Huwezi kumiliki/ kumilikishwa/ kuendesha LC 300 kama hutumii nguvu za giza

Huwezi kumiliki/ kumilikishwa/ kuendesha LC 300 kama hutumii nguvu za giza

Maisha ni siri, kuna sayansi iliyojificha inayomfanya mtu kuonekana bora kuliko wengine, maburungutu ya fedha na nafasi za upendeleo zinakuwa zinamfuata yeye tu, madili yote ya hela yanamfuata yeye; badala ya yeye kutumia nguvu nyingi kuzitafuta.

''They get rich b'se they do things in uncommon way'' Itafute hiyo ''uncommon way''
Hapo ndipo tofauti ya sisi na akina Bhakressa ilipo! Ila kuna raia wanakaza ubongo tu.

Fumbo la kiimani hilo!
 
Yamkini mazingira uliyokulia ndiyo yamekukutanisha na hayo, maana wanasema ukiwa rafiki na mwizi hata we unaweza kuwa mdokozi, nimeishi maisha ya mjini sijawahi Kutana na huu upumbavu wa kishirikina, watu wenye fikra za ushirikina wengi wanatokea vijijini. Zunguka kwenye miji ya watu walipendelea huo upumbavu huukuti na bado watu wana pull mandinga hatari ya mabosi wao.
 
Amini kabisa ulozi unahusika katika mafanikio ya mtu ni vile watu wana roho mbaya hawataki mfanikiwe wote ila ingekuwa tunaelekezana njia wanazo pitia za ulozi mafanikio tungekuwa nayo.

Tunaaminishwa sana kuwa ukifanya kazi kwa bidii unafanikiwa lakini hao wanao tuaminisha ukifika ofisini mwao unakuta udi na ubani kama sio ulozi ni nini sababu ya kuchoma udi na ubani?
Mganga ni Connection tu kama hauna Connection sahihi utaenda vijiji vyote na hakuna kitu utapata zaidi ya kupoteza nauli na wazee kula kuku zako na mbuzi..
 
LC 300 and alike is not for everyone.

Sugua sana goti msikitini na makanisani, omba sana Mungu utaishia kwenye Prado mchaga.

Huku kwa ma LC 300 ni dunia nyingine, dunia ya maagano, lazima uwe na nguvu za giza sio kulinunua tu hata kuliendesha, hakuna mjinga atakubabidhi milioni 500 uzurure nayo mitaani kwenye kila aina ya risks.

Hakuna washirikina kama madereva wa serikali na mabasi ya mikoani plus malori, hizo kazi huzipata kwa kuroga na kuhonga sana, mjinga nani ajukabidhi na milioni upige nayo misele.

Tanzania ukichukua fomu tu Ugombee Ubunge watakuja wazee wakulazishe kukupa hirizi au wakufanyie kisomo.

, Mungu wetu kuna limit ya mafanikio ametuwekea sisi waafrica, kuna level tukifika huwa tunamkufuru,Tunajiona tumefanikiwa kwaakili zetu ndio maana misikitini na makanisani wale waumini wa kweli wanamaisha ya chini au ya kawaida sana, wale matajiri ukiwafuatilia ndio wamiliki wa majini, washirikina wakubwa.

Waafrica ni wanafiki sana, bado hatujaacha dini zetu za asili, kuanzia ijumaa mpaka jumapili tutaenda misikitini na nakanisani, tukitoka hapo tunapishana kwa waganga.

Asilimia kubwa tuko hivyo.

Tuendelee kuendesha crown tu ili tufike mbinguni.

Mimi binafsi sijawahi kwenda kwa mganga ila nimefanya kazi na watu ni washirikina hatari na nusu,Na yanapanda vyeo tu wanachodekiver hukioni.

Africa tukifika maendeleo kama ya ulaya makanisa ya kiroho ya akina mwamposa an a like yatafutika, tutabaki na yale madhehebu yetu makuu. Kuna watu wanajifanya kuombewa wakishafanikiwa huwaoni tena kanisani.Walifuata miujiza sio kujiweka karibu na Mungu ili waione pepo.

Pata picha unaamka asubuhi maji bombani hayakatiki,umeme haukatiki,ada ya watoto haisumbui,wakimaliza masomo wanaoata ajira, ukiumwa una uwezo wa kujitibia Agha khan,unadrive gari kali na una nyumba yako ya kuishi????

My friend Mwamposa atabaki na wale wateule wachache wanaotaka kwenda mbinguni,na sio wapenda miujiza
Kwaiyo wazungu wakifanikiwa huwa wanaona wamefanikiwa kwa nguvu ya nani?
 
Waganga wenyewe hawazitaki hizo hela, wanawaachia ambao hawajui madhara yake na waliojawa na tamaa.

Wanatamba nazo lakini mwisho wao hauwezi kuwa mzuri.
Mwisho wetu sote hauwezi kuwa mzuri kwasababu wote mwisho wetu ni kufa au kuzeeka Kisha kufa na hivyo vyote sio vizuri kwa mwanadamu
 
Yamkini mazingira uliyokulia ndiyo yamekukutanisha na hayo, maana wanasema ukiwa rafiki na mwizi hata we unaweza kuwa mdokozi, nimeishi maisha ya mjini sijawahi Kutana na huu upumbavu wa kishirikina, watu wenye fikra za ushirikina wengi wanatokea vijijini. Zunguka kwenye miji ya watu walipendelea huo upumbavu huukuti na bado watu wana pull mandinga hatari ya mabosi wao.
Umeishi mji upi?nimezaliwa DSM enzi za Nyerere,hakuna sehemu kuna ushirikina kama kariakoo,usione maduka yale ukadhani yspoyapo tu,wapemba,wakinga ni noma kariakoo ni jehanam kabisa

Asubuhi nenda Azania front au KKKT kariakoo,kuna ibada za asubuhi,wale sio wajinga kumuomba Mungu,kuna vita ya kiroho sana huko maofisini hata hao wasomi wanarogana mno,huwezi kuamini ila ndio hivyo,madereva wa STK waogope
 
Tofautisha mchawi na mshirikina
Wachawi wanaongozwa na miiko ya kazi yao,ni mchezo wa kijinga faida yake ni kujifurahisha tu ila wrngi hawana maendeleo,africa kuna washirikina wengi sana,wataenda kanisani na misikitini na kwa waganga wataenda kisirisiri
Kikundi kimoja cha nyimbo za kumsifu mungu kiliwahi kutoa kibao kimoja kinaitwa "Mchanganyo"

Ukiisikiliza vyema hiyo kwaya utapata maana sahihi ya kauli yako ndugu Mdukuzi, naungana nawe na nimekuelewa vizuri Sana!
 
Back
Top Bottom