Huyu kaka kabila la Mkurya alinishangaza!!!!

Huyu kaka kabila la Mkurya alinishangaza!!!!

Duuuuu....! Sisi wakurya ni wapole sana mtoa mada anatusingizia
 
NAHUJA Kuna mwingine mwanaume wa dar lakini anafungulia kiganja soda/bia sasa sijui ungekua unazimia ukienda nae bar!.
 
Jana nikiwa kwenye ofisi za kampuni za mabasi za Adventure na Saratoga jijini Mwanza niliona kituko cha kumalizia mwezi wa Julai, 2018 kutoka kwa kaka ambaye alijigamba kuwa ni mkurya na kweli lafudhi yake ni ya kabila la kikurya.

Kaka huyu ambaye alikuwa maeneo hayo ya ofisi waligombana na mwenzake (wote 2 wanaonekana shughuli zao sio mbali na ofisi hizo). Katika ugomvi huo yule kaka mwingine ambaye sio mkurya akamtukana yule mkurya tusi la kuhusu viungo vya siri vya mama yake mzazi, tusi ambalo wengi wanapenda kulitumia.

Kaka mkurya, alighadhibika sana kusikia tusi lile. Hapo pembeni alikuwepo muuza kahawa, amewasha jiko la mkaa na juu yake kabandika birika la chuma anachemsha kahawa kwa ajili ya wateja wake ambao walikuwa wamekaa kwenye benchi wakiwa wanaongea story zao hasa za kuhusu mheshimiwa Waitara kujivua ubunge.

Ghafla kaka yule mkurya aliyetukaniwa mama yake, akaepua lile birika la kahawa, AKACHOTA MKAA KWA MIKONO YAKE, AKAUSHIKA ULE MKAA MIKONONI KWA SEKUNDE KADHAA, HALAFU KILICHOFUATA AKAMFUATA YULE ALIYEMTUKANA, AKAMGANDAMIZIA ULE MKAA MGONGONI MWAKE, yaan sio kwamba alimrushia ule mkaa bali aliushikilia na kumgandamizia yule mgomvi wake mgongoni kwa mikono yake kwa sekunde nyingi!!!

Du! wateja waliokuwa wanakunywa kahawa walitimua mbio (wanaume wa Mwanza).

Nahuja mie nikasema hapa sitoki hadi nione mwisho wake, hapo kumbuka wanaume wamekimbia pamoja na muuza kahawa. Basi yule aliyekuwa anachomwa alipiga kelele za kuomba msaada lakini hakuna aliyemsogelea aliyekuwa ameshika moto nikiwemo na mimi.

Nililala usiku naota ndoto mbaya ya lile tukio.
Duuuu hapana so kwa hasira hizo kushika mkaa wa moto
 
Mwaka 2005 nilipokuwa namalizia form4 Tarime Secondary, siku hiyo tupo Buhemba tunapiga piga stori na wana mida ya saa moja jion wakaja wakurya wawili wanalumbana, kumbe wanalumbania kipande cha spring ya gari, huyu mmoja akidai ni chake huyu mwingine hataki kumpa, sasa sauti zikawa kubwa katika kulumbana kwao. Kidogo, yule aliyekuwa na kile chuma akampiga nacho kiunon mpaka tukasikia mshindo kutoka kiunoni, mpigwaji akatoa ukelele wa uchungu akamwambia narud Muraa. Jomba aliyepigwa alirudi na chupa za kutosha, akaanza kuzirushia mbali kuelekea aliko mbaya wake. Watu tulisambaa center nzima kila mtu akikimbia kujinusuru.

Analolizungumza Nahuja hata sishangai
 
Jana nikiwa kwenye ofisi za kampuni za mabasi za Adventure na Saratoga jijini Mwanza niliona kituko cha kumalizia mwezi wa Julai, 2018 kutoka kwa kaka ambaye alijigamba kuwa ni mkurya na kweli lafudhi yake ni ya kabila la kikurya.

Kaka huyu ambaye alikuwa maeneo hayo ya ofisi waligombana na mwenzake (wote 2 wanaonekana shughuli zao sio mbali na ofisi hizo). Katika ugomvi huo yule kaka mwingine ambaye sio mkurya akamtukana yule mkurya tusi la kuhusu viungo vya siri vya mama yake mzazi, tusi ambalo wengi wanapenda kulitumia.

Kaka mkurya, alighadhibika sana kusikia tusi lile. Hapo pembeni alikuwepo muuza kahawa, amewasha jiko la mkaa na juu yake kabandika birika la chuma anachemsha kahawa kwa ajili ya wateja wake ambao walikuwa wamekaa kwenye benchi wakiwa wanaongea story zao hasa za kuhusu mheshimiwa Waitara kujivua ubunge.

Ghafla kaka yule mkurya aliyetukaniwa mama yake, akaepua lile birika la kahawa, AKACHOTA MKAA KWA MIKONO YAKE, AKAUSHIKA ULE MKAA MIKONONI KWA SEKUNDE KADHAA, HALAFU KILICHOFUATA AKAMFUATA YULE ALIYEMTUKANA, AKAMGANDAMIZIA ULE MKAA MGONGONI MWAKE, yaan sio kwamba alimrushia ule mkaa bali aliushikilia na kumgandamizia yule mgomvi wake mgongoni kwa mikono yake kwa sekunde nyingi!!!

Du! wateja waliokuwa wanakunywa kahawa walitimua mbio (wanaume wa Mwanza).

Nahuja mie nikasema hapa sitoki hadi nione mwisho wake, hapo kumbuka wanaume wamekimbia pamoja na muuza kahawa. Basi yule aliyekuwa anachomwa alipiga kelele za kuomba msaada lakini hakuna aliyemsogelea aliyekuwa ameshika moto nikiwemo na mimi.

Nililala usiku naota ndoto mbaya ya lile tukio.
Ulipoamka ukakuta umejikojolea
 
Muraaa hawapendi maskhara kbs,
Kuna siku moja mkurya alikuwa kainama sasa mstari wa bonde matako ukawa nje!
Kuna jamaa akamtania oyooo muraaa mbona unaacha mali nje!wengine tukiona ivyo hali inabadilika.
Aroo mkurya aliinuka na kisu akaishindilia hapo kifuani kwa jamaa na muvi ndo ikaishia hapo
Waoga tuu
 
Hawa wakurya ndivyo walivyo,ukimuudhi ugomvi hauishi kirahisi hata ipite miaka minane.....wakimaindi wanaweza kukata hata miguu ya ng'ombe yote zizini
Kinachonipa mashaka ni hawa wakurya wa dar kina Mwita waitara wasiojielewa kama wakurya wa Tarime
 
Wakuria hatutaki dharau,fanya yote ila dharau kwetu ni mwiko,tunang'oa roho ya mtu kwa sekunde
Siku moja nilishuhudia kitu cha ajabu sana,kuna jirani yangu mkurya alimpeleka mwanae kwa bibi yake huko tarime dogo akiwa na miaka 3,dogo akaishi huko kwa muda wa miaka 2,baba yake akaenda likizo akarudi naye.
Siku kama mbili hivi toka dogo arudi ,tulikuwa tunapiga stori nje nyumbani kwao ,dogo alikuwa anacheza na wenzie mtaani ,nadhani akagombana na mwenzie akapewa kichapo,tulimuona dogo anarudi mbio analia ,moja kwa moja ndani akatoka na panga anakimbia kurudi huko alikopigwa ,yaani bila kumkimbiza na kumnyang'anya panga sijui ingekuwaje.
 
Back
Top Bottom