Huyu mchungaji anayedharau walimu na kudhalilisha waumini akemewe

Huyu mchungaji anayedharau walimu na kudhalilisha waumini akemewe

Maticha wamevurugwa usishangae kumuona ticha katwanga pigo private

Waalimu Wana miongozo yao ya kuvaa. Mmoja wa miongozo mwalimu wa kike hatakiwi kuvaa suruali au nguo ya kubana. Sasa baadala ya kuwalaumu walimu nenda ukailaumu wizara ya elimu.

Halafu mahuburi ya kuonesha kundi la watu fulani halifai huo ni ujinga. Mambo ya mavazi ni personal choice. Mbona wanawake wa kiislamu wengi huenda msikitini wamejivika kanga?. Tusilazimishe lifestyle ya njee ikaingia kanisani.
 
Nimeona video ya huyu dada ambaye anaonekana kuwa ni mchungaji akiwa anahubiri kanisani. Jambo lililonisikitisha ni kitendo cha kudharau taaluma ya ualimu hasa walimu wa kike wa shule za Msingi.

Kiongozi ni kioo cha jamii hivyo inatarajiwa kuwa maneno unayoyatoa yatakuwa ya kujenga na si kubomoa au kudhalilisha. Ajabu ni kuwa mchungaji huyo ambaye amesahau kabisa fadhila ya elimu aliyopewa na walimu hadi leo anaweza kusimama na kuhutubia watu malipo yake anatolea mfano usiofaa.

Dada huyo kaenda mbali zaidi kumdhalilisha muumini kwa kutaka kumpaka lipstick kanisani akiamini wanaofanya hivyo ndio huolewa. Hajui muumini huyo kama kaolewa au la. Hizi style za mahubiri zinakoelekea sio kwema kabisa. Imagine mme wa yule dada aliyedhalilishwa angekuwa pale church au yule dada angeamua kutoa unyonge si angemchapa ngumi na kusepa zake.

Tuwe tunachagua maneno ya kuhubiri na sio kuwadhalilisha watu wengine.

Natarajia TUCTA na CWT hata viongozi wa serikali watakemea tabia hii


View attachment 2244659
...Mkuu, hujatuambia alichosema! Umelalamika TU! Alisemaje?...
 
Kama kweli huyu Ni mchungaji na kuna waumini wataendelea kwenda kumsikiliza watakuwa waajabu itokee ndio nimehudhuria hiyo ibaada ningekatisha kwa kweli hakuna mahubiri ya hivyo huyo atakuwa Ni kungwi wa makahaba na sio mchungaji. Hapo hajadhalilisha walimu na huyo mdada tu kawadhalilisha wachingaji wote ulimwenguni
 
Mimi mwenyewe ni mchungaji na hiyo clip nimeiona kwakweli siyo nzuri ila tunaifanyia kazi huyu mtumishi hakutumia hekima kabisa katika mahubiri yake.

Maana mtumishi unapo hubiri neno la Mungu tunatarajia katika kinywa chako kutoke maneno ya kufariji, kuponya, kujenga, kupatanisha, matumaini, na kuelimisha watu ila katika maadlili mema ya mpendezayo Mungu, na siyo maneno ya kashfa na fadhaa kama aliyoyatamka yeye.

Sent from my TECNO B1f using JamiiForums mobile app
 
Kama ningekua Hugo mwanamke ningempiga kofi moja la uso nikawe maarufu, unaona kabisa roho Wa Mungu hayumo ndani mwake.
 
Nimeona video ya huyu dada ambaye anaonekana kuwa ni mchungaji akiwa anahubiri kanisani. Jambo lililonisikitisha ni kitendo cha kudharau taaluma ya ualimu hasa walimu wa kike wa shule za Msingi.

Kiongozi ni kioo cha jamii hivyo inatarajiwa kuwa maneno unayoyatoa yatakuwa ya kujenga na si kubomoa au kudhalilisha. Ajabu ni kuwa mchungaji huyo ambaye amesahau kabisa fadhila ya elimu aliyopewa na walimu hadi leo anaweza kusimama na kuhutubia watu malipo yake anatolea mfano usiofaa.

Dada huyo kaenda mbali zaidi kumdhalilisha muumini kwa kutaka kumpaka lipstick kanisani akiamini wanaofanya hivyo ndio huolewa. Hajui muumini huyo kama kaolewa au la. Hizi style za mahubiri zinakoelekea sio kwema kabisa. Imagine mme wa yule dada aliyedhalilishwa angekuwa pale church au yule dada angeamua kutoa unyonge si angemchapa ngumi na kusepa zake.

Tuwe tunachagua maneno ya kuhubiri na sio kuwadhalilisha watu wengine.

Natarajia TUCTA na CWT hata viongozi wa serikali watakemea tabia hii


View attachment 2244659
kwanza yeye mwenye hapaswi kusimama mbele kuhubiri. Amekosa sifa anamipasho kama waimba taarabu!. Na wanaoshangilia huenda waoga, hawajuwi au wanajipendekeza.
 
Mtu mishi anacheza na minds za wanawake.
Mwanamke hapendwi kwa makorokoro ila anapendwa kwa vile alivyo smart na vile anajiheshmu na kusimamia mambo yake.
Wanawake wetu wanajipamba wakitoka ila si wakiwa ndani so hayo mapambo si kwetu ila kwa watu wa nje ambao wanaishia kuwataman tu ila si kuwa na upendo nao
 
Back
Top Bottom