Ghazwat
JF-Expert Member
- Oct 4, 2015
- 23,718
- 66,267
Kocha huyo imeripotiwa kwamba tayari ameshakubaliana kimsingi kujiunga na Simba Sports Club baada ya kufanya mazungumzo na uongozi wa klabu hiyo.
Velud alikuwa kwenye bechi la ufundi la klabu ya FC Paris ya Ufaransa na anahusika kuibua na kukuza vipaji vya vyote wanaotamba ulaya, akiwemo mchezaji wa zamani wa Liverpool ambaye sasa yupo Crystal Palace zote za England, Mamadou Sanko na Lassana Diara aliyewahi kutamba Chelsea, Arsenal, Portsmouth na Real Madrid.
Mchezaji mwingine aliyepikwa na Velud wakati akikinoa FC Paris ni Gabriel Obertan aliyewahi kuchezea timu za Bordeaux, Lorient, Manchester United Newcastle United Wigan Athletic na nyinginezo.
Velud ndiye alikuwa kocha mkuu wa timu ya Togo kuanzia 2009 - 2010 cha akina Emmanuel Adebayor, Kilichoshambuliwa kwa risasi kilipokuwa kikisafiri kwa barabara kwenda Angola kwenye fainali za kombe la Afrika (Afcon).
Hubert Velud amewahi kuzinoa klabu mbalimbali kwa mafanikio barani Afrika zikiwemo Toulon, FC Paris, Chalons-sur-Marne, Beauvais zote za Ufaransa TP Mazembe Englebert ya Congo DRC, Etoile du Sahel ya Tunisia, Es Settif na USM Alger za Algeria, pamoja na timu ya Taifa ya Togo
Baadhi ya mataji aliyotwaa;
Kocha huyo alifanikiwa kutwaa mataji kadhaa akiwa na timu mbalimbali, likiwemo la Ligi ya Algeria maarufu kama Ligue 1 mwaka 2013 akiwa na Es Settif, Super Cup ya Algeria 2013 akiwa na USM Alger na kubeba tena ubingwa wa Ligue 1 akiwa na kikosi cha USM Alger.
Kwa rekodi hizi, inaonyesha wazi kocha huyo ni mzoefu mwenye uwezo wa kuifikisha mbali Simba SC, zaidi ikiwa ni kuwapa mataji ya ndani na nje ukizingatia ni mwenyeji wa soka la Afrika.