Huu ndio uzi mpya wa Stars,sasa ni full ushindi!!!

Naona Adidas wametubwaga, Kuna brand kibao kama puma, new Balance, n.k, wote wakatae kudhamini?

Mkuu, hao wanakuja timu ikiwa na mafanikio. Hawafanyi udhamini bora udhamini tu. CHAN tupo hoi, Mataifa ya Afrika hoi bin taabani, kombe la dunia ndio usiseme. Sasa huo udhamini utawapa faida gani?
 
Hiyo rangi nyeupe msingi wake au insipration yake ni nini?

Kuna mataifa wanatumia rangi za bendera ya taifa husika. Wengine hutafuta rangi zenye maana fulani kwa nchi zao hata kama hazipo kwenye bendera. Sisi msingi wetu ni nini?
 
Hata mimi sielewi. Sijui ndio mambo ya Simba na Yanga kwenye timu ya taifa? TFF imejaa watu wa mizaha sana

Iam sorry to say,'' Jezi hazivutii, na wala hazichezi na watazianzia kwa waarabu wakipigwa bao 5-1. Mimi ni mtanzania lakini kwa stars hii. YATOSHA!

Hiyo rangi nyeupe imetokea wapi?

Watumie rangi za bendera. Ndio alama ya taifa hiyo

Wameamua kuwafurahisha Simba, majanga matupu!

Ikumbukwe Malinzi ni shabiki wa timu ya wananchi au wazee wa kimataifa tangu kitambo, sasa inakuaje amfurahishe mnyama?

Kiukweli JEZI za Taifa zinatakiwa ziwe na color ya bendera ya TAIFA.
TUSIPOTOSHE UKWELI.
MATAIFA YOTE NATIONAL TEAM IS A symbol of NATION,period.

Bora hata bukta zingekuwa nyeusi

uzi unatakiwa kuwa na rangi ya taifa tu, nyeupe ya nini??

Mkuu Jamali Malinzi come this way please.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu, hao wanakuja timu ikiwa na mafanikio. Hawafanyi udhamini bora udhamini tu. CHAN tupo hoi, Mataifa ya Afrika hoi bin taabani, kombe la dunia ndio usiseme. Sasa huo udhamini utawapa faida gani?

Kweli mkuu, wangempa ata Shweria Ngowi basi abuni na atangaze brand yake
 
Kwa mwendo huu safari tunayo. Hivi ni viashiria tosha vya kutokua makini. Sijui hata kama walizitathmini jezi zilizopita ndio wakaja na hizi!! Hivi ni kweli wametumia wataalam au ni watu wa hapo TIFUTIFU ndio wametupiga changa. Jezi za kindorrooobo kabisa!!
 
Heri washonewe vitenge maana kwenye mpira hawana faida,sometimes ikifikaga swala la timu la taifa mpaka natamani kukana utanzania
 
Hiv malinzi ana akili kweli huyu?
 
Heri washonewe vitenge maana kwenye mpira hawana faida,sometimes ikifikaga swala la timu la taifa mpaka natamani kukana utanzania

Hahahahahaaaa...kweli jf kiboko
 
Blatter alijiuzulu kutokana na pressure ya nchi za ulaya zenye nguvu kisoka. Siku Yanga, Simba au hata azam wakila njama na kususia ligi kuu huo ndio utakuwa mwisho wa uongozi wa TFF. Kumbukeni nchi za ulaya zilitishia kususia kombe la dunia. Nafahamu wako watakaosema Yanga na Simba hawawezi kufanya hivyo. Lakini wakumbuke hata Blatter alikuwa na mawazo kama hayo. Corruption iliyosambaa katika soka ya Tanzania ni mbaya na imesambaa kuliko hata corruption ya polisi wa usalama barabarani na TRA.
 
Hahahahahaaaa...kweli jf kiboko

Sasa hivi Tanzania inasifika kwa Kilimanjaro,mbuga za wanyama na ukikutana na watu wengine wa africa watakuambia Tanzania -Lagos ujue wanamzungumzia diamond platnumz,huko kwingine ufala
 
Hiyo rangi nyeupe msingi wake au insipration yake ni nini?

Kuna mataifa wanatumia rangi za bendera ya taifa husika. Wengine hutafuta rangi zenye maana fulani kwa nchi zao hata kama hazipo kwenye bendera. Sisi msingi wetu ni nini?

Msingi wa rangi nyeupe ni kuwafurahisha mikia full stop!
 
Mkuu, hao wanakuja timu ikiwa na mafanikio. Hawafanyi udhamini bora udhamini tu. CHAN tupo hoi, Mataifa ya Afrika hoi bin taabani, kombe la dunia ndio usiseme. Sasa huo udhamini utawapa faida gani?

Lakini Kama tunawalipa keshi haiwezekani?..
 
safi sana timu lenyewe pasua kichwa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…