Huu ndio mkataba unaomtesa Congo DR dhidi ya Rwanda na wakulimaliza hili ni Congo DR mwenyewe

Huu ndio mkataba unaomtesa Congo DR dhidi ya Rwanda na wakulimaliza hili ni Congo DR mwenyewe

Hivyo Rwanda walitegemea kupata support tena ya Angola, lakini ambacho walisahau ni kwamba maadam maslahi ya Angola yaani waasi wa UNITA walikua hawana support tena ya DRC hawakuwa na haja ya kumtoa Kabila na ndio hapa vita ikapata sura mpya kabisa iliobadili historia.

Mnamo August 22 majeshi ya Angola, Zimbabwe na Namibia yaliingia kwenye uwanja wa vita kupitia kusini mwa Kinshasa hivyo majeshi ya watutsi 800 (yaliyoongezwa nguvu na askari 2000 wa zamani wa Mobutu ) wakazingirwa katikati ya Kinshasa.

Vita ikachachamaa na Zimbabwe walitumia ndege za kivita huku Angola ikiingiza vifaru na mizinga mizito (Heavy Altirelly) huku askari wa Rwanda wakiwa na silaha nyepesi bila msaada wa ndege au vifaru. Hivyo wakawa hawana namna zaidi ya kusurrender.

Gen. James kabarebe hakuwa tayari kusurrender ingawa alikua amezingirwa katikati akiwa hana pa kutoka. Akaja na uamuzi mzito wa kuvamia Angola kwa nyuma ili wapate nafasi ya kupumua na kurudi kwao kishujaa kuliko kupata aibu ya kushindwa vita.

Mnamo mwezi september 1998, Makomandoo wa kitutsi (Rwanda, UG na Burundi) walivamia Eneo la Zombo de maquela huko Angola ambapo walisambaratisha majeshi ya Angola ya eneo hilo na kuteka uwanja wa ndege wa jeshi.

Walipodhani wamepata mwanya wa kutorokea, changamoto ilioonekana ni kwamba uwanja ulikua mdogo sana kwa ndege kubwa kutua hivyo alihitaji walau wiki 3 wapanue uwanja ndio askari watoroshwe.
Hapa pamenichanganya
Wakiwa Angola walipanua uwanja wa ndege na kufanikiwa kuondoka
Je wakati huo Congo kulikuwa na majeshi gani
 
Nimejifunza
  1. Usaliti hauwezi kumuacha mtu salama
  2. Tamaa mbele mauti yaja
  3. Hakuna rafiki wala adui wa kudumu
  4. Ukubwa wa pua siyo wingi wa kamasi
  5. Mwenzio akinyolewa weewe tia maji
 
Mobutu hakuwa na mpango wa kuwafukuza Banyamulenge.
Historia inaonyesha kwamba wale askari wa Kampeni za Kigeni za madini ndio waliofanya shooting iliyowafanya Banyamulenge wakasirike na waelekee Kinshasa.
Mobutu aliyafukuza makampuni ya kigeni.
Yale makampuni ya uchimbaji madini yakaondoka ,yakamnyima Mobutu ramani za kuchimbi madini.
Ndio wakaenda kufanya mpango wa kumuondoa Mobutu.
Mobutu sliondolews madarakani na State Department.
Kagame na Museveni walichaguliwa na State Department kumuondoa Mobutu.
Mercenary Kabila alipendekezwa na State Department kumuondoa Mobutu.
Na walikuwa wanafanya consultation na Nyerere,siyo baada ya kuchukua madaraka isipokuwa very soon after the march to Kinshasa began.
Again wazo la kumshirikisha Nyerere kama mshauri lilikuwa wazo la State Department.
Lakini Nyerere hakuambiwa na hakufahamu at any time kwamba anafanya kazi ya State Department.
State Department ni Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani.
Yaani Kampeni hizi zinavyokuja kuchimbi madini inaratibiwa na State Department.
Sasa umewasikia wale waasi jana walivyokuwa wanasema Goma.
Katika Press Conference wamesema wanataka kuiteka Kinshasa.
Na Tshisekedi anasema watu waliofanya mikataba mingi ya ajabu hapo zamani. Lakini sasa tunayakiwa kupigana tu. Hiyo mikataba ilikuwa ya makosa. Makosa yalifanyika. Lakini sasa tupigane. What else can we do?
 
Write your reply...Kuna mengi ya kutafakari pale wawili wanapogombana.
 
Back
Top Bottom