Huyu mchungaji anayedharau walimu na kudhalilisha waumini akemewe

Huyu mchungaji anayedharau walimu na kudhalilisha waumini akemewe

JFMemba

Senior Member
Joined
Jun 28, 2021
Posts
134
Reaction score
247
Nimeona video ya huyu dada ambaye anaonekana kuwa ni mchungaji akiwa anahubiri kanisani. Jambo lililonisikitisha ni kitendo cha kudharau taaluma ya ualimu hasa walimu wa kike wa shule za Msingi.

Kiongozi ni kioo cha jamii hivyo inatarajiwa kuwa maneno unayoyatoa yatakuwa ya kujenga na si kubomoa au kudhalilisha. Ajabu ni kuwa mchungaji huyo ambaye amesahau kabisa fadhila ya elimu aliyopewa na walimu hadi leo anaweza kusimama na kuhutubia watu malipo yake anatolea mfano usiofaa.

Dada huyo kaenda mbali zaidi kumdhalilisha muumini kwa kutaka kumpaka lipstick kanisani akiamini wanaofanya hivyo ndio huolewa. Hajui muumini huyo kama kaolewa au la. Hizi style za mahubiri zinakoelekea sio kwema kabisa. Imagine mme wa yule dada aliyedhalilishwa angekuwa pale church au yule dada angeamua kutoa unyonge si angemchapa ngumi na kusepa zake.

Tuwe tunachagua maneno ya kuhubiri na sio kuwadhalilisha watu wengine.

Natarajia TUCTA na CWT hata viongozi wa serikali watakemea tabia hii


 
Yeye mwenyewe sura yake ni kama dume kaniuzi sana huyu mchungaji atumie jukwaa lile lile kuomba walimu radhi la sivyo tunahama kanisa lake
 
Mchungaji wa mchongo
Sijapendaaaaa

Kwanini atuseme sisi tunaochana nywele?
Bagia njoo tuambizane hapa tunapata wapi vi peruvian hata vya mchongo Carleen

Nikijiangalia kwa huu mwaka lipstick nilipaka tu mara moja sababu ya sherehe sina hamu na huyo mchungaji 🤣🤣🤣🤣


Shost Lenie najua hujatinda nyusi 🤣🤣
Haya kesho chap chap 😂😂😂
 
Sijapendaaaaa

Kwanini atuseme sisi tunaochana nywele?...
Atasababisha wadada wa watu washindwe kwenda church kisa hawana lipstick au waende kwa kujishtukia.

Kanisani watu wanafata neno la uzima na wokovu, muhimu mtu aende smart kwa namna yake inatosha.

Mbona wengine tuko zetu nachuro na tunapeeeendwa adi tunapendwa tena😂

Nyusi sitindi tuone kama nitaachika au sitaenda mbinguni 🤣🤣🤣
 
Hii video kwangu inakatia njiani inafeli kudisplay
 
Kuna watu jumapili wanaaga wanaenda kanisani wanaingia hapo.

Na wenyewe wanaitikia kabisa Ameeen na sadaka heavy wanatoa.

Aseee inatia huruma kanisa kama hall la taarabu na mchungaji ndio isha mashauzi full michambo dadekiiii.
 
Bahati mbaya zaidi kuna watu wamekaa wanamsikiliza na kuitikia ameen.

Hovyo kabisa
 
Wengi mmetoa mapovu nadhani kwasababu hamna hela au ndio hao walimu wa shule ya msingi.

Huyo mchungaji lengo lake ni kuwajulisha mabinti wakae katika mvuto wa kupendeza na kumvutia mwanaume ili wapate waume.. sio wakae kishambashamba.

#MaendeleoHayanaChama
 
Kwani mdada kuhudhuria 'nyumba ya Mungu' lazima apake lipstick n.k.?
 
Wengi mmetoa mapovu nadhani kwasababu hamna hel au ndio hao walimu wa shule ya msingi.

Huyo mchungaji lengo lake ni kuwajulisha mabinti wakae katika mvuto wa kupendeza na kumvutia mwanaume ili wapate waume..sio wakae kishambashamba.

#MaendeleoHayanaChama
Mkuu mbona wengi tu kina Mgogo hutoa mahubiri ya namna hiyo ila hawatoi mifano ya kudhalilisha kada fulani au kuwadhalilisha waumini
 
Back
Top Bottom