Nikifa MkeWangu Asiolewe
JF-Expert Member
- Feb 26, 2024
- 6,944
- 14,351
Nipo tiyari kukosolewa lakini Kwa uthibitisho tu na sio mbwembwe zingine.
Kwanza hakuna kwenye biblia sehemu yoyote Ile watu walifanya harambee ya kumnunulia mtume ama nabii punda ama farasi Kwa Wakati huo maana hapakuwa na magari Wala pikipiki.
Hivyo usafiri wao ulikuwa Punda,Ngamia au farasi. Lakini bado sijawahi ona waumini/washiriki wa kipindi hicho wakifanya changizo Ili wanunue japo punda ya nabii/mtume wao.
Kwanini na sema haya? Saivi dini zimegeuka kuwa biashara kubwa sana na wengi wamekuwa wakitoboa ndani ya muda mfupi.
Sababu zake ziko wazi tu.
Hapa nitataja makanisa makubwa mawili tu kama mfano achana na miradi binafisi ya wakina Geodavie, Malisa, Mwamposa, Sunguye nk.
Tangu ni zaliwe na kukulia katika Ukristo bado sijawahi ona eti kanisa limejengwa na mtu mmoja ama hata wao wenyewe makao makuu.
Katika Kijiji chetu tulikuwa tunasalia darasani miaka ya 90 Na badae tukaanza michango tukanunua kiwanja wenyewe bila msaada wa paroko ama katekista baada ya kununua kiwanja tukafyatua matofali ya tope sisi wenyewe.
Hatimaye tukaezeka kwa nyasi. Ukumbuke mafundi ilikuwa Bure kufyatua nk Kila kitu tulifanya juu yetu wenyewe watu wakijitoa Hadi misosi Wakati wa ujenzi wa kanisa Hilo.
Baada ya kukamilisha watu walizidi kuongezeka mara dufu na hatimae tukafanya harambee na kuezeka Kwa bati na kujenga Kwa cement.
Katika kipindi hicho chote tulikuwa tunatoa sadaka na zaka tu michango ilikuwepo kama tu hapo kanisani Kuna muumini anahitaji msaada na tulikuwa tunatoa shilingi kumi ishrini na wenye uwezo watatoa shilingi200 hata 500 kabisa.
Sasa baada ya kuwa wengi na kuwa tumejenga michango ikaanza maradufu sijui ilitokea wapi hasa miaka ya 2006-2009 michango ilikuwa mingi mara imetoka jimboni au parokiani. Hapohapo tunaambiwa kumtegemeza katekista nk.
Ketekista huyu huyu mnaishi nae anakwakwe analima na kufanya Kila kazi lakini Cha ajabu anategemezwa(kuchangiwa)
Hadi Sasa michango imekuwa mingi sana na kutajirisha watu wengine tu.
Hapa ni makanisa yote hata Kwa wasabato mambo ni Yale Yale wanaweza wakaanza wao huita kundi Hilo kundi linakuwa la watu hata7 tu au chini/zaidi ya hapo.
Lakini punde wakiwa wengi tu michango na harambee kuuziwa vitabu vya roho ya unabii lesoni nk ukipiga hesabu unaona wazi kabisa hapa hizi ni biashara.
MFANO Kwa wasabato Kila baada ya miezi3 wanakuwa na lesoni mpya na wananunua na usiponunua Kuna mafungu kadhaa wakadhaa utasomewa ukitishwa kuwa hutakua kiroho utabaki Hivi Hivi miaka nenda Rudi.
Ukija kwenye vyombo vya mziki(choir) mtachangishwa kama kawaida kununua vyombo vya mziki vya kisasa. Yaani Kila kitu kinacho li husu kanisa mtachangishwa.
Lakini ikumbukwe kuwa Zaka na sadaka mnatoa Kila Leo na iwapo ikionekana matoleo yamekuwa kidogo atakuja kiongozi wa juu huko kuja kuhimiza watu wamtolee Mungu matoleo.
Kwa upande wa Roma wao wameenda mbali zaidi usipotoa michango na ikatokea ukapatwa na maswahibu basi tegemea hutapata msaada kutoka kanisani.
Ikumbukwe kule utauziwa Kila aina ya sanamu uitakayo japo sio lazima ila rozali ni muhimu utanunua Kuna kanga za bikira maria na batiki zenye picha ya yesu kabeba kondoo utauziwa. Sijui kanga za Wawata nk
Sasa Hivi tuna barua ya zawadi ya mtoto yesu ambayo tumepangiwa kiasi Cha kutoa Kwa waajiriwa!?
Ikifika kiangazi pia Huwa tunatoa shukuran ya mavuno (matomoro)
Pia Kuna matoleo maalumu Kila Misa hapa hutolewa Kila aina ya mazao inayopatikana maeneo hayo
MFANO wa matoleo hayo ni kama
Ndizi,tikiti mahindi,tambi,Mvinyo kama dompo,asali,mbuzi,kuku,mchele nk
Lakini michango Iko palepale na hawana huruma na maisha Yako.
Ukipata tatizo wewe utaombewa ila wao wakipata shida watahitaji Hela. Tuamke.
Kwa kifupi mambo ni mengi sana ambayo tunayafanya wenyewe tu bila kutegemea msaada wa wazungu (makao makuu) lakini punde tu tukikamilisha Hela zinaenda huko zote.
MFANO mkajichangisha mjenge shule ama hospital (jambo zuri ) Mtachangishana Kwa kushikana mashati Hadi shule/hospital mtamaliza lakini usitegemee eti Kwa sababu mlichangia Kwa kuuza kuku na mbuzi wako Ili ijengwe Ile shule utapata japo discount kidogo tofauti na yule hajachanga kabisa Bali ada utatoa kama kawaida na mtoto wako atarudishwa tu iwapo utachelewa kumlipia ada yake.
Cha ajabu ni kwamba Watoto wa wachungaji watasoma Bure Watoto wa maaskofu watasoma Bure kabisa licha kuwa hawo wachungaji wanalipwa mishahara minono kuwazidi Hadi waalimu.
Hapohapo wanaosomeshewa Watoto wao Bure usafiri wananunuliwa,nyumba anaishi Bure Tena nzuri chakula umeme na maji washiriki wanalipia.
Choo kikijaa kanisa litahusika kutoa Hela ya mzibuaji. Sasa unakaa unajiuliza inakuwaje hii na watu Bado hatuzinduki na kupinga haya mambo. Na hata itokee kanisani labda Kuna mtoto wa masikini asiye jiweza kusomesha na ana akili na hata kanisani ana mahudhurio mazuri namna Gani hawezi soma Bure otherwise washiriki washikane mashati kumchangia la sivyo hata soma abadani.
Nimesikia wasabato Hadi wamepelekana mahakamani Kwa kula rushwa mamilion ya kanisa. Hao wanaitwa watumishi wa Mungu wamemuibia Mungu Hela na suruhisho ni mahakamani Wala sio Kwa Mungu Tena.
Nimezungumzia makanisa mawili haya kama mifano achana na wajasiriamali wa hadharani kama nilivyo wataja hapo juu Hawa wameiga na kuja kiubunifu zaidi.
Ndio maana wanauza maji,vitambaa, mchanga na mafuta ya upako.Hawa wameiga tu.
Ifike mahala Sasa tutoke usingizini tupinge maana niliwahi kusikia mchungaji wa kisabato akisema michango itazidi kurindima Hadi yesu arudi. Kwa maana ya haraka yesu asiporudi mapema kazi tunayo na pona yetu yesu arudi mapema.
Nimeekeza Kwa uchache sana lakini yapo mengi zaidi yanafanyika.
Waafrica Vijana wenzangu wapo tiyari kuunda kwaya wakachangishana na kununua vyombo vya mziki vya mamilio ya shiringi. Lakini hao hao hawawezi kujichangisha walau wawe na kiwanda japo Cha kutengeneza sabuni kamwe hawawezi.
Tupingeni biashara hizi zilizo kuja Kwa mgongo wa dini.
Kwa maelezo haya yote naomba kujuzwa wapi kwenye biblia kumewahi kuwa na mshike mshike kama tulio nao Sasa?
NB: Usilete habari za Anania na safira hapa.
Kwanza hakuna kwenye biblia sehemu yoyote Ile watu walifanya harambee ya kumnunulia mtume ama nabii punda ama farasi Kwa Wakati huo maana hapakuwa na magari Wala pikipiki.
Hivyo usafiri wao ulikuwa Punda,Ngamia au farasi. Lakini bado sijawahi ona waumini/washiriki wa kipindi hicho wakifanya changizo Ili wanunue japo punda ya nabii/mtume wao.
Kwanini na sema haya? Saivi dini zimegeuka kuwa biashara kubwa sana na wengi wamekuwa wakitoboa ndani ya muda mfupi.
Sababu zake ziko wazi tu.
Hapa nitataja makanisa makubwa mawili tu kama mfano achana na miradi binafisi ya wakina Geodavie, Malisa, Mwamposa, Sunguye nk.
Tangu ni zaliwe na kukulia katika Ukristo bado sijawahi ona eti kanisa limejengwa na mtu mmoja ama hata wao wenyewe makao makuu.
Katika Kijiji chetu tulikuwa tunasalia darasani miaka ya 90 Na badae tukaanza michango tukanunua kiwanja wenyewe bila msaada wa paroko ama katekista baada ya kununua kiwanja tukafyatua matofali ya tope sisi wenyewe.
Hatimaye tukaezeka kwa nyasi. Ukumbuke mafundi ilikuwa Bure kufyatua nk Kila kitu tulifanya juu yetu wenyewe watu wakijitoa Hadi misosi Wakati wa ujenzi wa kanisa Hilo.
Baada ya kukamilisha watu walizidi kuongezeka mara dufu na hatimae tukafanya harambee na kuezeka Kwa bati na kujenga Kwa cement.
Katika kipindi hicho chote tulikuwa tunatoa sadaka na zaka tu michango ilikuwepo kama tu hapo kanisani Kuna muumini anahitaji msaada na tulikuwa tunatoa shilingi kumi ishrini na wenye uwezo watatoa shilingi200 hata 500 kabisa.
Sasa baada ya kuwa wengi na kuwa tumejenga michango ikaanza maradufu sijui ilitokea wapi hasa miaka ya 2006-2009 michango ilikuwa mingi mara imetoka jimboni au parokiani. Hapohapo tunaambiwa kumtegemeza katekista nk.
Ketekista huyu huyu mnaishi nae anakwakwe analima na kufanya Kila kazi lakini Cha ajabu anategemezwa(kuchangiwa)
Hadi Sasa michango imekuwa mingi sana na kutajirisha watu wengine tu.
Hapa ni makanisa yote hata Kwa wasabato mambo ni Yale Yale wanaweza wakaanza wao huita kundi Hilo kundi linakuwa la watu hata7 tu au chini/zaidi ya hapo.
Lakini punde wakiwa wengi tu michango na harambee kuuziwa vitabu vya roho ya unabii lesoni nk ukipiga hesabu unaona wazi kabisa hapa hizi ni biashara.
MFANO Kwa wasabato Kila baada ya miezi3 wanakuwa na lesoni mpya na wananunua na usiponunua Kuna mafungu kadhaa wakadhaa utasomewa ukitishwa kuwa hutakua kiroho utabaki Hivi Hivi miaka nenda Rudi.
Ukija kwenye vyombo vya mziki(choir) mtachangishwa kama kawaida kununua vyombo vya mziki vya kisasa. Yaani Kila kitu kinacho li husu kanisa mtachangishwa.
Lakini ikumbukwe kuwa Zaka na sadaka mnatoa Kila Leo na iwapo ikionekana matoleo yamekuwa kidogo atakuja kiongozi wa juu huko kuja kuhimiza watu wamtolee Mungu matoleo.
Kwa upande wa Roma wao wameenda mbali zaidi usipotoa michango na ikatokea ukapatwa na maswahibu basi tegemea hutapata msaada kutoka kanisani.
Ikumbukwe kule utauziwa Kila aina ya sanamu uitakayo japo sio lazima ila rozali ni muhimu utanunua Kuna kanga za bikira maria na batiki zenye picha ya yesu kabeba kondoo utauziwa. Sijui kanga za Wawata nk
Sasa Hivi tuna barua ya zawadi ya mtoto yesu ambayo tumepangiwa kiasi Cha kutoa Kwa waajiriwa!?
Ikifika kiangazi pia Huwa tunatoa shukuran ya mavuno (matomoro)
Pia Kuna matoleo maalumu Kila Misa hapa hutolewa Kila aina ya mazao inayopatikana maeneo hayo
MFANO wa matoleo hayo ni kama
Ndizi,tikiti mahindi,tambi,Mvinyo kama dompo,asali,mbuzi,kuku,mchele nk
Lakini michango Iko palepale na hawana huruma na maisha Yako.
Ukipata tatizo wewe utaombewa ila wao wakipata shida watahitaji Hela. Tuamke.
Kwa kifupi mambo ni mengi sana ambayo tunayafanya wenyewe tu bila kutegemea msaada wa wazungu (makao makuu) lakini punde tu tukikamilisha Hela zinaenda huko zote.
MFANO mkajichangisha mjenge shule ama hospital (jambo zuri ) Mtachangishana Kwa kushikana mashati Hadi shule/hospital mtamaliza lakini usitegemee eti Kwa sababu mlichangia Kwa kuuza kuku na mbuzi wako Ili ijengwe Ile shule utapata japo discount kidogo tofauti na yule hajachanga kabisa Bali ada utatoa kama kawaida na mtoto wako atarudishwa tu iwapo utachelewa kumlipia ada yake.
Cha ajabu ni kwamba Watoto wa wachungaji watasoma Bure Watoto wa maaskofu watasoma Bure kabisa licha kuwa hawo wachungaji wanalipwa mishahara minono kuwazidi Hadi waalimu.
Hapohapo wanaosomeshewa Watoto wao Bure usafiri wananunuliwa,nyumba anaishi Bure Tena nzuri chakula umeme na maji washiriki wanalipia.
Choo kikijaa kanisa litahusika kutoa Hela ya mzibuaji. Sasa unakaa unajiuliza inakuwaje hii na watu Bado hatuzinduki na kupinga haya mambo. Na hata itokee kanisani labda Kuna mtoto wa masikini asiye jiweza kusomesha na ana akili na hata kanisani ana mahudhurio mazuri namna Gani hawezi soma Bure otherwise washiriki washikane mashati kumchangia la sivyo hata soma abadani.
Nimesikia wasabato Hadi wamepelekana mahakamani Kwa kula rushwa mamilion ya kanisa. Hao wanaitwa watumishi wa Mungu wamemuibia Mungu Hela na suruhisho ni mahakamani Wala sio Kwa Mungu Tena.
Nimezungumzia makanisa mawili haya kama mifano achana na wajasiriamali wa hadharani kama nilivyo wataja hapo juu Hawa wameiga na kuja kiubunifu zaidi.
Ndio maana wanauza maji,vitambaa, mchanga na mafuta ya upako.Hawa wameiga tu.
Ifike mahala Sasa tutoke usingizini tupinge maana niliwahi kusikia mchungaji wa kisabato akisema michango itazidi kurindima Hadi yesu arudi. Kwa maana ya haraka yesu asiporudi mapema kazi tunayo na pona yetu yesu arudi mapema.
Nimeekeza Kwa uchache sana lakini yapo mengi zaidi yanafanyika.
Waafrica Vijana wenzangu wapo tiyari kuunda kwaya wakachangishana na kununua vyombo vya mziki vya mamilio ya shiringi. Lakini hao hao hawawezi kujichangisha walau wawe na kiwanda japo Cha kutengeneza sabuni kamwe hawawezi.
Tupingeni biashara hizi zilizo kuja Kwa mgongo wa dini.
Kwa maelezo haya yote naomba kujuzwa wapi kwenye biblia kumewahi kuwa na mshike mshike kama tulio nao Sasa?
NB: Usilete habari za Anania na safira hapa.