tuhuma zake binafsi. Hili linafanywa sawa na watawala na siyo sawa.

Kuhusu huyu bidada, nasema tu karma ipo. Nitaishia hapo.
 
Nchi hii ilianza kuharibika pale wanamuziki, Mamiss na waigizaji wa Bongo movies walipoanza kupewa nafasi nyeti serikalini! Hebu tuwe serious kidogo Kwan hao Mamiss na wanamuziki hawawezi kubaki huko kwenye kutoa burudani mpaka waje na huku serikalini na chamani kutuongoza?
Hao waliopewa nafasi kabla ya mamiss etc wamefanya nini cha maana. Zaidi ya wizi!!!
 
Kuna wengi hapa ukiwauliza Hoyce Temu amefanya makosa gani, hawajui. Lakini wanamshushia rungu!
Wengine hapa lawama zao zinasomeka kana kwamba aliiba pesa.

Mfano kosa LA kuvujisha siri za shirika. Ni nani hajawai kufanya ili kosa? Hata huyo aliyempa dada wa Taifa siri za Hoyce amefanya kosa hilo hilo!

Nitoe tu angalizo Kwa wale ambao tupo kwenye vibarua vya kuajiriwa.

Tusijisahau sana, tukumbuke taratibu na miiko ya kazi, nimesoma hayo maamuzi ya kesi ya dada yetu nikaona jinsi ambavyo mambo madogo yanaweza kukuweka matatani.

Kama ulivyosema, wengi wanalaumu na kumrushia maneno dada wa watu bila kujua shida Iko wapi, wengine wameenda mbali kuhusisha umiss, uchaga na hili sakata.

Kwa ufupi, Hadi kufikia hapo, ni yeye alikata rufaa dhidi ya maamuzi ya kesi yake iliyomfanya akapiteza ajira pamoja na kutokupatiwa likizo ya uzazi. Huo mchuano umeenda Hadi kufika Kwa katibu mkuu wa UN. Lakini hayo ni mambo yalitokea huko awali sema kumbe alikua anaendelea kupambana chini Kwa chini, nafikiri alishauriwa vibaya na utakuwa alilenga apate fidia Kwa maamuzi ya kuonewa.

Nikirudi kwenye ushauri Kwa sie tuliopo kwenye vibarua kuzingatia miiko ya kazi, unaona kabisa inakatazwa kufanya kazi nyingine nje ya ajira Yako bila kutoa taarifa Kwa mwajiri wako, hata kama haulipwi, lazima utoe taarifa waone kama hakuna muingiliano wa kimaslahi.

Utaona aliendelea na vipindinvyake vya watu wenye shida channel ten na haikua na tatizo Kwa vile alitolea maelezo na kupata kibali Cha mwajiri.

Tumeona kesi ya EFM, mwajiri anasisitiza hayo ni maoni ya mfanyakazi binafsi na sio kampuni au taasisi ya EFM.

Mambo ya kutumia email ya ofisi Kwa vitu binafsi napo haijakaa vizuri, Iko siku linaweza kutokea jambo ukaingia matatani. Uchunguzi wa Hawa jamaa hua sio wa kubahatisha, wanafukua Kila kitu.

Wanaweza kuondoka Hadi na hard disk kwenda kufanya investigation zao, ukiweza, mambo binafsi fanyia kwenye vitendea kazi vyako ambavyo havihusiani na vile vya ofisi.
 
Mimi simu yangu aioneshi picha ila najibu kulingana na komenti za watu mimi hapo nashauri uyo mtoto aliye fanyiwa icho kitendo akimbizwe hospitali na huyo mtuhumiwa akamatwe afungwe kifungo cha maisha mana ataendelea kuharibu watoto wengine kama watamuacha huru
Mkuu huku sio Facebook
 
Nitoe tu angalizo Kwa wale ambao tupo kwenye vibarua vya kuajiriwa.

Tusijisahau sana, tukumbuke taratibu na miiko ya kazi, nimesoma hayo maamuzi ya kesi ya dada yetu nikaona jinsi ambavyo mambo madogo yanaweza kukuweka matatani...
Hivi hii issue ni kweli? Mimi naona kama ni propaganda tu za mitandaoni kwa sababu dada wa watu ni mzuri mno kwa sura. Nilifikiri labda ni mambo tu ya kwenye mitandao kuwasakama watu maaraufu
 
Hivi hii issue ni kweli? Mimi naona kama ni propaganda tu za mitandaoni kwa sababu dada wa watu ni mzuri mno kwa sura. Nilifikiri labda ni mambo tu ya kwenye mitandao kuwasakama watu maaraufu
Soma maamuzi ya hiyo kesi amepost jamaa PDF ndio utaelewa mkasa mzima Kiongozi.

Binafsi naona amejitakia mwenyewe Kwa kutibua mambo ya zamani.
 
Naomba likn address ya mahali ilipo attachment

un.org
https://www.un.org › unatPDF
Judgment No. 2021-UNAT-1174


1672731083396.png

Temu was charged with misconduct and was subjected to a disciplinary process

Judgment

52. Ms. Temu’s appeal is dismissed and the UNDT Judgment is affirmed.

Dated this 29th day of October 2021.
(Signed)
Judge Knierim, Presiding
Hamburg, Germany

(Signed)
Judge Halfeld,
Juiz de Fora, Brazil

(Signed)
Judge Raikos
Athens, Greece
Entered in the Register on this 4th day of January 2022 in New York, United States.

(Signed)
Weicheng Lin, Registrar
 
Back
Top Bottom