Huna marafiki wa kweli, tusidanganyane

Huna marafiki wa kweli, tusidanganyane

Equation x

JF-Expert Member
Joined
Sep 3, 2017
Posts
33,679
Reaction score
49,841
Wengi tunaamini wale watu wanaotuzunguka katika mazingira yetu ya kila siku ndio marafiki wa kweli; iwe tunakutana nao maeneo ya starehe kama bar, sehemu za miziki, harusini, au sherehe yoyote; iwe tunakutana nao makazini, idarani, chamani n.k; iwe tunakutana nao misibani, mahospitalini n.k, iwe tunakaa mtaa mmoja, majirani n.k

Ila ukweli wale sio marafiki, bali ni watu wakubadilishana nao tu mawazo kutokana na mazingira mliopo. Watu wengi hukosea na kuamini watu wanaokutana nao katika mazingira hayo wanaweza kuwa marafiki wa kweli; ila ukweli unakuja kugundulika baada ya kuangukia pua, pale utakapowahitaji na hawatakuwepo, zaidi ya wewe mwenyewe kupambana na hali yako na haijalishi uliwekeza kiasi gani kwao.

Kwa kifupi kupata rafiki wa kweli, ni mchakato mrefu sana zaidi ya unavyotafuta mchumba; ambaye mtafanana mitazamo, ambaye wewe ukisema ‘yes’ naye atasema ‘yes’ akisema ‘no’ naye atasema ‘no’.

Na hii itapelekea kuwa na umoja wenu kutokana na idadi mliopo, mfano; ‘the big three’, ‘the big five’ n.k

Kuna video moja ilirekodiwa hospitali moja huko nje, jamaa amelazwa hospitalini anapumulia oxygen, marafiki zake wamekuja kumuona hapo hospitalini, wahudumu wakawa wanawaambia muda wa kumuona mgonjwa umeisha mnatakiwa muondoke; wale marafiki zake walikataa, wakasema tutakaa naye hapa hapa mpaka dakika ya mwisho na hatutaondoka, kama kuna mahitaji yoyote yanatakiwa yapatikane, yatakuja wao wakiwa pale pale.

Je hao wasaka tonge wako ulionao, wataweza kuwa kama hao marafiki wa jamaa?​
 
Hilo mbona liko wazi..ndomaana tunawaambia kataa ndoa kila siku oeni...kaeni na wake..hao ndo kidogo pamoja na shido zao ila ni rafiki wa kweli...kingine nikuulize kitu gani ambacho unataka uwekeze sana ili ukiangukia pua uone hujasaidiwa...ninachojua life hakuna fairness hakuna huruma ..so ishi nao tu ila kamwe usimkopeshe rafiki hela kubwa mimi nishajua marafiki zangu ni wa kunywa nao pombe na kifanya nao kazi ..basi...so siwekezi hela kwao labda time tu
 
Hilo mbona liko wazi..ndomaana tunawaambia kataa ndoa kila siku oeni...kaeni na wake..hao ndo kidogo pamoja na shido zao ila ni rafiki wa kweli...kingine nikuulize kitu gani ambacho unataka uwekeze sana ili ukiangukia pua uone hujasaidiwa...ninachojua life hakuna fairness hakuna huruma ..so ishi nao tu ila kamwe usimkopeshe rafiki hela kubwa mimi nishajua marafiki zangu ni wa kunywa nao pombe na kifanya nao kazi ..basi...so siwekezi hela kwao labda time tu
Hao sio marafiki bali ni watu wa kampani tu
 
Katika wengi niliokutana nawo,naweza kusema mimi ndiyo nilikuwa mkweli kwao,lakini jinsi wanavyokaa na kuigiza,kufuatilia maisha yako nk...nilichoka kuwaweka karibu hawo wadudu.kuna wengine wao kila siku wanaomba msaada wa hela,na kazi wanafanya ila elasijui huwa wanapeleka wapi. Binafsi siwezi kumuita mtu rafiki kwa sababu hakuna rafiki mzuri zaidi ya yule ninaemuona kwa kioo.
 
Katika wengi niliokutana nawo,naweza kusema mimi ndiyo nilikuwa mkweli kwao,lakini jinsi wanavyokaa na kuigiza,kufuatilia maisha yako nk...nilichoka kuwaweka karibu hawo wadudu.kuna wengine wao kila siku wanaomba msaada wa hela,na kazi wanafanya ila ela zao wanapeleka wapi. Binafsi siwezi kumuita mtu rafiki kwa sababu hakuna rafiki mzuri zaidi ya yule ninaemuona kwa kioo.
Uko sahihi, kila mtu kwa mtazamo wake anajua rafiki wa kweli ni yupi, ukirejea kwenye mada kwa mfano nilioutoa wa video, inatafsiri huyo rafiki wa kweli anatakiwa aweje.
Kutokana na changamoto za kiuchumi, wengi tumekuwa na urafiki wa kuigiza, mtu ataigiza kwa kuwa ananufaika na kitu fulani na si zaidi ya hapo.​
 
Urafiki ni kitu kizito sana na urafiki sio ukisema ndio na yeye aseme ndio. Urafiki sio kukubaliana kwa kila kitu bali kuambiana ukweli hata kama unamkera mwenzio kwa sababu unachojali ni maendeleo yake zaidi kuliko atajihisije.

Urafiki ni kufurahia maendeleo ya mwenzako genuinely hata kama anakupita

Urafiki ni kujitoa, urafiki ni kutokuhesabiana fadhila, urafiki ni bond kubwa kwa mtu ambaye hamna uhusiano wa damu.

Ukipata rafiki kwa maisha haya ni achievement kubwa japo ni kheri usiwe nao kuliko kuwa nao ambao si sahihi

Urafiki wa kweli upo ila ni nadra kuupata
 
Back
Top Bottom