Huu ndio Mtihani kwa ACT-Wazalendo: Kukubali maridhiano na kuunda Serikali

Huu ndio Mtihani kwa ACT-Wazalendo: Kukubali maridhiano na kuunda Serikali

Dawa ya kudumu ACT watafute namna wawe na jeshi lao la polisi na vikosi vingine, ukifika muda wa kupiga kura wawahimize watu wao wakapige kura kwa wingi, wakiibiwa haki yao, ndio hivyo vikosi vyao vitoke vikapambane na hao wajuaji waliozoea kuua raia wasio na hatia kila wakati wanapodai haki zao.

Maridhiano ni ujinga mtupu, kila siku CCM wataunda serikali hata kama hawakushinda kihalali, na hao ACT wataendelea kupewa nafasi za chini, kwani CCM wana hati miliki ya kuitawala Zanzibar? kama wanayo basi wafute mfumo wa vyama vingi kote Bara na Zanzibar wabaki peke yao.
 
ACT watasusa, uchaguzi utarudiwa kwa yale majimbo manne na CCM inaweza kuwaachia CUF hivyo viti vinne hivi ili waunde GNU na maisha yaendelee.

Mwaka 2025 ACT wataingia tena kwenye uchaguzi na most likely wataibiwa tena.

Vicious circle will continue
 
Ni heri kufa ukiwa na msimamo wako kuliko kujipendekeza kwa hao wanaojiona wana hati miliki na hii nchi,kila nafc itaonja umauti hata hao mnaowaabudia ipo cku watakufa tu na huo ni mwisho wa ngebe na jeuri zote cjui mimi cjarbw ataenda kulisemea hlo mbele ya Allah
Hoja nzuri sana hii.
Uchaguzi wa 2015, Maalim Seif akiwa CUF, walifanya ujinga kususia uchaguzi ule wa marudio, na matokeo ya uchaguzi huu ni kufidia makosa, sasa Maalim kupitia ACT, ameadhibiwa. Hata hivyo, kufanya kosa, si kosa, kosa ni kurudia kosa, Maalim Seif alifanya Kosa ile 2015, sasa 2020, asilirudie kosa!.
P
 
Ni heri kufa ukiwa na msimamo wako kuliko kujipendekeza kwa hao wanaojiona wana hati miliki na hii nchi,kila nafc itaonja umauti hata hao mnaowaabudia ipo cku watakufa tu na huo ni mwisho wa ngebe na jeuri zote cjui mimi cjarbw ataenda kulisemea hlo mbele ya Allah
Hoja nzuri sana hii.
Uchaguzi wa 2015, Maalim Seif akiwa CUF, walifanya ujinga kususia uchaguzi ule wa marudio, na matokeo ya uchaguzi huu ni kufidia makosa, sasa Maalim kupitia ACT, ameadhibiwa. Hata hivyo, kufanya kosa, si kosa, kosa ni kurudia kosa, Maalim Seif alifanya Kosa ile 2015, sasa 2020, asilirudie kosa!.
P
 
Mimi ningemshauri Maalim, kama atakubali kuingia kwenye serikali basi awe na demands ambazo huyi rais wa kulazimishwa azikubali. Kwanza kikosi cha mazombi kifutwe, pili wawajibishwe wote waliohusika katika kuruhusu silaha za moto kutumika na wauwaji wa raia wachukuliwe hatua, uchaguzi ngazi ya wawakilishi na wabunge urudiwe. Vyenginevyo awaachie sirikali yao tu waendeshe watakavyo wenyewe, tofauti iliopo Zanzibar ni kubwa na muhimu kuliko Zanzibar yenyewe saiv. Maalim akikubali ivi ivi bila demands basi ajue ameua upinzani 2025, na asitegemee kama kutakuwa na muamko wa watu mana hakuna jipya atakalowaambia wananchi wakatambua kuwa ni maneno tu.
Nakuunga mkono labisa ndugu yangu[emoji1548]
 
Na kwa mujibu wa Katibu, wanapaswa kuwa na majibu ndani ya siku saba kutoka siku ambayo Dk Mwinyi ataapishwa.
ACT watafanya makosa makubwa kumpendekeza Maalimu Seif kwa nafasi hiyo!
 
Maalim asikubali kuingia kwenye huo uchafuzi maana ni kama vyombo vya dola vimepoka uhuru wa wananchi kwanini ashiriki kwenye serikali ya hivo. Atakuwa anahalalisha wizi wa kura uliofanyika. Hivi ACT ya kukosa kura za wawakilishi Pemba ambako tangu kuanza kwa vyama vingi hawajawahi kushinda
 
Maafisa Vipenyo waliopo ACT na Chadema wanaripoti kuwa ACT itasusia serikali ya umoja wa kitaifa kwa kuwa hata ikiundwa Vingunge wote mbali ya Seif hawatoingia kwny Cabinet kwa kuwa sio Wawakilishi na pia Katiba haimlazimishi Rais Mwinyi kuteua Wajumbe wa baraza kutoka upande wa pili hivyo automayically kina Bimani, Jussa, Mazrui watakuwa nje ya viti vya Uteuzi

Upande wa Bara Chadema wamepanga kususia Bunge kwa kuwa Viongozi wakuu wote na Wajumbe wa Kamati kuu ya Chadema wamepoteza majimbo yao hivyo hata wakiruhusu wabunge wa viti maalum waende pamoja na wa kule Rukwa bado kwao binafsi hawatapata manufaa japo wanabishana kuwa kama watasusia ikitokea Serikal ikawanyima Ruzuku ambayo kwa sasa haitopungua 70 million kwa mwezi hali itakuwaje na huku hawana Ubunge?

Binafsi Halima Mdee anataka wasisusie kwa kuwa ana uhakika wa kupata Ubunge wa viti maalum hivyo atakuwa anatumikia kipindi cha nne mfululizo na kuwa Mbunge aliedumu bungeni muda mrefu zaid
ACT watafanya kosa kubwa kama watasusia Serikali ya Umoja wa Kitaifa. Wao waombe kwa kuwa wana viti vichache basi Mwinyi ateue japo wabunge wanne au watano kutoka ACT ili wakina Jussa waweze kuingia serikalini.

Pi huku bara kama CHADEMA watamkataza mbunge wao wa Nkasi na pia wale wa viti maalum ambao wanaweza kufika hata kumi basi watakuwa wamejiua zaidi. Mimi nawashauri wale wabunge wa viti maalum watakaoteuliwa na yule wa Nkasi waende bungeni hata kama chama chao kitapinga, ikiwezekana bunge litunge sheria kuwalinda na ubunge wao dhidi ya ubabe wa viongozi wao.

Katika siasa inatakiwa utumie kila fursa unayoweza kuipata. Kule Israel, waarabu ambao wamekubalika kama raia wa Israel hugombania ubunge ma umoja wao unajulikana kama joint list bungeni, sio kwamba wanaikubali serikali ya Israel la hasha ila wanapigana toka ndani na ni chama cha tatu kwa ukubwa bungeni. Isingekuwa ni kuona aibu baadhi ya vyama vya waisrael vingewatumia kuiangusha serikali ila vinaogopa kuonekana vinashirikiana na adui.

Mfano mwingine, kule Kongo enzi hizo ikiitwa Zaire ya Mobutu, mahakama iliwahi kumhukumu mwanasiasa maarufu wa upinzani aliyeitwa Nguza Karl Bond adhabu ya kifo lakini baadae Mobutu alilazimika kumteua huyo huyo Nguza kuwa waziri mkuu wakati ule wa vuguvugu la upinzani wa vyama vingi linaanza na Nguza alikubali uteuzi huo akatolewa jela akawa waziri mkuu.

Hao wabunge japo wachache wanaweza kung'ara bungeni kwa hoja nzito kuliko chadema ilipokuwa na wabunge wengi. Hata hoja yao ya tume huru wanaweza kuipigania toka bungeni huku wemgine wakipigania huku nje.

Alternatively, kama Chadema wanasusia bunge basi wasusie na ruzuku wasichukue ili wasimamie kweli maneno yao.

Jambo moja wapinzani waelewe hakuna uchaguzi mwingine utakaofanyika hadi mwaka 2025 na jumuiya ya kumataifa haiwezi kushinikiza wala kufanikiwa kuilazimisha nchi huru nyingine kufanya uchaguzi. Pili Marekani sasa hivi sio dominant power duniani kuna China na Urusi ambazo zinaipinga Marekani katika medani mballi mbali za kimataifa.

Maridhiano ndio kitu pekee kitakachowawezasha wapinzani walau kuwa sehemu ya uendeshaji nchi lakini siasa za uanaharakati tena wa chuki dhidi ya serikali zitawaumiza wao zaidi. Hakuna mtu atakayeingia barabarani aache kwenda kutafuta riziki na pia ajiletee matatizo. Wakumbuke kuwa sisi wengine wapenda amani tunategemea tutumie barabara hizo hizo kupita kwenda kwenye shugjuli zetu hatuwezi kukubali tufe njaa kwa sababu barabara zinatumiwa kwa maandamano.

Duniani hapa hakuna mtu yeyote hata kama alikuwa rais mwanzoni anayeweza kupambama na serikali.
 
Hoja nzuri sana hii.
Uchaguzi wa 2015, Maalim Seif akiwa CUF, walifanya ujinga kususia uchaguzi ule wa marudio, na matokeo ya uchaguzi huu ni kufidia makosa, sasa Maalim kupitia ACT, ameadhibiwa. Hata hivyo, kufanya kosa, si kosa, kosa ni kurudia kosa, Maalim Seif alifanya Kosa ile 2015, sasa 2020, asilirudie kosa!.
P
Wacha ujinga wako cuf haikufanya ujinga ujinga akifanya mjinga mwenzenu JECHA kufuta uchaguz pasina matajwa ya KIKATIBA
#SUBIR UTEUZI
 
Mkuu hapa umeandika point ambayo hawa viongozi wa upinzani wakikosea kwa lengo la kutaka manufaa yao wao kama wao wajue wananchi wana angalia mchezo na the day has come wasije sema watanzania wanafiki.
Unafiki mtupu!Awaachie serikali yao.

Baada ya kutimiza walichotaka, ndio sasa wanajidai kutaka maridhiano wakati kuna madai kuwa watu wamepoteza Maisha kutokana na vurugu za uchaguzi.

Ni hivi, kinachafutwa sasa ni kushirikisha wapinzani ili kuihadaa dunia lengo likiwa ni kuwapoza wahisani ili waendelee kutoa mikopo na misaada..

Hata huku Bara, Mbowe,Lissu na Zitto, wanaaweza kualikwa Magogoni lengo likiwa ni kuonyesha wafadhili kuwa kuna maridhiano ili waendelee kutoa fedha.

Hivyo,msishangae hao niliowataja na wapinzani wengine wakaanza kushawishiwa kwa kupewa ubunge wa kuteuliwa ingawa naamini kamwe hawawezi kukubali.
 
Na ujue kaamua kustaafu siasa kwa aibu. Kwasabb kwa vyovyote vile Maalim hawezi kugombea tena urais kutokana na umri kumtupa mkono. Aweke masharti yenye maslahi kwa chama chake na nchi kwa ujumla yakikubaliwa akubali kuwa makamu wa kwanza.
Maalim hato staafu kwa aibu, na wala hajapata aibu na wala hawajawahi kupata aibu kisiasa. Hata akistaafu, Wazanzibari watamtambua kuwa Maalim ni shujaa wao aliepambana mwanzo mwisho. CCM wanajua kuwa Maalim ni mwiba kwao ambae anawakosesha raha. Tizama Jeshi walilolileta Zanzibar kwa jinsi wanavyomuogopa. Wamethubutu kumteka Mazrui, kumpiga Jussa ambao wote wanapendwa na wazanzibari lakini Maalim kikofi hawakumpiga kwa sababu wanajua tifu ambalo lingetokea. Yaani in short, huenda Maalim hakupata urais na kutetea Uzanzibari lakini Maalim vita ameshinda tayari, haitotokea CCM Zanzibar kukubalika, ninaamini kura zao za tarehe 27 tu ziliwaonesha picha halisi jinsi hata huko vikosini hawakubaliki.
 
Hoja nzuri sana hii.
Uchaguzi wa 2015, Maalim Seif akiwa CUF, walifanya ujinga kususia uchaguzi ule wa marudio, na matokeo ya uchaguzi huu ni kufidia makosa, sasa Maalim kupitia ACT, ameadhibiwa. Hata hivyo, kufanya kosa, si kosa, kosa ni kurudia kosa, Maalim Seif alifanya Kosa ile 2015, sasa 2020, asilirudie kosa!.
P
P
Unaweza kunisaidia aina ya ujinga waliofanya CUF!?
 
Ni cheo ambacho CCM wamekiweka kuwafubaza wapinzani. Bora akikatae ataheshimika.
Na hichi cheo walichokusudia kuwafubaza Wapinzani, kiliwatoa mikojo 2015 mpaka wakaamua kurudia uchaguzi.
 
Kufikiria kwa tumbo ni kushiriki uchaguzi wa Wabunge na Madiwani wakati uchaguzi wa serikali za Mitaa mlisusia na hakuna hoja yenu hata moja ambayo ilifanyiwa kazi hadi kuamua kushiriki, Mbowe na Zitto wangejua wangekosa Ubunge basi wangesusia Uchaguzi
Muda wote unafikiria kwa kutumia tumbo tu, au ubongo wako upo tumboni?!
 
Yaani mawazo haya yanaonyesha jinsi Watanzania wengi mnavyoishi kwa manufaa binafsi. Na ndio nyie mngekuwa ma IGP, NEC, Msajili wa Vyama... mngeua Watanzania wenzenu na kuiba chaguzi ili tu kulinda nafasi zenu. Wewe ndiye ungekuwa ni Maalim, tayari ungewatosa watu wako kwa sababu ya cheo!
Kumbuka hata mwaka 2001 baada ya Maalim kuwatumbukiza wapemba 21 wakauliwa na wengine wakawa vilema ( mmoja wao nakumbuka aliitwa Chuki athumani) na wakatelekezwa bila msaada bado aliingia katika maridhiano na kuwa sehemu ya serikali. Uwe unarejea historia.
 
Hoja nzuri sana hii.
Uchaguzi wa 2015, Maalim Seif akiwa CUF, walifanya ujinga kususia uchaguzi ule wa marudio, na matokeo ya uchaguzi huu ni kufidia makosa, sasa Maalim kupitia ACT, ameadhibiwa. Hata hivyo, kufanya kosa, si kosa, kosa ni kurudia kosa, Maalim Seif alifanya Kosa ile 2015, sasa 2020, asilirudie kosa!.
P

Ndugu Mayalla, Maalim Seif akirudia kosa alilolifanya 2015 kwa sababu tu ya kukosa Urais, dunia haitamuelewa, asipokubali kuchukua nafasi yake hiyo ya Makamu wa kwanza wa Rais ni dhahiri kuwa hatakii mema Zanzibar, ni mbinafsi na aendelee kungoja mpaka 2025 ajaribu bahati yake tena which could be too late. Ni vema aingie jikoni apambane akiwa ndani ya serikali. Hii itawezesha viongozi wengine ndani ya chama chake kuwa ndani ya mfumo rasmi kwa teuzi tofauti tofauti ndani ya serikali. Yaliyopita ni ndwele wagange yajayo!
 
Kumbuka hata mwaka 2001 baada ya Maalim kuwatumbukiza wapemba 21 wakauliwa na wengine wakawa vilema ( mmoja wao nakumbuka aliitwa Chuki athumani) na wakatelekezwa bila msaada bado aliingia katika maridhiano na kuwa sehemu ya serikali. Uwe unarejea historia.
Hilo kosa la kukubali maridhiano na kukalia ofisi zenye damu za watu waliouwawa kutokana na uchaguzi, ndiko kunafanya CCM iendelee kuwageuza kama chapata kila kipindi cha uchaguzi kikifika. Ni bora sasa kuacha hayo "maridhiano" feki ili CCM ijue hakuna wa kumlaghai kwa kumuonjesha kipande cha keki baada ya kumuibia. Wachukue madaraka yote, wawaongoze wazanzibar waliowapigia kura na kupata ushindi wa "kishindo" 75%
 
Back
Top Bottom