Wild Flower
JF-Expert Member
- Jul 20, 2023
- 378
- 766
Kuharibu nyaraka zinazohusiana na taarifa za kibinafsi, kama vile kiatambulisho cha NIDA, cheti cha kuzaliwa, taarifa za benki, taarifa za kadi ya mkopo, stahili za malipo, au risiti, ni muhimu ili kuhakikisha kuwa taarifa zako binafsi haziangukii mikononi mwa watu wasiostahili kuziona. Hii pia inasaidia kukulinda dhidi ya wizi wa utambulisho.
Hii ni njia bora za kuhakikisha kwamba taarifa zako binafsi zinaharibiwa vizuri na haziwezi kutumika vibaya.
1. Ikiwa unayo mashine ya kuchana nyaraka, tumia "shredder" ili kuziharibu, kisha weka vipande vya nyaraka katika mifuko na kuzitupa kwenye takataka. Shredders za hukata nyaraka hizo na hutengeneza vipande vidogo vya karatasi jambo ambalo linazuia wizi wa kutengeneza tena kurasa kamili kutoka kwa vipande vya karatasi.
2. Ikiwa eneo ulilopo kuna ruhusa ya kuchoma moto kufanya hivyo, unaweza kuchoma nyaraka hizo kwenye shimo la moto na kutawanya majivu yake.
3. Pia, unaweza kuloweka karatasi kwenye maji na bleach ili kuyeyusha nyaraka hizo.
4. Kwa nyaraka za kidijitali, unaweza kuzifuta kabisa kwa kuzifuta (overwrite), kuzidhoofisha (degauss) au kuharibu kifaa kwa kukiponda ponda kam vile hard disc ili kuhakikisha taarifa hazirejeshwi.
2. Ikiwa eneo ulilopo kuna ruhusa ya kuchoma moto kufanya hivyo, unaweza kuchoma nyaraka hizo kwenye shimo la moto na kutawanya majivu yake.
3. Pia, unaweza kuloweka karatasi kwenye maji na bleach ili kuyeyusha nyaraka hizo.
4. Kwa nyaraka za kidijitali, unaweza kuzifuta kabisa kwa kuzifuta (overwrite), kuzidhoofisha (degauss) au kuharibu kifaa kwa kukiponda ponda kam vile hard disc ili kuhakikisha taarifa hazirejeshwi.
Hii ni njia bora za kuhakikisha kwamba taarifa zako binafsi zinaharibiwa vizuri na haziwezi kutumika vibaya.