Huyu Floyd Mayweather ni kumuombea afulie tu

Tatizo lenu nyinyi maskini mnataka kuwapangia matajiri jinsi ya kutumia pesa zao.
Kama unajua sana maisha mbona wewe hizo pesa wewe huingizi
Maywether hatokaa afulie maisha yake yote yule ata leo akiita pambano ataingiza pesa ambazo wewe na ukoo wenu mtabaki kuziota

Maskini punguzeni kuhate. Umaskini wako haujasababishwa na maywether


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
hahhaa hili jamaa si ndio inasemekana halijui kusoma! yaani macellebs wa mbele wa hovyo sana aisee pamoja na mwenzie R.kelly ambae kwenye uwasilishwaji wa tuzo aliwekewa teleprompter awe anasoma akatia aibu hajui kusoma
 
Aliyoyapitia mtu mweusi,ndio yanasababisha jamaa awe hivyo..!
Ila haya maisha mafupi sana aisee,muache jamaa afanye kinachompa furaha..!
As long as hakuna madhara anayosababisha kwa jamii inayomzunguka,basi yupo sawa tu,hiyo inaitwa USINIPANGIE..!
 
hahhaa hili jamaa si ndio inasemekana halijui kusoma! yaani macellebs wa mbele wa hovyo sana aisee pamoja na mwenzie R.kelly ambae kwenye uwasilishwaji wa tuzo aliwekewa teleprompter awe anasoma akatia aibu hajui kusoma
Kuna wakati huwa nahisi haya maisha yako tricky sana...
Kujua kusoma sio big deal kwa mtu mwenye pesa kama Meiweidha..!
 


Naomba anuani yake tafadhali....nataka nimshirikishe mchawi wetu Mshanajr tukamuibie kishirikina.
 

Free big Meech namjua light skinned these are rappers pay homage to him.
Yupo Jela bado
 
Mungu ni wa ajabu sana, unaweza usikute asifulie..

Kwa imani yangu mimi mungu anapokupa ama kukunyima huwa vyote ni mitihani na katika mitihani yote aidha umshukuru ama umkufuru..
Wapo wanaopewa wanamshukuru mungu na wengine wanamkufuru mungu
Wapo wasiopewa wanamshukuru mungu na wengine wanamkufuru mungu. Najua nimeeleweka japo kwa uchache.
Mtu anapewa anashukuru anajua mali zinatoka kwake mola wetu mlezi na wala hazitumii vibaya, anatumia kwa njia ile inayompendeza allah huyu ni mwenye kufaulu, wapo wenye mali wanatumia kwa njia mbaya huyu ni mwenye kufeli

Na ndio maana tunafundishwa tunapoomba mali, tumuombe mungu atupe mali ambazo hazitakuwa mtihani kwetu, mali ambazo hazitatushinda nafsi zetu, mali ambazo hazitotupelekea kukufuru.

Kuna kisa kimoja cha nabii nadhani ni musa(a.s) alimuomba mungu yeye mussa ndio awe mgawa rizik allah akamkatalia musa akang'ang'ana, allah akataka kumuonesha kitu akamwambia musa aende akasimame sehemu hapo ndipo atakabiziwa hiyo kazi rasmi basi musa akaenda pale, muda si mrefu baada ya kufika eneo lile wakatokea watu wamekuja kuzika, walipomaliza Wakaondoka, muda si mrefu wakaja watu wakaifukua ile maiti wakaizini mussa aligadhabika mnoo, ila hakwenda kufanya kitu sababu alikuwa anasubiri jambo la msingi ambalo akikabidhiwa kirungu watu watamkoma, walipoondoka baada ya muda kupita mungu akamuuliza musa je watu wale unafanyaje, musa akajibu km akipewa yeye hyo kazi watu wale hawapati abadani asilani, mungu akamjibu kuwa hyo kazi haiwez, sababu yeye mungu anawapa wenye kumshukuru, wenye kumkufuru wacha mungu n.k.

Sasa wewe ndugu yangu unaweza ukaomba mwenzio afulie ndio akazidi kupiga mpunga, inakera ila ndio maisha yake.. [emoji23][emoji23][emoji23]

Sent using my nokia ya tochi
 
Wabongo kama kawaida yetu...
Akati anazisaka tunabaki watazamaji akizipata unataka umpangie matumizi dadekiii
Maisha mafupi aya anazipata kihalali mwache aenjoy maisha yake

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Alinikera katika hiyo video. Nikaona hapa ni bure kabisa.....

Hivi angekuja na hata dola milioni moja tu hapa africa akawekeza katika migodi ya dhahabu au almas fala huyu angekuwa katika hali gani.

Yaani mwenye akili ni Akon tu, ambae kachuma mahela kisha karejea Africa kufanya uwekezaji......

Haya ndio mafala yanayotufanya waafrika tuonekane akili hatuna

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Jamaa ana ushamba flani utadhani hizo hela aliziokota tu mahali...kumbe kahustle kuzipata lakini kama hajazizoea hela kabisaa... ushambaa mwingiii

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…