Huenda Ndugai alikuwa anajua tulichokuwa hatukijui, sasa tunakiona cha mtema kuni

Huenda Ndugai alikuwa anajua tulichokuwa hatukijui, sasa tunakiona cha mtema kuni

Nchi inayoheshimika na itakayoheshimika Ni Ile inayojitegemea kwa Mambo take mengi, nchi yetu lazima tuanze kuisimamisha na kuijenga wenyewe kwa mikono yetu wenyewe, Sasa hutaki tuchangie katika kuijenga Tanzania yetu he unataka Nani she atujengee nchi yetu,

Kwani hufurahi unapoona vituo vya Afya,shule,zahanati ,huduma za maji na umeme vikisambazwa huku na huko kutokanaa na michango yetu kidogo kidogo kulingana na vipato vyetu
Sasa mbona serikali haipunguzi matumizi yao kuendana na hali halisi? Wakati sisi tunaminyana kwenye tozo wao wanadai magari mapya ya kifahari na wengine ndio washajinunulia magari yenye kuweza kujenga hivyo vituo vya afya.
 
Huyo babu alikua sahihi.

Ila ndio hivyo tena pressure ya mamlaka ni kubwa kuliko haki kwa wananchi.

Ubaya zaidi ni pale mwenye mamlaka anapokua tofauti na yule mwenye nafasi hiyo ya kufanya maamuzi kuwanusuru wananchi.
 
Mkuu mbona kama ndugai alikuwa anataka tozo ziwepo au sijaelewa hapo?

Amesema tozo ziwepo ili tuijenge nchi yetu wenyewe sasa huyu alikuwa na huruma na sisi wananchi au ni vipi?

Me naona wale wale tu.
Mkuu izi vitu zina operate katika namna ambayo ni complicated kidogo... ukitaka kupata picha jiulize maswali kama haya, ni kwa nini serikali ndiyo inayotengeneza na kumiliki pesa ya nchi yake lakini wanataka izo pesa ziende kwa wananchi then wazichukue tena hata kwa dhuruma, utagundua kwamba maisha na uchumi wa taifa lolote linasimama kwa shuguli za uzalishaji(kilimo, ufugaji, viwanda na zingine nyingi) ambazo sisi walala hoi ni lazima tufanye.. ili tabaka tawala waishi kifalme.
Sasa izi issue za mikopo aliyoipigia kelele jamaa inafanya kazi katika mtindo kama huo, kinachorudishwa hapo ni asilimia fulani ya shughuli za uzalishaji na rasilimali za nchi ambazo kwa kiasi kikubwa tunakuwa kama tunawafanyia kazi hao mabwana wanaotukopesha,

Rejea maneno ya magu, mala nyingi alikuwa akisema hawa wakopeshaji wangekuwa na nia njema wangeacha kutukopesha au kusamehe madeni kabisa ili tunachokikusanya ndani ya nchi kifanye maendeleo... kwa sababu what happens, wanakupa mkopo then katika makusanyo yako ya mwezi ama mwaka(uzalishaji wako)... kuna asilimia ni moja kwa moja inalipa ayo madeni, japo kujinasua kwene hii mifumo ni ngumu... fatilia kuna documentary za watu wanaitwa economic hitmens zinaweza kukuongezea uelewa wa jinsi gani ivi vitu vinafanya kazi, inaumiza ila hatuna jinsi
 
Ndugai wewe ulikuwa muoga hata Jiwe ulimuunga mkono kiuoga tu!! sasa imekugharimu na huyu ni wewe usibishe!
 
Kuwa kiongozi mkuu wa muhimili mmoja mkubwa kati ya mitatu sio nafasi ndogo.
Ndugai wacha uongo!! hiyo ni kazi tena tamu sana km zilivyo kazi nyingine usitutishe hapa!! k vepi waiache wazi leo uone watu watakavyo changamkia! kma ni nafasi ndogo kwako siyo sisi!
 
Kuwa kiongozi mkuu wa muhimili mmoja mkubwa kati ya mitatu sio nafasi ndogo. Mzee alikuwa kwenye position ambayo kuna mambo lazima ayajue hata miezi, mwaka au miaka kadhaa kabla yetu sisi raia wa kawaida.

Kwa jinsi hali ilivyo kwa sasa, naanza kumuelewa alichokisema siku ile ambacho kilisababisha akapoteza nafasi yake. Huenda aliona mbali na hakutaka kushiriki huu udhalimu ndiyo maana wakamfanya walichomfanya.

Ukimya wa mrithi wake ndiyo hasa unaotia mashaka, maana pamoja na hali mbaya wanayopitia wananchi yeye kama kiongozi mkuu wa wawakilishi wa wananchi yupo kimyaaa.

Mawaziri nao ndiyo kabisaaaa wanatutukana live live kabisa, kwamba "Kama hatutaki tuhame nchi". Yani sisi wananchi tuhame nchi? Sisi wananchi? Sasa nadhani hajui kwamba kati ya uananchi na uwaziri kuna kimoja ni permanent na kimoja ni temporary.

Ndiyo maana nasema huenda Ndugai alikuwa anajua kinachopangwa na tunachoenda kukipitia wananchi. Japo na yeye huko nyuma alikuwa na makandokando mengi ila Mungu amuweke kwa kusimama kikataa kwenye jambo moja baya kati ya mengi.
View attachment 2333244

Ndugai hakupinga tozo, yeye alikuwa mfuasi na muumini mzuri wa tozo. Yeye alichokipinga ni mikopo tu...
 
Angekuwa serious angeachia ubunge aingie upinzani apambane kweli kweli tofauti na hapo ni tapeli tupu
Nyerere alisema upinzani halisi utatoka ndani ya chama tawala chenyewe. Si lazima kujiunga na chama cha upinzani. Ona sasa ni miaka 30 tangu upinzani uruhusiwe nchini. Nini walichoweza kufanya kubadili sera za taifa? Lakini mwana CCM akiwa jasiri kweli na kusema hoja zake ndani ya chama atasikilizwa. Ilianza kuonekana hivyo chini ya Magufuli na kama angemaliza miaka 10 ya uongozi bila shaka kungeonekana mabadiliko.
 
Nyerere alisema upinzani halisi utatoka ndani ya chama tawala chenyewe. Si lazima kujiunga na chama cha upinzani. Ona sasa ni miaka 30 tangu upinzani uruhusiwe nchini. Nini walichoweza kufanya kubadili sera za taifa? Lakini mwana CCM akiwa jasiri kweli na kusema hoja zake ndani ya chama atasikilizwa. Ilianza kuonekana hivyo chini ya Magufuli na kama angemaliza miaka 10 ya uongozi bila shaka kungeonekana mabadiliko.
Alikuwa zaidi ya shetani
 
Back
Top Bottom