Huwa mnawakanya mambo muhimu ya kuzingatia huko vyuoni?

Huwa mnawakanya mambo muhimu ya kuzingatia huko vyuoni?

Kwani ambao hawapiti vyuo huruka stage mkuu
Stage inategemea tu,,,ila kikubwa kwa vijana wengi hasa wanaopitia chuo hio ni stage kubwa ya kujifunza,,kuna wale wanajilipua wakifulia wanashindia mikate na maji hadi boom lingine maisha yanaenda, na kuna wengine wakishafulia matatizo ndo yanaanza mwisho wa siku wanarukaruka wanakutana na wakina pididi wanavuliwa vyeo na magonjwa juu.....kuna wengine hawajapitia vyuoni ila wakianza kupata maboom yakitaa akili zinawaruka
 
Oya wana Jamiiforums hivi hawa madogo kabla ya kwenda Chuo Kuenjoy na bata sijui Boom. Hivi huwa mnawakanya mambo muhimu ya kuzingatia huko vyuoni.... ✍️
images (12).jpeg
 
Siamini kama kumkanya mtu kunatosha kumzuia asifanye makosa.

Makosa ni mazuri, ni sehemu ya maisha, fanyeni makosa.
Nakubaliana na wewe.

Binafsi nipo chuo na nimejifunza kutokana na makosa
Kuweni makini.Mkirudi nyumbani na miupuuzi yenu mkifurushwa msianze visingizio.Tengenezeni maisha yenu kwanza halafu baadaye mtakula mbuguswa,mitowo,kuku hadi bata bila kuchungwachungwa kama ngedere-mwitu.
NB:Hata mkianza kujitegemea mtapaswa kufuata sheria za nchi accordingly!Maisha ni mchakamchaka.Jifunzeni kuishi kwa sheria,kanuni na malengo tangu mkiwa wachanga.
Nashukuru sana Mkuu, hili limepokelewa kwa dhati na ninaamini linaweza kubadilisha mtazamo na maisha yetu tunapoipambania elimu.

Nitazingatia Mkuu.
 
Wewe unamkanya nani umr wa miaka 17-29 ni umri wa kujifunza ni heri mtu asiruke stage Ili baadae tuondokane na wazee wa hovyo na wamama wanaopenda vijana
Aliyekwambia "uzee wa hovyo" na "wamama wanaopenda vijana" inaondolewa na kufanya starehe ujanani ni nani?
 
Back
Top Bottom