Huwezi amini kwamba hawa nao ni wasomi wa UDSM wanasaka degree

Wameigiza na kuja kuileta hapa, there is a hidden agenda behind this post.
 
Hawajalipia chumba wanapiga mahesabu ya kunywa pombe tu. Hiyo ni mabibo ila lawama kwa wanafunzi wanaobadili matumizi ya accomodation and meal allowance na kwenda kuolea wake. Kulala mzungu wa nne ni kawaida sana kwa mabibo, haikwepeki kulingana na maisha halisi. Ila bila godoro! Huyo amejitakia
 
Hiyo picha ni ya kweli, na mmoja wa hao waliolala tupo naye ndani ya shuttle bus sasa hivi
 
hapo umenena ukweli, unajua huu uhuru wa kila m2 kuandika na kutoa maoni kwa kila ki2 kinachokatiza maele yake ndiko kunakopotosha umma, kwa m2 aliepita mabibo akaishi anajua hali halisi, kajilaza kwenye vyuma anategemea nan amuonee huruma? kama bumu kapewa ina maana ameshindwa kujiongeza? basi elimu haikaa imkomboe kamwa kama ameshindwa kujimanage mwenyewe binafsi, kimsingi kama ulivyosema atakua hajalipia rumu na asipoangalia hicho kitanda atapewa mwingine, utamuona anakuja kulalamika tena humu ati vyumba vinatolewa kwa rushwa, akalale pale cafeteria c ndo alikowekeza hela zake, nonsense
 
msishangae sana haya maisha mbona yameanza kitambo sana hapo udsm... mimi nimekuwepo bibo tangu 2006 lakini life ilikuwa kama inavoonekana pichani
 
Nimecheka sana! Nilipomuangalia huyo wa juu. Japo inauma. Ni ishara ya wazi ya umasikini uliokithiri. Ni sehemu ya madhara ya 'no loan'. Huyo jamaa anayo imani kubwa sana na shule. Hatari ni pale atakapohitimu na kukosa kazi. Yote kwa yote, hosteli takribani vyuo vikuu vya Tz zipo hivyo. Kuna wanafunzi kibao, wasichana kwa wavulana, kibao wanauza vyumba na kwenda kubebana (kulala mzungu wa nne).
 
Hivi mnataka Chama Tawala kifanyeje
Godoro waibe Wanachuo, lawama Serikali
Hapo awali, kulikuwepo kila kitu sasa wanaoiba wanataka wenzao wakasome wapi?
Mtoa mada sijajua lengo lake ila Wasomi wa siku hizi mmekuwa lainilaini sana bora JKT irudi ili ukimaliza Foem VI upitie huko na ukifika Chuo utakuwa na Nidhamu.
Sisi mwaka Operesheni Nadhamu Makutupora kabla ya kwenda Chuoni tulilala kwenye vitanda vya chaga za fito za mitunduru na ukizubaa unafuga kunguni hasa.
sasa nyi hamjapitia huko mnataka mabadiliko gani tena, mletewe Godoro la Upepo na perfumes?

 

una uhakika kwamba wote hao wanapokea boom.una idea na kitu kinaitwa 'no loan'. unadhan wanafurahia kulala kwa staili hiyo.una habari kwamba wangeweza kujitutumua na hela zao ndogo za mfukoni na kulipia malaz hapo hostel lakin vyumba havitoshi hivyo wanaobahatika kupangiwa vyumba ni wachache.una habari kuwa zaidi ya 50% ya wanachuo wa mliman wanalala mzungu wa nne.unadhan wanapenda kulala sytle hiyo kwnye vitanda vidogo vya size ya 3,1/2 kwa 6. tafakari kwanza kabla ya kukurupuka na kucomment vitu usivyovifahamu vizuri
 
Hiyo ni ishara ya wazi ya umasikini ulioptiliza. Ni matokeo ya 'no loan'. Huyo jamaa wa deka ya juu anayo imani kubwa ssana na shule. Hatari ni pale atakapohitimu na kukosa ajira.
Wanachuo wenhi huuza vitanda vyao, kisha kulala wawili ili kupata hela za kukidhi mahitaji ya kila siku, wengi wao wanatoka familia duni sana. Si rahisi sana kwa wale wa 'mboga saba' kuuza vitanda. Hili nina uzoefu nalo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…