Huyu kanichosha

Huyu kanichosha

EINSTEIN112

JF-Expert Member
Joined
Oct 26, 2018
Posts
21,711
Reaction score
35,644
Naitwa Mr. Brian (Sio jina langu halisi). Umri wangu ni miaka 35 kwa sasa. Nilioa miaka mitano iliyopita na mke wangu hivi sasa anayo miaka 28.

Kusema kweli naipenda familia yangu na kama mwanaune najitahidi sana kuihudumia. Nyumbani kwangu tunao mabinti wawili wa kazi. Mmoja kwa ajili ya kusaidia kazi za ndani na mwingine kusaidia kulea watoto wetu mapacha wenye umri wa miaka miwili hivi sasa.

Pamoja na yote nayojitahidi kumtimizia mke wangu, yeye amekuwa mtu ambaye hatimizi majukumu yake kama mke.

Amekuwa na ile aina ya maisha ya mitandaoni, kwanza ni mtu wa kushinda sana Instagram, facebook, Watsapp, Snapchat na Jamii Forums

Katika Page zote za Umbea umbea, page za maeneo ya starehe, hoteli za hadhi hakosekani. Hana muda kabisa wa kunipikia chakula, kunifulia nguo na kazi nyingine zote wanafanya wadada wa kazi.

Nilimtafutia kazi katika kampuni fulani, alifanya kazi miezi miwili tu na kuacha maelezo yake eti mshahara ni mdogo mno ukilinganisha na elimu yake. Kumbe aliniongepea kwani ukweli ni kwamba alifukuzwa kutokana na uzembe kazini.

Sikuona tabu, nikamfungulia duka la bidhaa za nyumbani (mini-shop), lakini biashara hata ikawa haistawi, nilivyofanya uchunguzi nikaja kugundua kuwa sababu ni lugha yake mbovu kwa wateja kiasi ya kwamba ilikuwa haipiti siku bila kugombana na wateja kadhaa jambo lililofanya wateja kukimbia.

Nimechukua maamuzi mara kadhaa ya kumrudisha kwao lakini amekuwa akilia na kudai nimsamehe atajirekebisha lakini wapi, hubadilika muda mfupi na kurudi kwenye ujinga wake.

Jambo kubwa ambalo limefanya mpaka uvumilivu unishinde ni hili; Juzi kati kuna fedha Milioni mbili na nusu niliipata baada ya kuuza mazao yangu, kwa kuwa ile fedha nilipewa cash na ilikuwa siku ya Jumamosi usiku nikaazimia Jumapili baada ya kutoka Kanisani nakaiweke benki kupitia Wakala wa Fahari Huduma.

Kumbe mwenzangu aliziona, akachukua na kwenda kununua furniture, Oven, Friji na vikolombwezo vingine kwa ajili ya kumpa rafiki yake ambaye alikuwa anafanyiwa kitchen party Wiki iliyokua inafuata. Nilipomuuliza akawa akinipa stori za alufu ulela ulela. Hazina miguu wala mikono.

Nafikiri sasa nimechoka rasmi, hapo sijazungumzia masuala ya kunyimwa unyumba. Nafikiria Kutalakiana nae. Maana nahisi muda wowote naweza nikafa kwa pressure nikaacha wanangu bado wadogo.

Je , niko sahihi kwa maamuzi ya kumpa talaka nilee tu watoto mwenyewe maana sioni msaada wowote!
IMG-20190512-WA0003.jpeg
 
Huyo pichani ndo mkeo au huo Ni mfano tu
Sorry kwa kutoka nje ya maada chief
Mambo Kama haya ndo maana dakika ya mwisho nasemaga sitakuja h kuoa nitaishi single Kama yesu masiah.mbona hakuwa hata na uhusiano na mwanamke Wala hakujibebesha majukumu lakini amekufa akiwa most succesfull man in the history.
 
Huyo pichani ndo mkeo au huo Ni mfano tu
Sorry kwa kutoka nje ya maada chief
Mambo Kama haya ndo maana dakika ya mwisho nasemaga sitakuja h kuoa nitaishi single Kama yesu masiah.mbona hakuwa hata na uhusiano na mwanamke Wala hakujibebesha majukumu lakini amekufa akiwa most succesfull man in the history.
Hapana ni picha tu
 
Hii chai umeunga sukari au asali?
Naitwa Mr. Brian (Sio jina langu halisi). Umri wangu ni miaka 35 kwa sasa. Nilioa miaka mitano iliyopita na mke wangu hivi sasa anayo miaka 28.

Kusema kweli naipenda familia yangu na kama mwanaune najitahidi sana kuihudumia. Nyumbani kwangu tunao mabinti wawili wa kazi. Mmoja kwa ajili ya kusaidia kazi za ndani na mwingine kusaidia kulea watoto wetu mapacha wenye umri wa miaka miwili hivi sasa.

Pamoja na yote nayojitahidi kumtimizia mke wangu, yeye amekuwa mtu ambaye hatimizi majukumu yake kama mke.

Amekuwa na ile aina ya maisha ya mitandaoni, kwanza ni mtu wa kushinda sana Instagram, facebook, Watsapp, Snapchat na Jamii Forums

Katika Page zote za Umbea umbea, page za maeneo ya starehe, hoteli za hadhi hakosekani. Hana muda kabisa wa kunipikia chakula, kunifulia nguo na kazi nyingine zote wanafanya wadada wa kazi.

Nilimtafutia kazi katika kampuni fulani, alifanya kazi miezi miwili tu na kuacha maelezo yake eti mshahara ni mdogo mno ukilinganisha na elimu yake. Kumbe aliniongepea kwani ukweli ni kwamba alifukuzwa kutokana na uzembe kazini.

Sikuona tabu, nikamfungulia duka la bidhaa za nyumbani (mini-shop), lakini biashara hata ikawa haistawi, nilivyofanya uchunguzi nikaja kugundua kuwa sababu ni lugha yake mbovu kwa wateja kiasi ya kwamba ilikuwa haipiti siku bila kugombana na wateja kadhaa jambo lililofanya wateja kukimbia.

Nimechukua maamuzi mara kadhaa ya kumrudisha kwao lakini amekuwa akilia na kudai nimsamehe atajirekebisha lakini wapi, hubadilika muda mfupi na kurudi kwenye ujinga wake.

Jambo kubwa ambalo limefanya mpaka uvumilivu unishinde ni hili; Juzi kati kuna fedha Milioni mbili na nusu niliipata baada ya kuuza mazao yangu, kwa kuwa ile fedha nilipewa cash na ilikuwa siku ya Jumamosi usiku nikaazimia Jumapili baada ya kutoka Kanisani nakaiweke benki kupitia Wakala wa Fahari Huduma.

Kumbe mwenzangu aliziona, akachukua na kwenda kununua furniture, Oven, Friji na vikolombwezo vingine kwa ajili ya kumpa rafiki yake ambaye alikuwa anafanyiwa kitchen party Wiki iliyokua inafuata. Nilipomuuliza akawa akinipa stori za alufu ulela ulela. Hazina miguu wala mikono.

Nafikiri sasa nimechoka rasmi, hapo sijazungumzia masuala ya kunyimwa unyumba. Nafikiria Kutalakiana nae. Maana nahisi muda wowote naweza nikafa kwa pressure nikaacha wanangu bado wadogo.

Je , niko sahihi kwa maamuzi ya kumpa talaka nilee tu watoto mwenyewe maana sioni msaada wowote!View attachment 1094860
 
Naitwa Mr. Brian (Sio jina langu halisi). Umri wangu ni miaka 35 kwa sasa. Nilioa miaka mitano iliyopita na mke wangu hivi sasa anayo miaka 28.

Kusema kweli naipenda familia yangu na kama mwanaune najitahidi sana kuihudumia. Nyumbani kwangu tunao mabinti wawili wa kazi. Mmoja kwa ajili ya kusaidia kazi za ndani na mwingine kusaidia kulea watoto wetu mapacha wenye umri wa miaka miwili hivi sasa.

Pamoja na yote nayojitahidi kumtimizia mke wangu, yeye amekuwa mtu ambaye hatimizi majukumu yake kama mke.

Amekuwa na ile aina ya maisha ya mitandaoni, kwanza ni mtu wa kushinda sana Instagram, facebook, Watsapp, Snapchat na Jamii Forums

Katika Page zote za Umbea umbea, page za maeneo ya starehe, hoteli za hadhi hakosekani. Hana muda kabisa wa kunipikia chakula, kunifulia nguo na kazi nyingine zote wanafanya wadada wa kazi.

Nilimtafutia kazi katika kampuni fulani, alifanya kazi miezi miwili tu na kuacha maelezo yake eti mshahara ni mdogo mno ukilinganisha na elimu yake. Kumbe aliniongepea kwani ukweli ni kwamba alifukuzwa kutokana na uzembe kazini.

Sikuona tabu, nikamfungulia duka la bidhaa za nyumbani (mini-shop), lakini biashara hata ikawa haistawi, nilivyofanya uchunguzi nikaja kugundua kuwa sababu ni lugha yake mbovu kwa wateja kiasi ya kwamba ilikuwa haipiti siku bila kugombana na wateja kadhaa jambo lililofanya wateja kukimbia.

Nimechukua maamuzi mara kadhaa ya kumrudisha kwao lakini amekuwa akilia na kudai nimsamehe atajirekebisha lakini wapi, hubadilika muda mfupi na kurudi kwenye ujinga wake.

Jambo kubwa ambalo limefanya mpaka uvumilivu unishinde ni hili; Juzi kati kuna fedha Milioni mbili na nusu niliipata baada ya kuuza mazao yangu, kwa kuwa ile fedha nilipewa cash na ilikuwa siku ya Jumamosi usiku nikaazimia Jumapili baada ya kutoka Kanisani nakaiweke benki kupitia Wakala wa Fahari Huduma.

Kumbe mwenzangu aliziona, akachukua na kwenda kununua furniture, Oven, Friji na vikolombwezo vingine kwa ajili ya kumpa rafiki yake ambaye alikuwa anafanyiwa kitchen party Wiki iliyokua inafuata. Nilipomuuliza akawa akinipa stori za alufu ulela ulela. Hazina miguu wala mikono.

Nafikiri sasa nimechoka rasmi, hapo sijazungumzia masuala ya kunyimwa unyumba. Nafikiria Kutalakiana nae. Maana nahisi muda wowote naweza nikafa kwa pressure nikaacha wanangu bado wadogo.

Je , niko sahihi kwa maamuzi ya kumpa talaka nilee tu watoto mwenyewe maana sioni msaada wowote!View attachment 1094860
Oa mmoja wa hao house girls..
 
Back
Top Bottom