Huu mwezi mbona kama mgumu! Hivi mnatumia mbinu gani kuishi unapopita kwenye magumu na kutoka mshindi

inaitwa njaanuary , kaza tu braza yatapita , muda kama huu usiendekeze yeyote anaomba hela mpaka mambo yatulie
Ukijitoa ufahamu ukasheherekea sikukuu bila brake unaweza juta. January nimefulia kabsa lakini sidaiwi ada, sidaiwi kodi, sidaiwi chochote cha msingi yote niliyafanya kabla ya christmas. Maana kuanzia kodi, ada vyote vinalipwa january hivyo nakaa mguu pande
 
Pole…

Sisi wengine Mungu ni mwema.

Sasa hayo yote unasaidiwaje hata kama? Inabidi kuspecify nini hasa tatizo ili anayeguswa aweze kukugusa na wewe.
 
Mkuu. Nakupa hii fomla yahuu mwaka,fanya hiv kama una magumu kwenye biashara we komaa usiiache wala usiibadili ila kaa hapohapo na endelea na plani zako utatoboa
 
Tafuta michepuko mitano kwa malengo, ipo siku itakuokoa:-​
  • mama ntilie-atakusaidia chakula​
  • askari-mambo ya kisheria​
  • nesi- mambo ya hospitali​
  • hakimu-mambo ya kesi​
  • cashier- atakukopesha​
Achana na akina mwajuma ndala ndefu
 
We si unabeti correct score na unawini mara 4 kwa wiki
 
Ila Christmas watu wamekula bata sana, mpaka nikawa najiuliza hivi wanakumbuka kuna January kweli? Anyway chukua salary advance mkuu, itakuvuta vuta
 
We acha mkuu! Si wengine shule zimekomba kila kitu, nawahusia watu kuzaa watoto wachache,mmoja au wawili tu wanatosha kabisa.
 
Watu wengi huwa wanaspend December bila kuwaza January inakuwaje matokeo yake unaona kama mwezi mgumu mno.

Ila January hii ukiona umeweza kulipa kodi, watoto wakaenda shule na unakula jipige kifua mara 2 useme " nimeweza".

Na sisi kina mama tuwaombee sana wenza wetu waliofanikisha january kuwa smooth na watoto wameenda shule....baba watoto zetu Mungu awabariki mno.
 
Hamia mtaani kwangu, kuna kiwanda kinatoa maji baridi ya kunywa bure na kiwanda kingine kinatoa bure chakula cha mchana kila siku, ndizi mbivu, limau na pilipili ni juu yako.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…