Zanzibar 2020 Huu sasa ni ufalme; haiwezekani watoto na familia ya Mwinyi iteuliwe kugombea kuanzia Urais hadi Ubunge

Zanzibar 2020 Huu sasa ni ufalme; haiwezekani watoto na familia ya Mwinyi iteuliwe kugombea kuanzia Urais hadi Ubunge

#Ufalme au?

Hussein Ali Hassan Mwinyi ~ Mgombea URais Zanzibar

Abbas Ali Hassan Mwinyi-
Ubunge ~ Fuoni

Abdalla Ali Hassan Mwinyi -
Mbunge ~ Mahonda

Zubeida Shaibu (Mkewe Abbas Ali Hussein Mwinyi)
Mbunge ~ Mfenesini
kiongozi hawa watu wamekulia na kukua kwenye siasa ulitaka iwe vipi
patrik kluivert alikua mchezaji sasa hivi ni kocha sijui wapi uko mtoto wake nae kawa ivo ivo mchezaji kwahiyo hayo mambo hata kwenye siasa pia yapo
 
Ni kweli wangezitafuta kwenye biashara zao.. sio cake ya taifa. Maana wameshakula hiyo cake na wanaendelea kula.. wangewaachia wengine wale pia.. wao wangetafuta nje ya hela za uma. Kama mengi ama bakhressa.. jaribu kuwaza kura za maoni waliogombea na mama salma kikwete kama hata majina yao yamesomwa na kamati kuu
kiongozi keki ya taifa kweli wanaila ila bado hawajashiba
 
Usijali wanayo haki kugombea, sio lazima muwapigie kura.

Nitashangaa Abbas Mwinyi akiwa mbunge.

Hizo kura za majeshi , polisi na wazee wa Tume wakala wake ni nani ??? kama si Abbas mwenyewe
 
#Ufalme au?

Hussein Ali Hassan Mwinyi ~ Mgombea URais Zanzibar

Abbas Ali Hassan Mwinyi-
Ubunge ~ Fuoni

Abdalla Ali Hassan Mwinyi -
Mbunge ~ Mahonda

Zubeida Shaibu (Mkewe Abbas Ali Hussein Mwinyi)
Mbunge ~ Mfenesini
Kwani vigezo si elimu ya darasa la saba, kadi ya chama na sh.laki 1 au huko kwenu form ilikuwa million 50?
 
Hili la Salma Kikwete ni dhahiri mumewe hana power nyumbani kwao juu ya maamuzi ya Huyu mama!

It is beyond belief that she could decide to go and contest a parliamentary seat instead of taking care of an ailing retired politician!! Kama ukwasi Vasco Dagama amejilimbikizia wa kutosha!
kiongozi kwani umeambiwa mama salma hamtunzi mzee na sidhani kama ni suala la ukwasi
mbona hillary clinton alikua anawania urais USA na ana ukwasi wa kutosha mi nahisi watu wamezoea siasa na bado wangependa kuwa ktk uongozi
 
So sad inasikitisha
Watoto wao, wake zao, familia zao, wao siyo wa kujiajiri ni wa kuhudumiwa na serikali...inasikitisha sana!

Salma Kikwete ndiyo kanichosha zaidi! Ameshindwa kabisa kuwaachia wengine wale cake ya taifa??

Everyday is Saturday........................... 😎 I
 
kiongozi kwani umeambiwa mama salma hamtunzi mzee na sidhani kama ni suala la ukwasi
mbona hillary clinton alikua anawania urais USA na ana ukwasi wa kutosha mi nahisi watu wamezoea siasa na bado wangependa kuwa ktk uongozi
Unamfananisha Hliiary na Salma?
 
FRED lowassa
Salma Kikwete
Ridhiwani Kikwete
.....
.....
CCM INA WENYEWE. WENYEWE NDIO HAO. sisi kazi yetu ni kusema MITANO ZAIDI[emoji1787][emoji1787][emoji1787] ili waendelee kula mema ya nchi
Mbona hapo umemuacha aliyepitishwa juzi Khalfan Kikwete?
 
Saana tu
Uk kulikua na David milliband na Eddie Milliband,mmoja waziri wa Mambo ya nje,mwingine kiongozi wa wabunge
Us kulikua na Jeb na George Bush,bill na Hillary Clinton ndio demokrasia ukiona unapata kiungulia usiwape kura tu utapona fasta
Unatafuta mfano wa UK wakati unajua upuuzi wa nchi zertu hizi? Nawe utakuwa mpuuzi mwingine. UK Waziri anajiuzuru kwa kuendesha gari vibaya. Hapa kwetu waziri haguswi, mkewe, watoto, wakwe, nk. wote hawaguswi kwa sababu tu kuna waziri wanaweza pigiana simu.

Unapoingiza ukoo mzima ktk siasa ina maana ni kama kijiji chenu chote kimekuwa untouchable. Bado tuko hovyo na tunaishia kupata marais hovyo, na upinzani unageuka kuwa hovyo!
 
#Ufalme au?

Hussein Ali Hassan Mwinyi ~ Mgombea URais Zanzibar

Abbas Ali Hassan Mwinyi-
Ubunge ~ Fuoni

Abdalla Ali Hassan Mwinyi -
Mbunge ~ Mahonda

Zubeida Shaibu (Mkewe Abbas Ali Hussein Mwinyi)
Mbunge ~ Mfenesini
Kwanini Mzee Mwinyi asiseme Magufuri aongeze muda kwa manufaa ya familia yake.
 
Unapoingiza ukoo mzima ktk siasa ina maana ni kama kijiji chenu chote kimekuwa untouchable. Bado tuko hovyo na tunaishia kupata marais hovyo, na upinzani unageuka kuwa hovyo!
Unaonekana una stress ,hapa najaribu kupangua hoja ya usultani kwa mifano,kwa hiyo usultani uk ni halali kisa tu waziri akiendesha baiskeli anajiuzulu?
 
Kila mtu ana haki kikatiba, ila mama Kikwete na Mwinyi walichofanya sio sahihi. Mama salma kikwete angeachia hata ukoo mwingine nao ule national cake ya ubunge huko kwao kusini, maana yeye na mumewe wana asilimia 70 ya mshahara wa urais mpaka kufa kwao.
Kutoka kwenye u' first lady mpaka ubunge..[emoji44][emoji44]....!!!!....Kuna haja hapa ya marekebisho ya Sheria,iende sambamba na muongozo unaomtaka rais mstahafu kutogombea Tena nafasi yoyote ya kisiasa..
 
Ata ningekua Mimi lazima wanangu wawe juu na sio losers with alot of fu##ng excuses.......ETI OOH HAKI SAWA. ..!?? hakuna usawa tangu dunia kuumbwa....ata Mimi kwenye dili za kazi nawapa ndugu na rafiki zangu... full stop
 
FRED lowassa
Salma Kikwete
Ridhiwani Kikwete
.....
.....
CCM INA WENYEWE. WENYEWE NDIO HAO. sisi kazi yetu ni kusema MITANO ZAIDI[emoji1787][emoji1787][emoji1787] ili waendelee kula mema ya nchi
Wakina johnthebaptist hao kazi yao kushangilia.[emoji382][emoji382][emoji382]
 
Kila mtu ana haki kikatiba, ila mama Kikwete na Mwinyi walichofanya sio sahihi. Mama salma kikwete angeachia hata ukoo mwingine nao ule national cake ya ubunge huko kwao kusini, maana yeye na mumewe wana asilimia 70 ya mshahara wa urais mpaka kufa kwao.
Ukisikia tamaa na ubinafsi ndio hivi.Nyerere angekua hai angekemea hivi vitendo hawa wasasa wote matumbo mbele hakuna wa kumnyooshea mwenzie kidole dawa ni wananchi kuwakataa tu.
 
Back
Top Bottom