Hukumu ya Mdude Nyagali ni leo 14|06|2021

Hukumu ya Mdude Nyagali ni leo 14|06|2021

The Sheriff

JF-Expert Member
Joined
Oct 10, 2019
Posts
747
Reaction score
2,112
Leo Juni 14,2021 ni siku ya Hukumu ya Mpaluka Nyagali Mdude (32) kwa jina maarufu Mdude CHADEMA.

Namuombea Mdude, Hakimu atakaye soma hukumu Mwenyezi Mungu ampe Hekima kama ya Mfalme Suleiman.

Awali Upande wa mashtaka umemuondolea kada wa chadema, mdude nyagali shtaka la uhujumu uchumi lililokuwa likimkabili na kumfungulia shtaka la jinai la kusafirisha dawa za kulevya.

Inadaiwa Mdude CHADEMA ambaye ni mkazi wa Itezi Jijini mbeya, kakamatwa na kushitakiwa kwa tuhuma za kupatikana na unga unaodhaniwakuwa ni dawa za kulevya aina ya heroine. kufuatia taarifa za kiintelijensia zilizopatikana, mtuhumiwa alikamatwa mnamo tarehe 10.05.2020 majira ya saa 17:00 jioni katika msako.

Mara baada ya kukamatwa kwa huyu mtuhumiwa, polisi walikwenda nyumbani kwake mtaa wa mwasote – itezi jijini mbeya kwa ajili ya kufanya upekuzi na katika upekuzi huo kulikutwa busta tano [05] za unga udhaniwao kuwa dawa za kulevya aina ya heroine wenye uzito wa gram 23.4 ambao ulikuwa umehifadhiwa kwenye mfuko wa kaki ambao ndani yake kulikuwa na mifuko midogo miwili ya nylon. Pia matumizi ya dawa za kulevya ni kinyume na sheria ya udhibiti, utumiaji na usafirishaji wa dawa za kulevya ya mwaka 2015 kama ilivyofanyiwa marekebisho mara kwa mara.

Zaidi, soma: Mbeya: Mpaluka Nyagali Mdude akamatwa na Heroin, apandishwa kizimbani akikabiliwa na mashtaka ya Uhujumu Uchumi

- Mbeya: Mahakama imeahirisha kusoma hukumu ya Mdude Nyagali hadi Juni 28, 2021

Mdude.jpg

Mdude 1.jpg
 
Kila lakheri Mdude Mpaluka Nyagali

Japo aina ya Lugha ulizokuwa unatumia sikubaliani nazo
Lakini naungana na watanzania na watu wote Ulimwenguni kukuombea uweze kushinda jaribu hili siku ya leo.
Mwenyezi Mungu aonae silini asikupungukie hata kidogo, yeye aonae silini akutimizie haja za moyo wako siku ya leo.

 
Dua zangu za leo nimezielekeza huko kwa Mdude Nyagali aka Kiboko ya Ibilisi.
 
Kesi ya kubambikiwa madawa kwa kumtumia bint toka Arusha. Hata akifungwa Mungu yupo atalipiza kwa wote waliofanya hivo tena kwa KUFA kama alivyotufanyia miezi kadhaa
 
Mdude ni Kati ya vijana walioonewa vya kutosha na mwendazake.aliwahi kutekwa tukapiga kelele akaachiwa.Now wameamua kumpa kesi ya madawa ya kulevya bila aibu.

Hivi polisi wa nchi hii tukisema kwamba ninyi ndio wauzaji wakubwa wa dawa za kulevya mtakataa..hizo dawa alizoshikwa nazo mdude bila shaka ninyi ndio mliopandikiza, mlizotoa wapi, mlikuwa nazo kwa malengo Gani. Na je, ni kiasi Gani bado mnacho?

Mama samia naomba ulisuke upya hili jesho la polisi ni Moja Kati ya majeshi ya hovyo haijawahi kutokea. Huwezi kwenda polisi wakakuhudumia bila ya kutoa rushwa, labda kama mnafahamiana ndio akuonee aibu. Hawana huruma wala mapenzi na kazi yao.

Mnakumbuka ni jeshi hiki hili liliwahi kutoa ripoti kwamba wameua majambazi, baada ya uchunguzi kufanyika ikagundulika ni wafanya biashara, yaani wengi wao hawa ni majambazi wanaolindwa na dola.

Ikiwezekana kiundwe chombo pembeni ya kulifwatilia hili jeshi, yani polisi wakisema tumeua majambazi matano kwenye mashambulio. Hiki chombo kifwatilie kama kweli kulikuwa na shambulio na kama kulikuwa na umuhimu au uhalali wa hao majambazi kuuliwa wakisena kakamatwa na dawa wafwatiliwe kama ni kweli. Hapo watanyooka.

Juzi tubkuna Mzee wa Arusha walimwekea kipande cha pembe za ndovu wakamwambia atoe mill mia Moja, yaani hili jeshi lisukwe upyaa hawa waliopo wengi ni mizigo.
 
  • Thanks
Reactions: PNC
"Mwambieni huyo anaejiita Rais wa wanyonge, mnyonge ni Bibi yake sisi sio wanyonge"-Mheshimiwa Mdude Nyagali.

My take:Marehemu mpakwa mafuta aliamini kuwa yeye ni Mungu wa Tanzania na kumwambia maneno kama haya ni sawa na kuinajisi nchi ya Tanzania.
 
Mwenda zake alikua mtu WA ajabu
Sana udikteta ulimzid

Kenya rais WA Kenya aliwah kuitwa
Mbwa akiwa na mama yake na
Aliemtus hakumfanya kitu na alikua mbunge wa upinzan
 
"Mwambieni huyo anaejiita Rais wa wanyonge, mnyonge ni Bibi yake sisi sio wanyonge"-Mheshimiwa Mdude Nyagali.

My take:Marehemu mpakwa mafuta aliamini kuwa yeye ni Mungu wa Tanzania na kumwambia maneno kama haya ni sawa na kuinajisi nchi ya Tanzania.
View attachment 1818241
Hiyo mimba uliyodungwa na mwendazake itakutoa roho kwa siku lazima umtaje mara 62!

Mdude alikamatwa na cocaine za mbowe akizisambaza mikoa ya nyanda za juu kusini
 
Huyu dogo hana heshima kabisa, ukiachana na cheo, Magufuli ni sawa na baba yake kiumri. Hakupaswa kumtolea maneno kama hayo.

CHADEMA fundisheni vijana wenu maadili sio kun fu tu.
We naye huna hata akili...hapo kuna neno gani baya unalooona km siyo la heshima!?? Kukataa kuitwa wanyonge au au kusema mnyonge ni bibi yake!?? Nyie wajinga ndo mlimfanya mwendazake ajione amekamilika kila kitu!
 
Huyu dogo hana heshima kabisa, ukiachana na cheo, Magufuli ni sawa na baba yake kiumri. Hakupaswa kumtolea maneno kama hayo.

CHADEMA fundisheni vijana wenu maadili sio kun fu tu.
We naye huna hata akili...hapo kuna neno gani baya unalooona km siyo la heshima!?? Kukataa kuitwa wanyonge au au kusema mnyonge ni bibi yake!?? Nyie wajinga ndo mlimfanya mwendazake ajione amekamilika kila kitu!
 
Report Za Maendeleo Ya Jamii - Serikali Ya Awamu Ya 5.

1) Muuza kuku (Mr Kuku) abambikizwa kesi ya uhujumu uchumi na kutakatisha fedha zaidi ya Billioni 1 na usheee.

2) Muuza spare za simu (Mdude) akabambikizwa kesi ya kusafirisha madawa ya kulevya kutoka pakistani kwenda mbeya wakati hata passport wala kitambulisho cha NIDA hajawahi kumiliki.

3) Mwandishi wa habari Azory Gwanda apotea na watu wasiojulikana, walifika usiku wa manane na kumchukua nyumbani kwake, yasemekana walimwambia wanaenda matembezi.
 
Huyu dogo hana heshima kabisa, ukiachana na cheo, Magufuli ni sawa na baba yake kiumri. Hakupaswa kumtolea maneno kama hayo.

CHADEMA fundisheni vijana wenu maadili sio kun fu tu.
Kwahiyo heshima ni kukubali kuwa wewe ni mnyonge?
Nyie watu hamna utofauti na misukule, karne ya 21 bado mnaendelea kuishi kitumwa ilimradi muende chooni.
 
Back
Top Bottom