Huu sio uungwana, Makomandoo wa Yanga wamshushia kichapo kikali shabiki wa Yanga

Huu sio uungwana, Makomandoo wa Yanga wamshushia kichapo kikali shabiki wa Yanga

pesakilakitu

JF-Expert Member
Joined
Aug 17, 2024
Posts
1,618
Reaction score
2,861
Jamani Tanzania ni nchi ya amani, na pia katika upande wa michezo tunaamini katika fair play na uhuru wa kutoa maoni bila kufanyiwa ukatili.

Kuna video inasambaa kwa kasi kubwa mitandaoni ikimuonesha shabiki wa Yanga akijaribu kutoa maoni yake na kuwafariji mashabiki kua ni hali ya mchezo wa mpira wa miguu ukifungwa unakubali unajipanga.

Lakini katika hali usiyo ya kawaida walitokea wanaosemekana ni MAKOMANDOO wa Yanga na kuanza kumpiga shabiki huyo makofi na ngumi na mateke, na kijana wa watu japo alikua anakimbia kujihami lakini bado walikua wanamkimbiza huku wakiendelea kumshambulia.

Jambo hili ni baya sana na linachafua mpira wa miguu. Uongozi wa yanga ukishirikiana na mamlaka za kisalama pamoja na Bodi ya Ligi ziwachukulie hatua kali sana WAHUNI hao wanaojiita makomandoo wa yanga.
 
Nimeona hizo clips, wazo la ghafla likanijia.

Nikasema kama Yanga wana mabondia wa aina hii kwanini wanatumia njia ndefu kutafuta kombe??

Kwanini wasiwatume hawa vibopa wakalichukue kimabavu tu kuliko kuwachosha kina Mpumelelo wawatu?

Kwasababu mimi nahakika kabisa kwa nilichokiona kwa wale majamaa watatu wakiliamsha pale CAF ni zaidi ya Expendable. Lazima kombe waachie.
 
Dah, ndo mana Nembo ya Utopolo Ina picha ya Mabondia , nilikuwa sielewi wale Mabondia wamefata Nini Kwenye klabu ya Soka....!

Kumbeeeee Yanga Ina mabaunsa Siku Yanga ikifungwa hata ukicheka Mabaunsa wanakuwa Wanandondi!!
Kibano kitakuhusu.

Pole sana Shabiki aliyepigwa.!
 
Back
Top Bottom