Hussein Ramadhan'Sharo Milionea' aibiwa nguo zote alizokuwa amevaa kabla ya ajali.

Hussein Ramadhan'Sharo Milionea' aibiwa nguo zote alizokuwa amevaa kabla ya ajali.

Tatizo ni kubwa kwani hata polisi wakiwahi eneo la ajali huwa wanaiba simu na kuwa search majeruhi na maiti mifukoni kama wana hela. Hii hufanyika faster pale wanapowafukuza raia huku wenzao wakiingia kazini. Ila si polisi wote.
 
Double standard Government hizi ni mbinu za kutuondoa kwenye mijadala ya Kitaifa na kutulisha habari za kijinga, wakati haya ni matukio ya kila siku kwenye barabara zetu. Why Sharo is so special?

Mkuu,

Hivi mijadala ya kitaifa ndiyo ipi hiyo kama kinachojadiliwa hapa ni jambo linaloihusu jamii kama linavyoainishwa na wengi hapa janvini. Kama mambo kama haya yanafanyika kila siku kwa fikra zako basi hayapaswi kujadiliwa.

Kila jambo lina sehemu ya kuanzia. Na mjadala umeanzia kwa Sharo even if is not special but is Tanzanian like you.

Mkuki kwa nguluwe ni mtamu lakini kwa binadamu ni mchungu. God forbid, kama jambo hili lingetokea kwa mtu ambaye yuko karibu yako, naamini usingeliona kama siyo special na lisilohitaji mjadala wa 'kitaifa'.
 
Usisituke mkuu, kusema kweli ni jambo la kawaida marehemu kuibiwa kwenye ajali na ndo maana halisi ya ule msemo kufa kufaana. Na mbaya zaidi sometime hata majeruhi huwa wanamaliziwa ili kupoteza ushahidi. Kuna jamaa yangu ilibidi awambie vibaka, ''Jamani msiniibie mimi bado ni mzima''

God forbid. Sijui kama taifa tunaelekea wapi.
 
Kwa hiyo inataka kusema kuwa aerikali inajiendesha kukwepa mijadala kwa kusubiria matukioo na kuyashadadia..nn haswa kilipo kwa taarifa ya mkuu wa wilaya tena muheza inazuia nyie msizungumzee hiyo mnayoita mijadala..achane kuwaa wagonjwa.ukiacha fremansons hii homa nyingine kwenuu
.[
QUOTE=Matola;5126157]Double standard Government hizi ni mbinu za kutuondoa kwenye mijadala ya Kitaifa na kutulisha habari za kijinga, wakati haya ni matukio ya kila siku kwenye barabara zetu. Why Sharo is so special?[/QUOTE]
 
Mkuu wa Wilaya amesema watu warudishe mali za SHARO ikiwemo ngu alizovaa na kwa kuwa wanajulikana waliochukua?!!! Hivi wale waliochukua bag na camera ya Mwangosi si wanajulikana maana walimuua na kuondoka na kila kitu chake? Wamechukuliwa hatua gani kisheria? Niliona familia inakusudio kuidai serikali au niseme Jeshi la polisi!!! Watafanikiwa?? Maovu yamezidi na mbaya zaidi hata vile vyombo vy usalama tunavyoviamini tunaviogopa kama ukoma sasa!!
 
Mkuu wa Wilaya amesema watu warudishe mali za SHARO ikiwemo ngu alizovaa na kwa kuwa wanajulikana waliochukua?!!! Hivi wale waliochukua bag na camera ya Mwangosi si wanajulikana maana walimuua na kuondoka na kila kitu chake? Wamechukuliwa hatua gani kisheria? Niliona familia inakusudio kuidai serikali au niseme Jeshi la polisi!!! Watafanikiwa?? Maovu yamezidi na mbaya zaidi hata vile vyombo vy usalama tunavyoviamini tunaviogopa kama ukoma sasa!!

Mkuu,
makosa ni makosa tu. Hatuwezi kuharalisha kosa kwa kufanya kosa.
 

Mkuu,
makosa ni makosa tu. Hatuwezi kuharalisha kosa kwa kufanya kosa.

Mkuu sijahalalisha kosa ile nimeandika kimafumbo kidogo kuwa vile vya marehemu Mwangosi ilijulikana wazi kabisa vilichukuliwa na nani na hivi pia!! So ni vema fair justice ifanyike!!!
 
Ni aibu iliyoje kwa nchi ambayo tunajivunia umoja wa kuzungumza lugha moja! Umasikini si kigezo bali ukosefu wa roho ya utu. Inafika wakati pindi inapotokea ajari hata wale kweli wanaokuja kwa moyo wa kusaidia unawaona kama vibaka. Hivi tunaelekea wapi?
 
Mkuu sijahalalisha kosa ile nimeandika kimafumbo kidogo kuwa vile vya marehemu Mwangosi ilijulikana wazi kabisa vilichukuliwa na nani na hivi pia!! So ni vema fair justice ifanyike!!!

Mkuu,
Hapo nimekuelewa.

Hili ndilo tatizo kwa Polisi Tanzania. Wana profile case kitu ambacho ni unfair kwa jamii na kwa kufanya hivi, jamii inapoteza hata imani na utendaji wao as a result, watu wanaanza kuchukua sheria mikononi mwao.

Siyo kitu cha kushangaza pale watu wanapoanza kuwaita Polisiccm kutokana na profiling ya kesi mbalimbali.
 
Hili ni jambo la kawaida sana ajali inapotokea.Nakumbuka nilikuwa natoka Dar - Arusha tyre ya mbele ya gari tulilokuwa tukisafiria lilipancha maeneo ya Maili kumi [Korogwe] gari likaacha njia likaingia maporini bahati nzuri halikupinduka ndani ya dakika 5 tulikuwa tumezungukwa na vibaka kama hatukuwa na silaha tungekoma tukapiga risasi moja hewani wakatawanyika.Sasa pata picha Sharo alikuwa mwenyewe,keshakufa ana vitu vizuri nguo,fedha,simu na nk.

Mkuu hiyo silaha yako unakodisha?
 
Mkuu,
Wow, mbona umenishitua unaposema jambo la kawaida kabisa. Yaani kwa Tanzania marehemu kuibiwa mpaka nguo alizovaa?
Unashangaa nini mambo ya Tanzania ndugu yangu? Kama ukiwa umeumia wanaweza hata kukudhuru zaidi ili wachukue mali zako unashangaa kwa marehemu kuibiwa?
 
Double standard Government hizi ni mbinu za kutuondoa kwenye mijadala ya Kitaifa na kutulisha habari za kijinga, wakati haya ni matukio ya kila siku kwenye barabara zetu. Why Sharo is so special?

Mijadala ya kitaifa inafanyika wapi...miafrika bana. Huyu dogo kuibiwa vitu vyake baada ya ajali ni habari ya kijinga.
 
Maisha bora kwa wote.

Umasikini ukichanganyika na ujinga pamoja na kupokwa milingano... habari kama hizi zitasikitisha, lakini nashangaa kwa nini hatuna mbaya zaidi.

Wait, tunazo. Majambazi wanavamia magari na kuwafanyia abiria mbaya.
 
Rekebisha kichwa cha habari. Wizi umetokea baada ya ajali na si kabla ya ajali. Ina maana alikuwa anaendesha gari akiwa tayari alishaibiwa nguo.

Rekebisha namna ya usomaji wako' nguo alizokuwa amevaa kabla ya ajali' yawezekana alikuwa na nguo zingine ambazo hakuzivaa lakini kikubwa ni wizi wa nguo alizokuwa amevaa na kupata nazo ajali,sioni kama heading ina tatizo lolote, KABLA YA AJALI ALIKUWA AMEVAA NGUO NA ZOTE ZIKAIBWA ALIPOPATA AJALI...
 
Hayo mambo ni ya kawaida kwa wanavijiji wanaoishi pembezoni mwa barabara kuu zote sirikali inalitambua hilo! Nchi inaangamia.
 
Back
Top Bottom