Huawei wamezindua simu ya kwanza kujikunja mara mbili. Base model ni Tsh Mil 7.8

Mad Max

JF-Expert Member
Joined
Oct 21, 2010
Posts
26,961
Reaction score
77,890
Tumeona jana tarehe 09 Apple wamefanya yao kwa kutuletea iPhone 16 series. Same wine, new bottle!

Sasa bwana leo wakali wa hizi mambo Huawei wamefanya yao kwa kuzindua Huawei Mate XT Ultimate ambayo ni simu ya kwanza Duniani kukunjwa mara mbili.

Yaani iko hivi, ukiikunjua full unakutana na tablet yenye screen ya inch 10.2 diagonally.


Ukikunja upande wa kushoti screen inapungua inakua inch 7.9 ambayo bado ni kubwa ya kutosha tu.

Ukikunja tena upande wa kulia inakua simu yenye screen ya 6.4 screen.

Ya bei ndogo kabisa ni 256@ GB stirage inauzwa $2,800 (Tsh Mil 7.8) na ukitaka ya 1TB memory ipo, $3,400 (Tsh Mil 9.5) tu.

Tujitahidi kunywa maji na kula matunda wakuu.
 
Mpaka nifikie kutumia fordable smartphones tech yake itakuwa matured mno. Kwa sasa bado hazijanivutia hata resale value yake ni ndogo sana maana vioo vyake haviwezi kamwe kuwa na mwonekano mzuri wa kioo cha kawaida.
 
Sawa
Nadhani Msukuma atakuwa namba 1 kuinunua
 
Mbongo umeniahinda tabia, simu imetoka jana ushaanza kusema kioo hakina ubora?
Unaishi kijiji gani uko ukute hapo uko juu ya mpapai unatafuta mtandao.

Nani kakwambia foldable smartphones zimeanza jana?
Zipo Samsung Z Flip 5 na Z Flip 6, Z Fold 5 na Z Fold 6. Oppo wana foldable zao Find N series N, N2 na N3. Huawei wenyewe wana foldable nyingine kabla ya hii. Ni kwamba unaishi vichakani na wasaga mashineni huwezi ona hizo simu au nini?
 
Hahahaa ,karibu Idindilimunyo mkuu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…