Humphrey Polepole: Rais Magufuli anatekeleza Katiba Mpya

Humphrey Polepole: Rais Magufuli anatekeleza Katiba Mpya

Hiyo katiba mpya kaipitisha Magufuli peke yake mpaka aifate au mpaka wananchi wapige kura ya maoni,tueleweshane hapa maana labda mambo yashabadilika wengine hatujui.
 
Kwahiyo Rais hailindi na kuitetea pia hahifadhi Katiba aliyoapa kuilinda?[emoji15]
 
Tunataka chanel zile za bure zirudishwe la sivyo waturudishie analogia yetu maana antena bado tunazo. Hii ni laana na unyonyaji mkubwa kwa kutaka kuwakamua maskini wa nchi hii kila walichonacho.
 
Hiyo katiba mpya kaipitisha Magufuli peke yake mpaka aifate au mpaka wananchi wapige kura ya maoni,tueleweshane hapa maana labda mambo yashabadilika wengine hatujui.
Kigezo cha kuteuliwa lazima uwe kada..! Umsifie baba Muumb.. Uteuzi emezingatia vigezo na masharti kuzingatiwa.
 
Sasa huyu ndiye Polepole ambaye ni summit member of 'gt' na yupo hapa kama a verified user, hivi ndio Tanzania inaangamia nasi tukiona kweli!?
 
Polepole anataka kutuaminisha kuwa hakuna haja ya kuwa na Katiba Mpya kwa mwelekeo wake. Inavyoonekana tayari anaanza kusahau hata kile alicho ahidi hivi majuzi kuwa hatakaa kusaliti kile alichokuwa amesimamia kwenye suala la Katiba. Kweli Madaraka matamu, naam ni matamu zaidi ya asali.

Kwani referendum imefanyika yaani wananchi wamefanya maamuzi? Au wamefanya wao kwa niaba ya wananchi kwa style ya kwata ya kimyakimya? Kama wamefanya hivyo ni kuvunja sheria ya marekebisho ya katiba na haina uhalali na yanayofanyika kwa mujibu wa rasimu hayana uhalali kwa sababu sio official, hayatambuliki na wenye power=wananchi.
 
Polepole amekeua joka la kibisa hashuhuliki amekua waliwali.

nilimuona akiongea hayo mashudu chanel ten nilisikitika sana.
 
Ukitaka kujua tabia ya mtu mpe hela...haya ni ya kawaida kutokea Tz hata wazr flani aliruka andiko lake lakitaaluma juu ya katiba...wako waliomkana hata Yesu...
 
Huyu jamaa nilikuwa namheshim sana kipindi kile yuko tume ya katiba nashangaa nini kimempata leo hii haipiganii tena rasimu ile alitumia nguvu kushiriki kuiandika na kuitangaza.

Juzi kwenye mahojiano anadai eti rasimu ya warioba inafanyiwa kazi na magufuli tayari sasa najiuliza maoni kma wabunge wasiwe mawaziri limetekelezwaje na magufuli, muundo wa muungano,tume huru, maadili na miiko ya uongozi,kupunguza majimbo na nguvu za rais pia kufuta post kma za ukuu wa wilaya hizo zote zinatekelezaje ndani ya katiba ya sasa???

Hivi kweli polepole anaamini kwenye fikra wa mtu mmoja sio mfumo?? Sasa ikitokea magufuli kastaafu na kaja rais mwingine kipi kitamfunga wakati katiba mpya haipo kiuhalisia ila ipo kwenye FIKRA TU ZA MAGUFULI PEKE AKE??

Hivi kweli ina maana polepole hajui katiba ingesaidia mambo muhim ya nchi yapewe muongizo tayari ili hta aje rais dhaifu vp atabanwa tu afuate muongozo ule???

sasa nashangaa mtu aliyeamini katiba ingemdhibiti rais leo hii anaamini rais ndio anaitekeleza katiba isiyoonekana this is so low na offcially nimemfuta polepole kma mzalendo wa kweli na role modal kwenye harakati hizi za mageuzi ya kudai katiba mpya huyu amekuwa msaliti wa ndoto za mamilion ya watanzania waliotoa maoni yao kwa tume hii.
 
Tunataka chanel zile za bure zirudishwe la sivyo waturudishie analogia yetu maana antena bado tunazo. Hii ni laana na unyonyaji mkubwa kwa kutaka kuwakamua maskini wa nchi hii kila walichonacho.
Mkuu unaweza ukawa na hoja dadavua kiufasaha tupate mantiki yako.
 
Mwanasiasa yoyote yule sio wa kumuamini hata awe baba/mama yako.
 
Kwani referendum imefanyika yaani wananchi wamefanya maamuzi? Au wamefanya wao kwa niaba ya wananchi kwa style ya kwata ya kimyakimya? Kama wamefanya hivyo ni kuvunja sheria ya marekebisho ya katiba na haina uhalali na yanayofanyika kwa mujibu wa rasimu hayana uhalali kwa sababu sio official, hayatambuliki na wenye power=wananchi.
Tayari ameleo Ukatibu Wenezi huko CCM. Nchi za Afrika kweli tuna safari kufikia kujitambua. Sijui umasikini aka laana inatutafuna, kwakweli inasikitisha.
 
Back
Top Bottom