Huyu Gentamycine wa JF ni nani haswa?

Huyu Gentamycine wa JF ni nani haswa?

Nawaomba Moderators na Wamiliki wa JamiiForums fanyeni ' Utaalam ' wenu wote mnaoujua na kama ikiwa ni kweli Mimi GENTAMYCINE nina hii ID na nimejianzishia huu ' uzi ' mnifungie ' permanently ' Mimi kuwepo humu Jamvini. Halafu ifike muda Watu muache chuki na uswahili uliotawaliwa na Wivu kwa kudhani kuwa Mtu yoyote anayeuliziwa humu basi anajipigia ' Promo '. GENTAMYCINE sina haja ya Kujipigia ' Promo ' kwani Mimi tayari ni ' Promo ' tosha na ni maudhui yangu na uandishi wangu humu ambao mara nyingi huwa nauchanganya na ' ukomedi ' wangu wa asili ndiyo huwavutia Watu wengi hadi kupelekea Wao Kunipenda, Kunikubali na wengine kila Uchao ' Kunifolo '.

Na ndiyo maana hata Signature yangu tu inamajibu ya kutosha Kwenu ' Wanafiki ' wote inayosema ' Purely Talented and Charismatic Fella '.

Aliyebarikiwa kabarikiwa tu halafu ' Nyota ' ya Mtu inayong'aa kila Kukicha huwezi kuizima hata ufanyeje na msinichukie Mimi kuwa Kipenzi cha Members wengi hivi bali jiulizeni nyie ' mnaonichukia ' na kusema huu ' uzi ' nimejianzishia mwenyewe kwamba kwanini hamkubaliki kama GENTAMYCINE huku wengine mkiwa na muda mrefu humu JamiiForums kuliko Mimi niliyejiunga rasmi humu mwaka 2013.

Na kwa taarifa yenu tu ni kwamba kadri mnavyozidi ' Kunichukia ' na kunionea ' Kijicho ' humu ndiyo mnazidi kunifanya niwe ' maarufu ' na niwe mbunifu wa kuja na mada mbalimbali motomoto ambazo zinazidi kunifanya niwe tofauti na nyie. Waswahili ni Waswahili tu siku zote.

naona umeamua kutupa za uso.siyo siri mimi mwenyewe ni shabiki wako unanikosha sana na uandishi wako uliojaa umajivuni uliotukuka.
 
Acha kuibia watu

JamiiForums huwa tunaenda na ushahidi ulio Kuntu kabisa hivyo Mimi kama GENTAMYCINE nimekuruhusu uweke hadharani hicho nilichokiiba na kama pia Wewe au huyo niliyemuibia ananijua na ana Picha yangu ruhsa kuiweka hapa hadharani ili Mimi unayedai nimeiba nijulikane na nikamatwe vinginevyo nawaachia Moderator na Uongozi mzima wa JamiiForums kupitia akina Paw ,JamiiForums na Maxence Melo mwenyewe uweze kutoa ' Hukumu ' inayostahili Kwako. Nausubiri huo ushahidi wako uliopelekea Wewe kusema Mimi niache Kuibia Watu.
 
naona umeamua kutupa za uso.siyo siri mimi mwenyewe ni shabiki wako unanikosha sana na uandishi wako uliojaa umajivuni uliotukuka.

Sinza hawajambo Kijana? Bado upo pale pale Posta PPF Tower? Naona Mtandao wako ule sasa unafanya vyema Kijana hongera mno. Nisalimie wale Vijana wenzako wawili unaoishi nao hapo Sinza. Kwa Wambulu na Wanyankole wako umeenda kuwasalimia lakini?
 
Sinza hawajambo Kijana? Bado upo pale pale Posta PPF Tower? Naona Mtandao wako ule sasa unafanya vyema Kijana hongera mno. Nisalimie wale Vijana wenzako wawili unaoishi nao hapo Sinza. Kwa Wambulu na Wanyankole wako umeenda kuwasalimia lakini?
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Siku hizi JF watu wameamua kujipigia promo.

Embu weka picha ya huyo mtu tumuone kwanza halafu weka na link alizoandika zenye hoja motomoto tuzione.

Isije kuwa mnakuja na ID mpya.
Hilo nalo neno
 
Hivi si inawezekana mtu akaunda ID feki (anonymous) kisha akaitumia kuisifu ID yake iliyo maarufu?

Nakuomba pitia post yangu # 56 ina majibu yako ya kutosha tu tafadhali na pia kama utakuwa na ushahidi wowote juu ya madai yako weka hapa hadharani au uwasilishe haraka kama siyo upesi sana kwa wenye huu Mtandao wangu pendwa wa JamiiForums ili waweze kunichukulia hatua kali za Kinidhamu ili iweze kuwa Fundisho kwa Members wengine wenye hizo unazoziita Multiple ID's.
 
Hilo nalo neno

Siyo Kosa lenu ila najua kinachowatesa ni Kitu kidogo tu nacho ni Mimi kuwa 100% ' Purely Talented and Charismatic Fella '. Na bado nitawatesa mno hadi mpasuke kwa Wivu na Kunichukia.
 
Siyo Kosa lenu ila najua kinachowatesa ni Kitu kidogo tu nacho ni Mimi kuwa 100% ' Purely Talented and Charismatic Fella '. Na bado nitawatesa mno hadi mpasuke kwa Wivu na Kunichukia.
Hakuna akuchukuiye mkuu huo ni mtazamo wako mdogo
Haters makes yuh famous so keep the fire burning if that is what yuh believe! !

Sent from my SM-J110H using JamiiForums mobile app
 
Nakuomba pitia post yangu # 56 ina majibu yako ya kutosha tu tafadhali na pia kama utakuwa na ushahidi wowote juu ya madai yako weka hapa hadharani au uwasilishe haraka kama siyo upesi sana kwa wenye huu Mtandao wangu pendwa wa JamiiForums ili waweze kunichukulia hatua kali za Kinidhamu ili iweze kuwa Fundisho kwa Members wengine wenye hizo unazoziita Multiple ID's.
Nimeuliza JE INAWEZEKANA? Hilo tu. Sijashutumu mtu, mbona una mashaka?
 
Hakuna akuchukuiye mkuu huo ni mtazamo wako mdogo
Haters makes yuh famous so keep the fire burning if that is what yuh believe! !

Sent from my SM-J110H using JamiiForums mobile app

Sijasoma na sijui Kiingereza Mkuu hivyo kama vipi naomba unitafsirie kwa Kiswahili tu hapo ulipoandika kwa lugha hiyo adhimu ya Malkia na Waliberali.
 
Siku hizi JF watu wameamua kujipigia promo.

Embu weka picha ya huyo mtu tumuone kwanza halafu weka na link alizoandika zenye hoja motomoto tuzione.

Isije kuwa mnakuja na ID mpya.
24293931_322914031524635_1835261501088240493_n.jpg
 
Back
Top Bottom