Huu umilikishwaji wa vitega uchumi muhimu vya nchi kwa waarabu, ni uwekezaji au uvunaji?

Unamaanisha TRA inatupiwa sana jicho na TISS hivyo uzembe na wizi hakuna? Au upo kidogo kulinganisha na bandari?

Umesema watanzania ni wazembe hawana ufanisi na wezi, hizo clearing agents zikiwa private watu wa TRA wa kwenda kukagua, kukadiria na kuchukua kodi watakua wa kutoka nchi gani?
 
Muongezee huyo Lokopromo kuwa hiyo Bandari ya Bagamoyo ilikuwa kwanza inalenga kuleta Generation 4 ships ambazo kwa sasa zina dock Durban peke yake katika eneo hili. Pia Bandari ya Bagamoyo ilikuwa na package ya Industrial estate ambayo ingezalisha bidhaa zote zile Watanzania wanafuata Guangzhou
 
Mwambie pia Bams kuwa TBL by 90% ni mali binafsi with InBev majority shares. Je kuna mapungufu gani kwenye uwapo wa bia au kutengeneza ajira, kukusanya kodi na Serikali kupata gawio?
 
Hata yale ambayo hayajukufanya vizuri at least yalitoka mikononi mwa Serikali na yakapunguza mzigo wa Serikali kutoa subsidy kila mwaka kwa ajili ya kuyaendesha. Mashirika kama NMC, RTC, NBC etc
Lengo la kubinafsishwa ilikua kupunguza mzigo kwa serikali au kuleta tija na faida kwenye uchumi wa nchi? Kama yalishindwa kukua na kuleta faida kwenye uchumi ipi ilikua faida ya kuyabinafsisha?

Maswali yangu kwako yalikuja kutokana na like ulichokua umeandika na kuonyesha ubinafsishaji ulifanikiwa ukatolea mfano TBL, bila kujua mashirika mengi yalikufa kabisa
 
Mwambie pia Bams kuwa TBL by 90% ni mali binafsi with InBev majority shares. Je kuna mapungufu gani kwenye uwapo wa bia au kutengeneza ajira, kukusanya kodi na Serikali kupata gawio
 
Hapa tunazungumza vitu ambavyo tunahisi vingetokea, hatujui kama ingekua hivyo au osingekua hivyo. Story za uwekezaji huwa nzuri mwanzoni
Swali nililokuuliza huyo ni kipi kimefanya mama samia asiendelee na mazungumzo ikiwa alifufua mazungumzo na huyo mwekezaji na serikali ikakaa nae mezani lakini wakshindwana. Je ni mama samia aliona ni story tu kama hizi zako bila uthibitisho wa kwenye mkataba au kulikua na nn?
 
Serikali za uchumi wa soko hazifanyi biashara, ila zile za controlled economy zinafanya biashara. Kwote huko kuna pros na cons.

Lakini best practice ni Serikali kujikita na utengenezaji sera, regulatory na kukusanya kodi tu
 
Huyo mwenzako hapo amesema huko TRA Kuna the finest wanaoweza kulinda pesa zinazokusanywa
Wanajaribu lakini kuna red flags nyingi na ndiyo tatizo kubwa la Watanzania wanataka utajiri wa haraka haraka
 
Serikali za uchumi wa soko hazifanyi biashara, ila zile za controlled economy zinafanya biashara. Kwote huko kuna pros na cons.

Lakini best practice ni Serikali kujikita na utengenezaji sera, regulatory na kukusanya kodi tu
Nirahisishe swali, hizo serikali za uchumi wa soko ni zipi? Namaanisha taja nchi flani
 
Kuna regulatory framework inayo check yote hayo
 
Kwani hapo TPA wewe uko idara gani? Usiogope mabadiliko kwani ukiwa mchapa kazi wataķu take on board tu
 
kati ya vitu tunavyotakiwa kuwa makini navyo, hiki ni kimojawapo. ukiona mtu anaita ndugu zake wamiliki mashamba ya jumuiya ujue amehakikishiwa kwamba watamlinda, na pia kikinuka anapo pa kukimbilia na wamemhakikishia akikwapua mali watamtunzia huko kwao. Shindwa kabisa shetani kwa Jina la Yesu.
 
Arusha hakuna uwanja wa ndege wa kimataifa
 
Kwani hapo TPA wewe uko idara gani? Usiogope mabadiliko kwani ukiwa mchapa kazi wataķu take on board tu
Kutoka kutoa points ambazo pengine zingeweza kuleta mjadala mzuri mpaka kuhamia kwenye utani
Sihusiki na kazi yoyote TPA, maswali yangu yamekuja kutokana na kile mlichokua mnakiandika hapa
 
Tulaumu WASOMI wenye vyeti Kwanza Ila akiri Hamna kabisa, thinking yao iko low Sana, alafu ukute huyo mshauri ana MKE na watoto anaitwa Baba Bora au mama Bora HUKU akitaka watoto wao wapate baraka za Mungu, (mara nyingi wanapataga RAHANA ya ukoo).
Najiuliza aliyeahauri serikali kuamisha kituo cha mabasi ubungo kwa kuandika Sababu zenye mantiki alafu huyo huyo akaweza na kumkaribisha MCHINA awake EAST AFRICA COMMERCIAL AND LOGISTICS CENTRE pale pale ambapo miundo mbinu ilikuwepo Kwa 90%, na kusababisha tatizo kubwa zaidi hapo badae. Ama tuna tatizo tumewapa MAMLAKA mkubwa kisheria wanasiasa kupanga Maisha yetu au hatuwashirikishi watafiti WABOBEZ tunapotaka kupanga miji na biashara.ni mpumbavu pekee na darasa la Saba asiye na Chet anaweza kuishaurui serikali kumruhusu Mchina awake biashara yake pale inayotegemea kuwa na warehouse, shops kama 2000, maroli kuingia pale , MWENDO Kasi kuwa pale, reli kuwa eneo Hilo na road network kuwa pale alafu eti 33yrs ndo itakuwa Mali ya WATZ.. KUNA HAJA YA KIZAZI KINACHOSOMA SASA MASHULENI NA VYUONI KUWA NA STUDY TOUR nje ya nchi yao Kwa mwaka angalau 1, katika kipindi cha masomo Yao wajifinze mataifa mengine walivyo wabinafsi kutawaaliwa na Mgeni au Muwekezaji kuwa na nguvu kuliko mzawa..if u want a peace start a war..Karljang. tuna WASOMI wapuuzi na wasio focussed wanaoharib KIZAZI chao kwa ubinafsi na uchoyo uroho na roho za uchawi mioyoni kwao...Ila ukimuona anatembea utadhani ni mtu mwema. Aibu sana
 
Mna chuki tu na mwarabu,na hamumchukii mwarabu kwa uarabu wake,Bali dini yake,angelikua mkiristo Wala msingetokwa jasho la makalio kumpinga,pingeni na Airtel na nmb tuone
Hio Airtel unajua inamilikiwa na nani? Na hio nmb unajua inamilikiwa na nani? Unaweza kuweka dondoo kwa ndani na si kutuuliza sisi maswali unatukera... Weka info! Na sikujibu kwa jazba
 
Hio Airtel unajua inamilikiwa na nani? Na hio nmb unajua inamilikiwa na nani? Unaweza kuweka dondoo kwa ndani na si kutuuliza sisi maswali unatukera... Weka info! Na sikujibu kwa jazba
Airtel ya mhindi,nmb serikali Ina hisa chini ya 32%,Kuna wazungu ndani ya nmb,pigeni kelele na huko
 
Nimekupata mkuu
Report ya CAG 2022, angalia humo uone bilioni 4 zilizvyopotea BOT kwa sababu tu waliziteketeza sababu ya uchakavu. CAG akagundua haikua sahihi, uliza sasa nani alikamatwa au kuwajibishwa
Tunahangaika na kilichopo kwenye sahani wakati sufuria zima bado limeshikiliwa na hao hao
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…