Huyu kaka kabila la Mkurya alinishangaza!!!!

Huyu kaka kabila la Mkurya alinishangaza!!!!

Mwisho wa tukio, walimchukua yule kaka aliyechomwa wakaanza kumpaka asali, na yule katili akawa pale pale wala sikuona aliyethubutu kumkamata!!
Ilinitisha sana mkuu Antonio de Guzman
Pole sana kwa kuogopa nahuja but kwa mie wala nisingeogopa maana nishashuhudia matukio zaidi ya ilo like watu wanakatana mapanga live
 
Hakunaga kidogo wala kikubwa.

Ndio maana, unaambiwa ni heri ukutane na Dubu aliepoteza mtoto kuliko mwanadamu mwenye hasira (anaweza fanya mengi sana).

Na huyo dogo ajifunze, kulimaliza lile aliloloanzisha. Sio una provoke watu huku ukitegemea kila mtu yupo weak, na mjinga.
😳😳
 
Jana nikiwa kwenye ofisi za kampuni za mabasi za Adventure na Saratoga jijini Mwanza niliona kituko cha kumalizia mwezi wa Julai, 2018 kutoka kwa kaka ambaye alijigamba kuwa ni mkurya na kweli lafudhi yake ni ya kabila la kikurya.

Kaka huyu ambaye alikuwa maeneo hayo ya ofisi waligombana na mwenzake (wote 2 wanaonekana shughuli zao sio mbali na ofisi hizo). Katika ugomvi huo yule kaka mwingine ambaye sio mkurya akamtukana yule mkurya tusi la kuhusu viungo vya siri vya mama yake mzazi, tusi ambalo wengi wanapenda kulitumia.

Kaka mkurya, alighadhibika sana kusikia tusi lile. Hapo pembeni alikuwepo muuza kahawa, amewasha jiko la mkaa na juu yake kabandika birika la chuma anachemsha kahawa kwa ajili ya wateja wake ambao walikuwa wamekaa kwenye benchi wakiwa wanaongea story zao hasa za kuhusu mheshimiwa Waitara kujivua ubunge.

Ghafla kaka yule mkurya aliyetukaniwa mama yake, akaepua lile birika la kahawa, AKACHOTA MKAA KWA MIKONO YAKE, AKAUSHIKA ULE MKAA MIKONONI KWA SEKUNDE KADHAA, HALAFU KILICHOFUATA AKAMFUATA YULE ALIYEMTUKANA, AKAMGANDAMIZIA ULE MKAA MGONGONI MWAKE, yaan sio kwamba alimrushia ule mkaa bali aliushikilia na kumgandamizia yule mgomvi wake mgongoni kwa mikono yake kwa sekunde nyingi!!!

Du! wateja waliokuwa wanakunywa kahawa walitimua mbio (wanaume wa Mwanza).

Nahuja mie nikasema hapa sitoki hadi nione mwisho wake, hapo kumbuka wanaume wamekimbia pamoja na muuza kahawa. Basi yule aliyekuwa anachomwa alipiga kelele za kuomba msaada lakini hakuna aliyemsogelea aliyekuwa ameshika moto nikiwemo na mimi.

Nililala usiku naota ndoto mbaya ya lile tukio.
Picha ziko wapi?
 
😛😛😛😛 Watu wana hayo "machatu" kiasi kwamba hata akivaa ana namna ya kulilaza ili likae vyema kwenye boksa. hahahahahahah
[emoji3] [emoji3] [emoji3] [emoji3] [emoji3] ngoja nikae kimya nitafakari tukio la mkurya
 
Back
Top Bottom