Huko Kenya jeshi linakaribia kuwaunga mkono waandamanaji. Mageti ya bunge yamevunjwa na waandamanaji wapo ndani ya bunge wanafanya chochote watakacho

Huko Kenya jeshi linakaribia kuwaunga mkono waandamanaji. Mageti ya bunge yamevunjwa na waandamanaji wapo ndani ya bunge wanafanya chochote watakacho

Mganguzi

JF-Expert Member
Joined
Aug 3, 2022
Posts
1,604
Reaction score
3,715
Sauti ya umma imekita kambi huko Nairobi, Kenya! Hali imekuwa tete sana! Waandamanaji wamechoma moto ofisi ya gavana wa Nairobi na kuvamia bunge, bendera zote zimetelemshwa na mgahawa wa bunge umevunjwa, waandamanaji wameonekana wakila chakula na kutapanya kila kitu!

Jengo la Seneti limevunjwa na waandamanaji wameingia ndani ya bunge! Huku mamia wakilanda landa juu ya meza ya spika na kuharibu kila kitu! Yawezekana huu ukawa ndio ushindi wa kwanza wa waandamanaji kuwahi kufanyika Afrika Mashariki!

Utawala wa Ruto upo shakani na watabiri wa mambo ya siasa wanaona kuwa huu unaweza kuwa ndio mwisho wa utawala wa Ruto! Ajabu ni kuwa baadhi ya askari waliovalia mavazi ya jeshi wameonekana wakiwapatia maji ya kunywa baadhi ya waandamanaji jijini Nairobi na kuwapa nguvu ya kusonga mbele! Hii ni ajabu na hata walipoanza kuvunja mageti ya jengo la Seneti hakuna askari aliyejaribu kuwazuia!

Tuiogope sana dharau kwa tunaowaongoza. Kuna wakati binadamu huchoka pamoja na baadhi ya waandamanaji kupoteza maisha kwa kupigwa risasi na mabomu lakini bado raia wanasonga mbele.

PIA SOMA
- LIVE - Yanayojiri Maandamano Kenya: Waandamanaji wafika Bungeni, wawili wauawa kwa risasi
 
Ifike muda pia serikali ithamini vyombo vyake vya dola hao polisi wana nguvu ya kutosha kudhibiti maandamano ila wamejifanya kama wameshindwa hivi ili adhma itumie kwani wanachopigania raia kina faida na kwao askari.

Gharama zinapanda halafu mishahara ya askari ipo chini unategemea nini hapo!?
 
saiv nahis kama kuna nguvu ya mabepari nyuma ya hili suala
 
Hongereni sana wakenya Kwa kuchukua hatua.lakini watanzania wapuuzi kweli sijui wanazuiwa na Nini kwenda bungeni kuvunjavunja viti au kuchoma moto Hilo bunge zima
Fanya wewe mkuu wengine watafuata
 
Wanajeshi nao ni binadamu na pia jeshi liko siku zote kwa ajili ya kuwalinda wananchi , pia hizo tozo zinawaumiza wao na familia zao pia.
 
IMG-20240405-WA0001.jpg
 
Ifike muda pia serikali ithamini vyombo vyake vya dola hao polisi wana nguvu ya kutosha kudhibiti maandamano ila wamejifanya kama wameshindwa hivi ili adhma itumie kwani wanachopigania raia kina faida na kwao askari.

Gharama zinapanda halafu mishahara ya askari ipo chini unategemea nini hapo!?
Mmoja wao alierusha bomu juzi kwa wananchi akalipukiwa na mikono imekatika yote miwili, sijui kwa sasa anawaza nini au anafikiria nini akiwa kitandani hospitali.
 
Uongozi mzuri ni wa kifalme huu wa democracy ni ujinga sana. Hasara walioisababisha garama za maisha zitapanda zaidi
 
Back
Top Bottom