Huu hapa ukweli kuhusu majini (eneo ambalo wanapatikana kwa wingi jijini Dar es Salaam)

Huu hapa ukweli kuhusu majini (eneo ambalo wanapatikana kwa wingi jijini Dar es Salaam)

Sio mimi niliowaitwa wenzangu wajinga wakati maelezo yako hayana uthibitisho 100% kwahio nadhani kuwaita wajenga hatuwatendei haki huenda mimi na wewe ndio wajinga hatuelewi na wenyewe ndio werevu (tunachodhani ndicho sisi kumbe sio)

Mfano mapepo yanayowapata watu kuna watu scientifically wanasema zile ni multiple personality disorder (sasa hapo wajinga ni wao au sisi)?...; Sijui lakini kuliko kushikana uchawi na majirani zetu ni bora tuka-treat hio multiple personality disorder....
Punguza ujuaji bro.

Najua umekaririshwa sana shuleni, lakini punguza munkari kidogo.
 
Dhana ya Mungu kuwapo ni coping mechanism kwa baadhi ya watu. Inawapa faraja kwamba hata kama wao hawana majibu ya maswali magumu, kuna Mungu anajua.

Hata kama wanapata matatizo, Mungu atasawazisha kwa haki siku moja.

Sasa, ukiwaonesha hawa watu kwamba huyo Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote hayupo, wanaona umewaondolea coping mechanism, umewaondolea identity kama viumbe wa Mungu, umewaondolea mengi sana.

Wengi wanakataa, hata kama ni kwa cognitive dissonance.
Acha ujuaji basi, kaah unaboa bwana mkuu
 
Punguza ujuaji bro.

Najua umekaririshwa sana shuleni, lakini punguza munkari kidogo.
Kati yangu mimi na wewe nani anajifanya mjuaji ?

Sio wewe ambaye unatuelezea kuhusu na kuwajua majini ? (Sasa hapo Mjuaji nani)?

Mbaya zaidi unalazimisha watu wakuamini / waamini vitu abstract...., In my book that is not Kosher
 
Acha ujuaji basi, kaah unaboa bwana mkuu
Kwani umeambiwa kusoma ninachoandika ni lazima?

Mimi watu wanaoni boa nimewaweka ignore list, unakaribishwa kuniweka ignore list usione chochote ninachoandika.

Mimi ushaniboa na nishakuweka ignore list, kuanzia hapa sitaona unachoandika.
 
Katika ulimwengu wa roho, Dar es salaam ni jiji ambalo wanaishi binadamu na majini..

Majini ni nini?

In my personal opinion which is based upon my personal understanding of the spiritual world, majini ni viumbe ambao kwa ujumla wao wapo more advanced in technology kuliko binadamu KWA ujumla wetu.

Ninapo sema kwa ujumla wao, majini wapo more advanced in technology kuliko binadamu simaanishi kwamba majini wote wapo more advanced in " technology" kuliko binadamu wote.

La hasha .

Ni SAWA na tunaposema Marekani ndio taifa lililo endelea kiteknolojia kuliko mataifa yote duniani, hatumaanishi kwamba every individual american is more advanced in technology than every person who is not an American.

La hasha. Wapo raia kutoka nje ya Marekani ambao wao KWA sababu ya mahaba yao kuhusu teknolojia wame yatafuta KWA kina maarifa kuhusu teknolojia kadha wa kadha na uki walinganisha katika ufahamu wao juu ya teknolojia na wamarekani wengi, utakuta raia hao wa mataifa nje ya Marekani Wana ufahamu mkubwa kuhusu teknolojia kuliko idadi kubwa tu ya wamarekani.

Wapo wahindi ambao wame ajiriwa Marekani kama wataalamu wa IT, Nuclear etc.

Vivyo hivyo kwa upande wa majini na binadamu.. Wapo binadamu wengi ambao Wana maarifa mapana kuliko majini...

Ninasema wao majini wameendelea kiteknolojia kuliko binadamu KWA maana ya kwamba uki chukua kiwango cha juu cha teknolojia kinacho milikiwa na majini ukalinganisha na kiwango cha juu cha teknolojia kinacho milikiwa na binadamu BASI kile kiwango cha juu cha teknolojia kinacho milikiwa na majini kipo juu zaidi ya kiwango kinacho milikiwa na binadamu wanao ishi katika sayari ya dunia. ( Nimesema binadamu wanao ishi katika sayari ya dunia kwa sababu ufahamu wangu unaniambia kwamba wapo viumbe wenye kufanana na binadamu " humanoids" ambao wanaishi kwenye sayari na makundi nyota ( galaxies) mengine.

Mungu ali tengeneza a billions of ADAM and EVE couples, ambao ali waplant kwenye mashamba ( sayari) yake mbalimbali yaliyopo katika galaxies tofauti tofauti KWA sababu ambazo nitazielezea wakati mwingine.

Marekani ndio taifa lenye teknolojia ya juu duniani lakini wamarekani wenye access na maamuzi juu ya hiyo teknolojia itumike vipi wanaweza wasizidi elfu mbili.

Vivyo hivyo kwa majini. Pamoja na kwamba Ufalme wa kijini kwa ujumla wake ( kuna falme nyingi sana za kijini ) una hodhi teknolojia ambayo ipo juu kuliko teknolojia tunayo hodhi binadamu lakini majini wenye access na hiyo teknolojia au wanao weza kutumia hiyo teknolojia wapo wachache sana.

Katika.matrilioni ya majini wanao ishi katika sayari ya dunia pamoja sayari mama yao katika mfumo wetu wa jua ( solar system) majini wenye access na teknolojia ya juu ya majini wapo chini ya elfu ishirini.

Sayari mama ya majini katika mfumo wetu wa jua ni VENUS. Huko ndipo yalipo makao makuu ya majini katika ukanda huu wa kinyota.

Majini hawaishi BAHARINI. Tunafikiri majini wanaishi BAHARINI KWA sababu kwenye bahari yetu upande wa bahari ya Hindi ndipo kulipo na short cut ya kwenda kwenye sayari ya Venus.

Duniani yapo maeneo saba katika ulimwengu wa roho ambayo ni njia panda zinazo ikutanisha sayari ya Venus na sayari ya dunia.

Maeneo hayo yapo katika bahari ya Hindi katika mikoa ya Dar es salaam, Tanga,Lindi,Mtwara, eneo la Unguja, Pemba na eneo jingine lipo nchini India.

Katika maeneo hayo ndipo ulipo njia ya short cut kutoka kwenye sayari ya dunia HADI ilipo sayari ya Venus yalipo makao makuu ya majini katika ukanda huu wa kinyota.

Kikawaida/.kisayansi( KWA teknolojia ya binadamu) safari kutoka duniani HADI ilipo sayari ya Venus huchukua siku 109.

Lakini kwa teknolojia ya kijini safari kutoka duniani HADI kwenye sayari Venus kupitia BAHARINI, hutumia dakika saba.

Ndio zile habari ulizo kuwa ukisimuliwa utotoni kwamba mtu akienda bahari saa tisa usiku na mayai saba ya ndege mmoja wa porini yaliyo fanyiwa vitu fulani fulani halafu akatamka Maneno fulani kisha akayatupa mayai hayo BAHARINI BASI bahari hupasuka na huonekana jiji zuri la dhahabu ambalo limeendelea kuliko duniani na kuna viumbe kama watu wanaishi huko plus kuna watu maarufu kutoka duniani wapo huko.

Huko ndipo ambapo wanadamu hupaita kuzimu.

Ndio maana husemwa umbali kutoka duniani HADI kuzimu ni kilometa sifuri.

ITAENDELEA KESHO.

MAHALI AMBAPO MAJINI WANAPATIKANA KWA WINGI JIJINI DAR ES SALAAM.

Jijini Dar es salaam yapo maeneo kumi na moja ambako hawa viumbe majini WANAPATIKANA KWA wingi sana.

Kati ya maeneo kumi na moja lipo eneo moja ambalo viumbe hao hupatikana kea wingi zaidi.

Huko bara Mizimu ni roho za watu walio fariki zamani au majini wa watu walio fariki. Yani kwamba KILA mtu anakuwaga na jini wake kwenye mwili wake. Huyu mtu akifa roho yake hurejea mbinguni lakini huyu jini wake hubaki duniani kuendeleza mahusiano na ndugu wa marehemu.

Lakini kwa washirikina na wachawi wa pwani, mizimu ni majini walio kusanyika sehemu moja kwa wingi.

SASA KWA washirikina na wachawi wa viwango vya juu waliopo jijini Dar es salaam, eneo hili ninalo lisema hujulikana kama Mizimuni (.Sio Kawe Mzimuni)

Huitwa Mizimuni kwa sababu katika eneo hilo kuna.idadi kubwa sana ya majini. There is an active djinn city in the area.

Kama umewahi kupewa dawa yoyote ile ya kichawi ukaambiwa nenda kaichome au kaifanye hivi vile nakadhalika ukafanya hivyo ukiwa ndani ya jiji la Dar es salaam na dawa hiyo isifanye kazi bas probably hukufanya jambo hilo katika eneo ambalo majini wapo active..

Ukifanya uchawi wowote ndani ya eneo hilo uchawi huo hupata majibu ya papo KWA papo.

KWA mfano watu wengi hawajui kuhusu kazi ya mafusho mbalimbali. Kazi kubwa ya mafusho ni kufungua anga la majini husika.

Chochote cha kishirikina unacho kifanya katika eneo hilo hutoa majibu ya papo KWA papo KWA sababu majini wapo active sana katika eneo hilo. Chochote kuanzia mafusho, kafara nakadhalika.

Je ni wapi mahali hapo? Usisumbuke kuni dm KWA sababu sitokwambia chochote ingawa nina pajua.

Ni mwiko kutoa siri hii. Unacho takiwa kufanya ni wewe mwenyewe kuanza kutembelea KILA kata ya jijinla dar es salaam na kufanya hizo kafara au kuchoma mafusho kupingana na siku husika. Mwisho wa siku utapajua ni wapi kupitia majibu utakayo yapata katika sehemu husika.

Kuisaidia tu muda mzuri wa kufanya hivyo ni usiku kuanzia saa tisa.

JE MAJINI HUFA?

Ndio majini HUFA.

JE MAJINI WATAIONA PEPO ?

(Jibu langu halitokani na ulicho fundishwa kwenye dini yako Ila linatokana na ufahamu wangu kuhusu majini)

Majini wote wazuri KWA wabaya hawata iona pepo.

Kwanini?

Pepo wamehaidiwa binadamu tu.

Majini wamenyimwa pepo KWA sababu GANI?

KWA mujibu wa elimu halisi ya majini. Majini wamenyimwa pepo KWA sababu huishi kwa maelfu ya miaka.

KWA mujibu wa elimu ya majini. Viumbe wanao ishi miaka mingi wakisha kufa ndio wamekufa. Hawapewi nafasi ya kuishi tena kwa mara nyingine. KWA hiyo majini na viumbe wengine ambao wanaishi miaka mingi sana hawana pepo KWA mujibu wa elimu ya majini..

Majini walipata wapi teknolojia yao?

Tofauti na watu wengi wanavyo fikiria kwamba eti majini waliumbwa wakiwa na ufahamu wa KILA kitu, majini hawa kuumbwa wakiwa Wana ufahamu wa KILA kitu.

They started with a very humble beginning.

When they start to live in this planet they were as dumb and ignorant as Adam and Eve.

Walijifunza mambo yote wanayo yafahamu leo hii kupitia challenges walizo kutana nazo..

Hata sisi binadamu hatu kuanza kurusha ndege. Tulijifunza kurusha ndege.

Binadamu bado tunayo nafasi ya kujua mambo mengi sana kuhusu hii dunia.

KWA mtazamo wangu. Binadamu watako kuja kuishi hapa duniani miaka elfu kumi ijayo watakuwa wanatucheka binadamu tunao ishi SASA hivi KWA kushindwa kwetu kupata maarifa yakutufanya tuishi milele.


JE MAJINI WANAJUA KILA KITU?


Hapana majini hawajui KILA kitu. Ila miongoni wapo majini wanao jua vitu vingi kutushinda sisi binadamu. Tofauti baina yetu sisi binadamu na majini katika maarifa ni kwamba huyu jini ambae hajui KILa kitu lakini anawajua majini ambao WANAJUA vitu vingi.

Anawajua sio kwamba ana access nao au anaweza ku interact nao.

Ni kama vile wewe unavyo jua kwamba wapo watu wenye teknolojia ya nuclear lakini huna access nao.

Majini wengi hasa hawa wanao interact na waganga na wachawi ni majini wanao toka katika madaraja ya chini sana miongoni mwa majini na wengi wao hawana access na baadhi ya majini walio katika madaraja ya juu.

Wapo binadamu ambao KWA sababu ya maarifa yao Wana access na majini wa madaraja ya juu ambao hawa majini wa madaraja ya chini hawana access nao.

JINSI MAJINI WA UGANGA WANAVYO SHIRIKIANA NA BINADAMU....

Hii naiweka kwenye comment. Usi comment KWANZA mpaka ni ielezee hii


Hii ni sawa na hadithi ya Abunuwas tu.

Umeshindwa hata kutoa definition ya neno "Jinn" (Genie), sasa utawezaje kumuelezea Jini?!!
 
Uzi si wangu ila nitakujibu kwa uchache sio tanzania pekee nchi nyingi zipo lkn zile zenye ukingo wa bahari au MAZIWA SPECIAL milima mikuu misitu minene na mito pamoja na MAJANGWA makubwa

mfano km ulimsoma vizuri alikwambia mfano shotcut ya VENUS ipo DAR ES SALAM
Barani AMERICA ni kama MEXICO
MEXICO kuna SHOTCUT nyingi za Kuingia HIDDEN word kuweza kuzifikia SAYARI mbalimbali
pia MAREKANI hvyo hvyo
wakati UCHINA pia kuko hvyo kuna SHOTCUT pia na maeneno mengine DUNIANII

lakini kuna SAYARI nyingine huwezi kufika kwa kutokea DUNIANI bila kwanza kufika sayari MAMA
7bu hata MAJINI wenyewe sio wote wanaoweza kuzifikia hizo SAYARI
Na hata majini wenye kuishi HUKO ufanya SAFARI ndefu kuja SAYARI nyingine lakini hawawezi kuja DIRECT duniani

na pia kuna SAYARI nyingine huwezi kufika(BINADAMU) au JINI kuja DUNIANI bila kuondokea ENEO fulani hapa DUNIAN
mfano kuna AINA ya MAJINNI wana nguvu sana wao njia ya kuu ya kufika DUNIANI na kuondoka ipo MAREKANI pekee ili kuweza kufika katika SAYARI yao na SAYARI yao ni ya kipekee na imeendelea sana

na pia sio kila JINI ana uwezo wa kufika hapa DUNIANI hapana ni wachache kwa MISSION MAALUM na KIBALI MAALUM

kusema ukweli watu wanakosa MAARIFA kwa kejeli
lkn km mngekuwa mnauliza maswali kwa kutaka kujifunza HAKIKA mngejifunza mengi sana KUHUSU hii DUNIA yenu
SIkufahamu km LIKUD angekuwa na ufahamu mkubwa hivyo ingawa kuna mengine yupo tofauti kidogo ila siwezi kushangaa
Ndio tabia za MAJINN wakikupa ELIMU yao katika maneno 10 chukua matatu yale unayoona yana mantiki hutakiwi kuwaamini sana MAJINNI watakuteka AKILI yako 7bu ya uwezo wao mkubwa wa PSYCHOLOGY kiasi kuna wengine wanafikia mpk 80 ya kusoma mawazo na ikawa hvyo

mfano niliambiwa usiniongopee unamuona huyu anajua unachowaza hvyo kila unachoongea zungumza ukweli
hapo inakuwa tayari kashaanza kuisoma MIND yako
ushawai sikia kifaa fulani kinaittwa LIE DETECTOR MACHINE basi jamaa alogundua hcho kifaa alikuwa na uwezo mkubwa mpk wakawa wanamuona chizi

WAZUNGU wanawafahamu vizuri MAJINNI na zipo Filamu nyingi sana zinawaelezea uwezo wao MAISHA yao even mpk FILAM nyingine zinakuwekea kabisa madhari ya SAYARI zao
Very true...wazungu washenzi sana aisee hivi vitu wanavijua sana aisee na vilishawekwa kwenye movie. Juzi nimegundua hilo baada ya kusoma ule uzi wa 'sasa nipo huru '.
Ngoja nianze kuzitafuta hizo movie zinazotoa ufunuo wa hiyo miji ya kijini. Kama unajua majina nitajie maana nimeziona zamani nikawaga nazipuuzia
 
First off, this is a logical non sequitur.

But to answer your question.

Among other things.

Nime patent software for simple, low cost, low energy, container based for NAS served electronic library consolidation system for offline school / document management systems.
Mkuu acha wanaotaka kujifunza wajifunze...we know some fools never learn,usiwe mmoja wao
 
Hata mimi nimeacha. Watu wajinga sana humu. Badala watulie wajifunze yale wasivyo yajua wao wanaleta ujuaji kwa kuelezea yale ambayo KILA mtu anayajua.


Ukristo unasema majini walikuwa malaika mbinguni wakamuasi Mungu wakiwa na SHETANI Mungu akawafukuza mbinguni kisha akawa rename ( kuwait's devils)

Waislamu wanasema majini waliumbwa na Mungu ili wamuabudu na kwamba wapo majini waliomuasi Mungu na wapo ambao wanamtii Mungu.


Mimi sijaja kuelezea hicho ambacho wakristo na waislamu Wana kifahamu.

Nimekuja kuelezea kile ambacho hawakifahamu.

Ila wao wanataka waendelee kufahamu vile wanafahamu.
Mkuu, fools never learn. Usiwajali,tupe madini
 
Unaweza kuwa mganga wa kienyeji ndio maana huyajui maandiko, hapa kwenye majini sikupingi.
 
We ndo maskin wa kifikra ambaye unataka kila kitu mtu aprove kwako who are you au umefanya Nini

Watu wote wenye akili duniani waliopita ukiwasoma walikua wanaprove watu wrong, Sasa wewe unataka watu wakuprove wrong huoni kama una upeo mdogo sana

Nakuongelea wewe sababu wewe kila kitu unataka evidence as if wewe umefanya makubwa sana hapa Dunia kumbe ni mbarara mmoja hivi

Unavyokomalia watu wakupe evidence wewe una evidence yeyote Ile ambayo ume-formulate kwenye world of technology and science zaid ya kucopy za wanaume wenzako
Kiranga ni miongoni mwa wajinga wasiotaka kujifunza...na watu wa hivi huwa wanauelewa mdogo sana
 
Sijaona haja kubwa ya kumchallenge mwenye uzi, kwasababu hii ni kama elimu tu kama elimu zingine kama unataka kufahamu soma kwa umakini,
Nitakushangaa wewe unaeamini mambo ya Mungu alafu haya mambo ya majini unayaponda bora Kiranga ambae haamini pande zote mbili.
Mtoa mada endelea kutupa elimu tupo sisi ambao yakiletwa mambo ya mungu tunasoma, kijini, mambo ya sayansi walete tunapenda kusoma kila kitu ambacho mtu ana utayari wa kutushirikisha tufahamu,
Mkuu LIKUD endelea kutupa madini.
Kiranga ni wale wapumbafu wasiotakaga wengine wajifunze tofauti na wanachokiamini wao. Sababu haimpunguzii kitu akikaa kimya kwa faida ya wengine,ndio maana nimediriki kumuita mpumbav
 
Back
Top Bottom