Huu ni mpira wa kishamba sana

Ujinga sana, badala ya kufikiria kupambana na TP Mazembe, Al ahly, Zamalek, wanaishia kulumbana tu, timu zimejaa ujinga ujinga tu
Hivi vilabu vikongwe vina uswahili mno nadhani tatizo ni viongozi wakuu wa hivi vilabu.
 
Mkuu kama Senzo kajiuzulu, kuna ubaya gani Yanga kumwajiri wakiamini atawasaidia? Simba wanazingua, wanafanya ujinga na kwa kuwa wamejazana tff wameshindwa hata kuamua kesi ya mkataba wa Morrison. We unadhani kuna utata gani kwenye suala la Morrison? Simba wamejitangaza wao ni miamba, wanaweza kufanya lolote watakalo. Yanga hatutakubali kuburuzwa na mtoto wetu wenyeww
 
Luc hakukosea kusema mashabiki wa Utopolo wanaropoka ka manyani.
Mwenyekiti wa Kamati ni Yanga lia lia afu ameshindwa kuamua kesi bado unawalaumu TFF.
Hivi kama Yanga wangekua na documents sahihi za mkataba na Morison kulikua na haja gani ya kuchelewa kuamua wakati documents zinajionesha. Kwa hali inavyoonesha ni kwamba mkataba wa Morrison na Yanga ulikua wa magumashi ndo maana inakua shida kuamua ipi ni nyeupe na ipi ni nyeusi.
Saizi tunaambiwa eti kuna baadhi ya nyaraka zinatakiwa ziletwe kesho ili uamuzi utoke.
 
Mkuu haina haja ya kuhangaika kesho itafika mbona.
Siku zote njia ya muongo ni fupi.
 
 
Hans Pope,Manara na Magori ni kirusi cha Soka la Bongo,na pia sioni usomi na credibility ya MO katika hili amekubali kuendeshwa kama gari bovu na hao Waswahili.
Ko hao tu ndo wanaoharibu Mpira mzima wa bongo?
Miaka yote hao walikuwepo?
Mbona soka halikuendelea?
System nzima ina matatizo na sio watu watatu kama ulivyoandika.
Na hii haiwezi futika labda hizi timu mbili zife kabisa.
 
nikweli kabisa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…