Huyu customer care wa benki hii hana kazi ya kufanya?

Planett

JF-Expert Member
Joined
Mar 20, 2014
Posts
10,497
Reaction score
16,180
Straight to the topic,

Juzi kati kuna hela nilikua natarajia iingie kwenye acount yangu sasa nikawa nimeangalia sana salio ile siku kama mara 8 hivi ila hela ikawa haijaingia, nikaona isiwe kesi nikatulia zangu.

Sasa mida ya jioni nikaona simu inaita nikapoke, aliyepiga akajitambulisha kua ni customer care wa bank husika kwa sauti nzuri inayovutia. Maongezi yalikua hivi:-

Customer care:- Naitwa _____ napiga simu kutoka EXPORTIMPORT BANK, naongea na Planett ?
Mimi :- Ndio
Customer care: Nimeona umeangalia salio hapa nilitaka kukujuza kua KUNA HUDUMA NYINGINE UNAWEZA KUZIFANYA ZAIDI YA KUANGALIA SALIO
Mimi :- Kimya huku nikijiuliza "what the fvck am I hearing"
Customer care:- Planett unanipata
Mimi :- ahsante nashukuru, nikaondoka hewani.

We mdada wa hiyo bank uache kufuatilia maisha ya watu.
 
πŸ˜‚πŸ˜‚ aisee kumbe tunafatiliwa namna iyo
 
🀣🀣🀣🀣🀣 customer care ametisha sana🀣🀣🀣
 
Nimecheka snaa sah πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚

Ila bro una kifua sana. Mi ningeropoka matusi yote ninayoyajua.
 
Umeona anakuzingua ee!Siku nyingine akizingua mtongoze aache zake mkuu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…