Jumbe Brown
JF-Expert Member
- Jun 23, 2020
- 12,077
- 12,786
Safari ya kupigania UELEWA ni ndefu mno.
Ni sawa na safari ngumu ya mtoto KUJIFUNZA.
Tulipo sipo pale pa JANA... kama Taifa tumetoka kupata habari magazetini, redioni mpaka kuja BLOGU, ziko zilizokuwa za UDAKU mpaka zile MAKINI.
Leo tuna FORUMS tofauti kama JAMII FORUMS (hakika ni hatua adhimu isiyoweza KUFANYIWA KEDI).
Kitu kigumu duniani ni kubadilisha UELEWA WA WATU (understanding) na kamwe TUSIWAONE MAADUI WENYE KUPITILIZA wale wote wenye UELEWA tofauti na kizazi chetu hiki chenye MABADILIKO MAKUBWA kiuchumi, kisiasa,kisayansi na kijamii.
Wako watu waitwao "wahafidhina," hawa si wa kuwatukana bali ni kuzidi kutumia NJIA BORA zenye kupeleka ujumbe MARIDHAWA ambao itafika SIKU watakuja kuuelewa tu. Kama HAWATAJIBIDIISHA kuelewa WAKIWA HAI basi watakuwa kama wale waitwao "GOYYIMS" na ndugu zetu WAYAHUDI.
Kizazi chetu na cha watoto wetu kinapitia zama zinazoonekana HATARI kubwa kwa NORMS zetu "WAAFRIKA" kitamaduni na hata kisiasa kwani UWAZI ULIOPITILIZA si miongoni mwa "elimu" ifundishwayo kuanzia UNYAGONI, JANDONI na masimulizi ya WAHENGA wetu, hapa ndipo ILIPO CHANGAMOTO kubwa kwa wale wanaoonekana FOREMEN wa kuyaleta "haya" mabadiliko MAPYA.
Kubwa ni kutambua kila zama zina mambo yake, na ni ngumu kwangu kuziishi zama alizoishi BABA WA BABU YANGU. Kubwa ni kuyachukua mazuri yao, kuyaboresha na kujua kuwa Kuna KESHO YANGU lakini pia kesho ya WAJUKUU ZANGU ambayo SITOWEZA KUIZUIA. Kubwa ni kuwakumbusha tu WASIZIACHE zile TUNU ADHIMU za UTU WA MWAFRIKA na TAMADUNI ZETU, kazi itakuwa ni kwao.
Tunaishi Katika dunia ya UTANDAWAZI ambao una changamoto zake ila hauwezi KUZUILIKA wala KUKATALIKA na jamii za walimwengu.
Hapohapo hatuna budi kutii SHERIA zilizopo...kubwa tu ni jukumu la WABUNGE WETU kutunga SHERIA zisizo za KUKOMOANA...na pia SHERIA zinazoendana na CHANGAMOTO YA DUNIA YA SASA.
Kama Taifa ni IMANI yangu kubwa TUTAFIKA kwa kila mmoja wetu kumuelewa MWENZAKE though it takes time ila DESTINATION hiyo HAITOEPUKIKA.
Ni sawa na safari ngumu ya mtoto KUJIFUNZA.
Tulipo sipo pale pa JANA... kama Taifa tumetoka kupata habari magazetini, redioni mpaka kuja BLOGU, ziko zilizokuwa za UDAKU mpaka zile MAKINI.
Leo tuna FORUMS tofauti kama JAMII FORUMS (hakika ni hatua adhimu isiyoweza KUFANYIWA KEDI).
Kitu kigumu duniani ni kubadilisha UELEWA WA WATU (understanding) na kamwe TUSIWAONE MAADUI WENYE KUPITILIZA wale wote wenye UELEWA tofauti na kizazi chetu hiki chenye MABADILIKO MAKUBWA kiuchumi, kisiasa,kisayansi na kijamii.
Wako watu waitwao "wahafidhina," hawa si wa kuwatukana bali ni kuzidi kutumia NJIA BORA zenye kupeleka ujumbe MARIDHAWA ambao itafika SIKU watakuja kuuelewa tu. Kama HAWATAJIBIDIISHA kuelewa WAKIWA HAI basi watakuwa kama wale waitwao "GOYYIMS" na ndugu zetu WAYAHUDI.
Kizazi chetu na cha watoto wetu kinapitia zama zinazoonekana HATARI kubwa kwa NORMS zetu "WAAFRIKA" kitamaduni na hata kisiasa kwani UWAZI ULIOPITILIZA si miongoni mwa "elimu" ifundishwayo kuanzia UNYAGONI, JANDONI na masimulizi ya WAHENGA wetu, hapa ndipo ILIPO CHANGAMOTO kubwa kwa wale wanaoonekana FOREMEN wa kuyaleta "haya" mabadiliko MAPYA.
Kubwa ni kutambua kila zama zina mambo yake, na ni ngumu kwangu kuziishi zama alizoishi BABA WA BABU YANGU. Kubwa ni kuyachukua mazuri yao, kuyaboresha na kujua kuwa Kuna KESHO YANGU lakini pia kesho ya WAJUKUU ZANGU ambayo SITOWEZA KUIZUIA. Kubwa ni kuwakumbusha tu WASIZIACHE zile TUNU ADHIMU za UTU WA MWAFRIKA na TAMADUNI ZETU, kazi itakuwa ni kwao.
Tunaishi Katika dunia ya UTANDAWAZI ambao una changamoto zake ila hauwezi KUZUILIKA wala KUKATALIKA na jamii za walimwengu.
Hapohapo hatuna budi kutii SHERIA zilizopo...kubwa tu ni jukumu la WABUNGE WETU kutunga SHERIA zisizo za KUKOMOANA...na pia SHERIA zinazoendana na CHANGAMOTO YA DUNIA YA SASA.
Kama Taifa ni IMANI yangu kubwa TUTAFIKA kwa kila mmoja wetu kumuelewa MWENZAKE though it takes time ila DESTINATION hiyo HAITOEPUKIKA.