Huyu kijana Goodlucky Gosbert anajua sana

Haha kuna ule wimbo wake unaitwa Mimi ni muujiza kama sikosei, kuna sehemu anaimba na mdada hivi ana lishepu kama lotee halafu amevaa suruali ya jeans imembanaa basi yule dada hakuna anachofanya zaidi ya kujigeuza geuza kuonyesha shepu lake....nikiangaliaga aibu huwa naona mimi
kabadilika sana hadi havutii tena
 
waimbaji wa dini siku hizi wanaimba bongo fleva
 
Naomba jinsi ya kubarikiwa kwa kusikiliza wimbo wa kidini. Naona kila mtu anasema wimbo umembariki.
 
Mkuu kwann umechagua kuwaumiza wenzako kihisia na kiroho. Utaki wabarikiwe ?
 
Sasa hii inatofauti gani nasi tukisema hakuna bongo flava tamu kama iliorekodiwaga na P.Funk majani iliokuwa imesheheni ujumbe na ala za kusisimua. Ila haimaanishi kwamba bongo flava ya sasa ya kina Wasafi ni nzuri sana au mbaya ni kwamba zama zimebadilika. Gospel za mistari ya bibilia sahivi hazina mvuto ndio maana tumeamia kwenye Sweet Gospel za akina Joel Lwaga, Mercy Masika, Goodluck Gosbert, Angel Benard na kiukweli zinanibamba mno japo mie ni muislam kiasili.
 
Sasa jamaa ana shida gani mbona yupo smart tu mzee baba, au ulitaka avae suti za Lesi Wanyika na Tai pana kama Panga ndio awe na muonekano wa mcha mungu?
 
Me napenda nyimbo zake ila kuna style fulani hivi anaongea siipendi kabisa..in short sielewi kwa nn anaongea hivo yaan mkenya si mkenya dah...apunguze
Hio si ni effect ya studio, inaitwa "auto tune" inaremba sauti tu ila sometime ikizidi ndio inakera!
 
To me naangalia ujumbe na staili ya uimbaji. Lengo la kuimba ni nini? Jibu lipo ktk staili unayoimbia...hivi mwangalie muimbaji anachoimba na maisha yake anayoishi.....unakuta mtu anachokiimba hakiishi ila anaburudisha tu. Nafkiri ktk misingi ya uimbaji nyimbo za kikristo siyo kuburudisha bali ni kuhubiri kupitia uimbaji.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…